Posts

Showing posts from June, 2026

HALMASHAURI WILAYA YA MBEYA BALAA WATUA UNGUJA KUJIFUNZA MBINU MPYA

Image
     Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline,                 UNGUJA   Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya katika kuongeza jitihada za kuweza kuongeza ufanisi mkubwa  katika saula zima la uwajibikaji na kujinza mambo mbali mbali imeamua  kwenda kufanya ziara maalumu ya  kikazi Zanibar katika visiwa vya eneo la  Unguja ambayo itaweza  kuwasaidia watendaji pamoja na madiwani katika kuongeza weledi na utekelezaji wa majukumu yao mbali mbali ya kila siku.   Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Mbeya  Bi. Erica Yegella amebainisha kwamba katika ziara hiyo wameambatana  na baadhi ya watendaji pamoja na  madiwani mbali mbali  kwa lengo la kuweza  kwenda kujifunza  mafunzo mbali mbali kwa kioindi cha siku nne ambayo yataweza kuwasaidia katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao ya kikazi ya kila siku. Yegella amesema kwamba  lengo kubwa la Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia...

WATANZANIA WATAKIWA KUACHA KUSIKILIZA WANASIASA NA WANAHARAKATI WANAOCHOCHEA VURUGU

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline            DAR ES SALAAM  WATANZANIA wameaswa kuacha kusikiliza wanaharakati na wanasiasa wanaochochea vurugu na uvunjifu wa amani nchini, kwa kuwa watu hao hawana nia njema kwa taifa. Rai hiyo imetolewa  Juni 4, mwaka jijini Dar es Salaam na mwanafalsafa wa Pan-Afrika kutoka Zimbabwe, Dkt. Joshua Maponga, wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliohusu uzinduzi wa makala inayozungumzia matukio yaliyojitokeza kabla na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.Makala hiyo imeandaliwa na kampuni ya African Spear Head Media. Dkt. Maponga alisema kuwa baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) yamekuwa yakipokea fedha kutoka mataifa ya nje kwa lengo la kuhamasisha vitendo vinavyokwenda kinyume na maadili na amani ya nchi, ikiwemo vurugu na migawanyiko kati ya wananchi na viongozi wao. Amesema hali hiyo ni hatari kwa ustawi na usalama wa taifa, hivyo akashauri Serikali kuchukua hatua za kufanya uhakiki wa ma...

TAKUKURU TEMEKE YAWAFIKISHA MAHAKAMANI WATUMISHI KWA WIZI WA TSH.169,617,529

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline         DAR ES SALAAM  TAASISI ya Kupambana na Rushwa Mkoa wa Temeke(TAKUKURU) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mashtaka,imewafikisha Mahakamani watumishi wa Halmashauri  hiyo na OR-TAMISEMI kwa tuhuma za wizi na ubadhirifu wa fedha kiasi cha shilingi 169,617,520 maarufu kama Fedha za BAKAA. Akizungumza na waandishi wa habari Juni 2,2026  Jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Temeke, Fransis Luena amesema watumishi waliofikishwa  mahakamani kwa makosa hayo kutoka OR-TAMISEMI DODOMA ni Annie Maugo-Afisa Hesabu Mwandamizi,Tumsifu Kachira-Afisa Hesabu Mwandamizi Daraja la na Aidan Mponzi-Afisa Hesabu Daraja la 1. Aidha ,amesema watumishi wengine  kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni ,Jonathan Manguli-Afisa Hesabu 1 na (MUSE),Godfrey Martiny-Mkuu wa Kitengo Cha Fedha na Uhasibu,Juvenalis Mauna-Mkuu wa Kitengo Cha Udhibiti Taka na Usafi wa Mazingira,Josephat Mutembei-Mhandisi,Bibiana Mde...

COSTECH COSTECH, WIPO KUKUZA MILIKI BUNIFU NCHINI .

Image
     Timothy Marko DmNews Online                 DAR ES SALAAM.  TAASISI  ya Miliki Bunifu Duniani (WIPO) Kwakushirikiana na Tume ya Sayansi Nchini (COSTECH) imezindua mpango Maalumu wa Uhamishaji wa Teknolojia kwa maendeleo ya Jamii.  Akizungumza Leo  Juni Mosi,2026 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Nchini (COSTECH) Dk Amos Nungu amesema kuwa Mradi huo unaangazia Teknolojia bunifu ambazo nisahihi kwa Mazingira ya Tanzania.  "Tunataasisiza utafiti kuhusiana na Mradi huu Utahusisha Mkoa wa Njombe kama Eneo la Mradi wa Majaribio"Amesema Mkurugenzi wa COSTECH  Dkt Amos Nungu DKt.Nungu Ameongeza kuwa Program hiyo inalenga kukuza  sekta ya Kilimo na Mifugo.  Amesisitiza kuwa takribani Teknolojia (15) zimeidhinishwa na taasisi hiyo kwa kushirikiana na Taasisi ya Miliki Bunifu Duniani (WIPO). "Hili nijambo kubwa tukifanikiwa tutaweza kuboresha miradi mbalimbal...