TRA YAJITOSA KUSAIDIA JAMII
Na Eliasa Ally DmNewsonline
IRINGA
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Iringa imeendelea kuonyesha mshikamano na jamii kwa kuwasaidia wagonjwa wasio na uwezo wa kulipia gharama za matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa.
Zoezi hilo limefanyika Juni 25, 2026, ikiwa ni sehemu ya shughuli zinazoendelea kuelekea maadhimisho ya miaka 30 tangu kuanzishwa kwa TRA.
Mkurugenzi wa idara ya fedha kutoka TRA Dinah Msuya amesema TRA wamekabidhi misaada mbalimbali ikiwemo malipo ya baadhi ya bili za matibabu kwa wagonjwa wenye uhitaji, pamoja na zawadi kwa wagonjwa na wauguzi wanaotoa huduma hospitalini hapo.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Dkt. Alfred Mwakalebela, ameipongeza TRA kwa hatua hiyo na kutoa wito kwa taasisi nyingine za umma na binafsi kuiga mfano huo kwa kuwasaidia wananchi wenye mahitaji mbalimbali, hususan katika sekta ya afya.
Nae mmoja wa wagonjwa walionufaika na msaada huo ameishukuru TRA kwa moyo wa kujitoa na kuwajali wananchi wenye changamoto za kifedha, akisema msaada huo umewapa matumaini na kupunguza mzigo mkubwa waliokuwa nao. 






Comments
Post a Comment