Posts

Showing posts from May, 2026

JESHI LA POLISI YA WASHIKILIA WATU 6 KWA TUHUMA KUKUTWA NA KICHWA CHA MTU

Image
  Timothy Marko DmNewsOnline           DAR ES SALAAM.  JESHI  la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema linamshikilia Said Ali (31) Mganga wa kienyeji nawengine( 5) kwa kukutwa na kichwa chamtu kinachodaiwa James Temba Mkaazi wa kitunda Wilaya ilala.  Akizungumza Leo May 13,2026 jijini Dar es Salaam Kamishina wa Kanda Maalumu CP.Murilo Jumanne Murilo amesema kuwa mnamo March 30 Mwaka huu jeshi hilo lilianza Uchunguzi wa Shauri hilo nakuwabaini watu sita ambao majina yao yamehifadhiwa kwa Uchunguzi zaidi akiwemo Mganga huyo kudaiwa kuhusika na tukio hilo.  "Tunawashikilia watu sita ikiwemo Mganga Said Ali maarufu SIDE kwakuhusika na shauri hilo,taratibu za kisheria zinaendelea kuhusiana na shauri hili" Amesema Kamishina wa Polisi Kanda Maalumu CP.Murilo Jumanne Murilo.  CP Murilo Ameongeza kuwa Nivyema Wananchi wakawa watulivu juu ya ufuatiliaji wa kichunguzi  kwa kushirikiana jeshi hilo na taasisi zingine zakiuchung...

TARURA BORESHENI BARABARA ZA KATA MAFINGA

Image
  Na Mwandishi wetu, DmNewsonline                     IRINGA Baraza la Madiwani la halmashauri ya mji Mafinga limeiomba wakala wa barabara wa mijini na vijijini (TARURA) Wilaya ya MufindI kuboresha Barabara katika kata za halmashauri hiyo ambazo nyingi ziliathiriwa na mvua nyingi iliyonyesha maeneo mbalimbali nchini. Maswali ya madiwani hayo yameulizwa wakati wakijadili taarifa za kamati za robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026, wakisema changamoto ya Barabara za kata imekuwa ni kubwa katika halmashauri hiyo hali inayokwamisha wananchi kufanya shughuli za maendeleo.  Akijibu hoja za madiwani hao meneja wa TARURA Wilaya ya Mufindi Muhandisi Nelson Maganga amesema kuwa serikali imejipanga kupeleka tabasamu kwa wananchi kwa kuboresha barabara ambazo hazipitiki huku akiwashauri madiwani kuridhia kuanza kuboresha kwa barabara ambazo zitakuwa na tija kwa watu wengi. Mwenyekiti wa halmashauri ya mji Mafinga Reginant Kivinge amewapo...

MAFINGA YAENDELEA KUNG’ARA UKUSAJI WA MAPATO YA VUKA LENGO KWA ASILIMIA 105

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                       IRINGA  HALMASHAURI  ya Mji Mafinga imefanikiwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kufikia asilimia 105 katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2025/2026. Mafanikio hayo yameelezwa katika kikao cha Baraza la Madiwani cha tathmini ya utekelezaji wa shughuli za robo ya tatu, ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Reginant Kivinge, amesema hatua hiyo imetokana na ushirikiano mzuri kati ya madiwani, wakuu wa idara pamoja na watendaji wa halmashauri waliotekeleza majukumu yao kwa weledi na uwajibikaji. Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji Mafinga, Fidelica Myovella, amesema halmashauri itaendelea kuzingatia maelekezo ya Serikali ikiwemo kujibu hoja za ukaguzi na kusimamia vizuri ufungaji wa hesabu ili kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya ndani. Naye Afisa Serikali za Mitaa kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa w...

KIBAHA MANISPAA KUCHUKUA HATUA YA KUKABILI CHANGAMOTO YA MAJI.

Image
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dkt .Mawazo Nicas akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani lililofanyika Mei 12/2026 katika jengo la Halmashauri hiyo na kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa Dkt.Rogers Shemwelekwa na wa kwanza Kulia ni Naibu Meya wa Manispaa Aziza Mruma. NaGustaphu Haule,DmNewsonline                      PWANI  BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha limepanga kuchukua hatua ya dharula ya kutatua  changamoto ya maji kwa kuchimba visima vya maji na kupeleka matenki ya maji katika Kata ambazo zimekuwa na changamoto kubwa ya ukosefu wa hudumal ya maji. Mbali na kutatua changamoto ya maji lakini pia baraza hilo limepanga kutatua changamoto ya barabara zake za ndani kwa  kuhakikisha wanaanza kujenga barabara hizo kwa kiwango cha lami japo kidogo kidogo. Mipango ya utatuzi wa changamoto hizo imefanyika katika kikao cha kikanuni cha Baraza la Madiwani lililofanyika Mei 12/2026 lililole...

RC MAKONGORO AIBUKA MSHINDI KUSHUHUDIA KOMBE LA DUNIA NCHINi CANADA

Image
 Na Angelina Mganga,DmNewsOnline          DAR ES SALAAM  MKUU wa Mkoa wa Rukwa ,Charles Makongoro Nyerere ametangazwa  kuwa mshindi kupitia  droo ya FIFA WORLD CUP 26 ,Fainali ndo Mpango naTemboCardVisa inayochezeshwa na Benki ya CRDB Katika droo hiyo wamepatikana washindi watatu waliojinyakulia TV Janja Smart  za nchi 85 pamoja na king'amuzi. Washindi  hao waliojinyakulia Tv  Janja ni Amina Kaswale Awadhi, Esther Dauson Kabakama na Lusekelo Michael Mwamwala. Makongoro ameibuka  mshindi katika droo hiyo  pamoja na wenzake wawili  kwenda nchini Canada kushuhudia Fainali za Kombe la Dunia. Akizungumza kwa njia ya simu na watangazaji wa droo hiyo Charles Makongoro Nyerere amewapongeza kwa kutoa huduma Bora kwa wateja wao na kuelezea furaha yake kwa kuwa miongoni mwa washindi waliopata fursa yakushuhudia  Fainali ya Kombe la Dunia. Naye Meneja Mwandimizi Kitengo cha Kadi CRDB Benki,Karington Chahe  amesema ...

WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA BIDHAA ZA BATTERIES ZINAZOZALISHWA NCHINI.

Image
Timothy Marko DmNews Online                                DAR ES SALAAM.  KATIKA kuhakikisha  Sekta ya Uwekezaji inakua kupia Sekta ya Viwanda,  Kampuni ya Izzo  Batteries imekuja kuwekeza Sekta ya Batteries za Magari na Mashine ilikuweza kuhakikisha Watanzania  wananufaika na Bidhaa zinazozalishwa hapa Nchini. Akizungumza Leo Mei,12 ,2026 Jijini Dar es Salaam  Meneja wa IZO Batteries  IZZO  Mahange amesema kuwa Bidhaa za Batteries  zinazozalishwa kwenye Kampuni hiyo zina dhamana ya miaka 10 ,Ambapo tayari Kampuni hiyo ina mawakala Takribani 150 Nchi nzima.  "Batteries zetu zinazozalishwa hapa nchini,tayari Kampuni yetu imezalisha Ajira takriban 50" Amesema Meneja Izzo  BATTERIES IZZO Mahange.  Naye balozi wa Kampuni hiyo Dotto Magari amesema kuwa Bidhaa hiyo ya Bettries Izzo zinaubora kwenye Mashine pamoja Magari, sambamba na Bajaji . "Hii ni furs...

SUBIRA MGALU :KAMATI TUMERIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA KAMPUNI HII YA ORYX ENERGIES,

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline              DAR ES SALAAM  MWENYEKITI wa kamati ya  Bunge Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo mkoani Pwani mh. Subira Mgalu amesema Serikali inatambua  mchango wa Sekta binafsi Nchini na ndio maana unaweka Mazingira wezeshi ya kufanya shughuli zao,huku wakiridhishwa na uwekezaji wa oryx Energies hapa Nchini. Mgalu ameyasema hayo  Mei 9, 2026 Jijini Dar es salaam baada ya kamati yake kufanya ziara ya kutembelea Kampuni ya Oryx Energies  ambapo wabunge wamepata nafasi ya kuona namna shughuli za uzalishaji bidhaa mbalimbali za Kampuni hiyo zinavyofanyika ikiwepo vilainishi na gesi ya kupikia majumbani. Mgalu amesema kamati inatambua mchango na uwekezaji uliofanywa na oryx energy na  katika kipindi Cha miaka minne imeweza kuchangia Pato la Taifa la shilingi Tilioni 1.2 na pia imetoa ajira za moja kwa moja  1000  na kwa  asilimia zaidi ya 90 ni vijana ...

WAJASIRIAMALI WADOGO STENDI YA MAGUFULI WAPATIWA VIZIMBA

Image
  Na Mwandishi wetu DmNewsOnline             DAR ES SALAAM  WAJASIRIAMALI wadogo wa Kituo cha Mabasi Stendi ya Magufuli Jijini Dar es Salaam wamekubali kurejea kwenye vizimba walivyopangiwa na uongozi wa stendi. Akizungumza na waandishi wa habari Mei 7,2026 Jijini hapo,John Shayo mmoja wa wafanyabiashara waliorejea kwenye vizimba  kwa niaba ya wenzake amesema kwamba wamekubali  maelekeo waliopewa na uongozi wa stendi hiyo "Sisi kama wafanyabiashara wadogo tuliokuwa tumeweka biashara zetu ndani ya stendi tumekubali maelekezo yaliyotolewa na uongozi kwamba turudi kwenye vizimba kisha huku tuje kwa ajili ya kufanya biashara za kubeba mikononi tu ",amesema Naye Mwenyekiti wa Jengo la Abiria,  Haruna Silanda amesema kurejea kwa wafanyabiashara wadogo kumeleta usawa na mivutano isiyo na tija ,hivyo analishukuru kundi hilo kukubali maelekezo yaliyotolewa na uongozi wa stendi na wameonyesha umoja na mshikamano umerejea. "Kwetu kama viongozi...

Kuelekea Siku ya Wauguzi Duniani mamia wazidi kujitokeza Garden kupima afya bure

Image
  Na Eliasa Ally,DmNewsonline                     IRINGA KATIKA  hali iliyojawa hamasa, mshikamano na upendo kwa jamii, viwanja vya Garden Manispaa ya Iringa vimegeuka kuwa kitovu cha matumaini baada ya kuanza rasmi kwa shughuli za utoaji bure wa huduma za afya kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wauguzi Duniani, Mei 12 mwaka huu.  Mamia ya wananchi wamejitokeza kupata huduma mbalimbali huku wakionesha furaha na matumaini mapya juu ya sekta ya afya. Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Iringa, Dk. Alfred Mwakalebela, amesema lengo la kupeleka huduma hizo katikati ya mji ni kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuondoa hofu iliyojengeka kwa baadhi ya watu kuhusu huduma za afya hospitalini. Dk. Mwakalebela amesema ni muhimu kwa jamii kuona kuwa wahudumu wa afya ni sehemu yao, watu wanaowajali na wanaotamani kuwaona wakiwa salama kiafya muda wote.  Amesema huduma hizo si tu tiba, bali...

DC MSANDO ATOA MAAGIZO KWA TANESCO NA TARURA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

Image
    Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline               DAR ES SALAAM  JESHI la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam limeungana na wazimamoto duniani kuadhimisha Siku hiyo katika maonesho yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam  Akizungumza katika Maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa  wa Dar es Salaam,Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Wakili Albert Msando ametoa maagizo kwa Jeshi la  Zimamoto na Uokoaji kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) pamoja na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini(TARURA) kuwa ujenzi wa  miundombinu ya Barabara na wale wanaounganisha umeme kuwa makini ili inapotokea majanga  ya moto iwe rahisi kuyadhibiti. Amesema  Zimamoto wanatakiwa kujiridhisha ubora wa vifaa vinavyotumika kuunganisha umeme kwenye  maeneo ya biashara,masoko na maduka wahakikishe vifaa hivyo viko salama,kama haviko salama aliyeunganisha huduma hiyo achukuliwe hatua za kisheria. ...

ZIMAMOTO WAONESHA UMAHIRI WAKUOKOA MGONJWA KUTOKA GHOROFA YA TISA

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline           DAR ES SALAAM  JESHI la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam limeungana kuadhimisha Siku ya Wazimamoto Duniani katika maonesho yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam  Jeshi Hilo limeonyesha matukio mbalimbali yanayohusisha shughuli za uokoaji ambapo katika hali isiyo ya kawaida kabisa,Askari mmoja ameonyesha umahiri wa  hali ya juu na wakuwavutia watazamaji. Maonesho hayo yalikuwa ya ukakamavu na uwezo wa haraka wa kukabiliana na dharura  kumuoko mgonjwa aliyekuwa katika ghorofa ya tisa ya jengo. Maadhimisho ya Siku ya Zimamoto Duniani yameonyesha umahiri mkubwa wa Jeshi