Posts

Showing posts from May, 2026

AHADI ZA CHAMA CHA MAKINI ZATIKISA ISIMANI WANANCHI KUPEWA MATREKITA 2 BURE KILA KATA

Image
  Na Eliasa Ally,DmNewsonline       IRINGA. ZIKIWA zmesalia siku tatu kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika Jimbo la Ismani kufutia kifo Cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo William lukuvi kufariki Dunia ,vyamba mbalimbali vimeendelea kunadi sera zake kwa wananchi. Katika kuhakikisha Chama Chama cha MAKINI  kimedhamiria kuchukua kikoba hiyo kimetoa ahadi kwa wananchi kuwa endapo kinampa kura Mbunge wao basi Kila kata ndani ya Jimbo hilo watapewa Trekta kwa ajili ya kilimo bure. Pia mgombea huyo amesema mbali na kutoa Trekta hizo lakini wananchi wataendelea kunufaika na suala la elimu bure kwa watoto wa familia za kawaida. Kauli hizo zilitolewa Mei 28, 2026 Katika mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika  Kijiji cha Mlowa, Kata ya Mlowa na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa Costa Kibonde, ambapo wananchi walijitokeza  kusikiliza sera za Chama hicho. "Chama chetu kupitia mgombea wetu huyu mkitupa ridhaa katika Jimbo hilo tu tatoa matrekta mawili kwa kila kata ndan...

ENDING MALARIA IS AN AFRICAN DEVELOPMENT PRIORITY

Image
Dm News Tz As Africa marks Africa Month and reflects on the ambitions of the African Union’s Agenda 2063, malaria experts are calling for malaria elimination to be viewed not only as a public health challenge, but as a critical development priority that will shape the continent’s resilience and future growth. Despite decades of progress, malaria continues to place significant pressure on African economies, education systems, and healthcare infrastructure. According to the WHO World Malaria Report 2025, Africa still carries the overwhelming majority of the global malaria burden, with children under five and vulnerable communities most affected. Beyond the immediate health impacts, repeated malaria infections continue to disrupt livelihoods, reduce productivity, and affect long-term educational outcomes across endemic countries. Adults often miss work multiple times a year due to illness, while children lose valuable school days, impacting learning and future opportunities. “The persiste...

ATE YABORESHA TUZO ZA MWAJIRI BORA 2026 KWA MFUMO MPYA WA UWAZI NA USHIRIKISHWAJI

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsTz Dar es salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Adv. Suzanne Ndomba-Doran amesema Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka 2026 (EYA) zimeboreshwa kwa mfumo mpya unaolenga kuongeza uwazi, ushirikishwaji na kuendana na mabadiliko ya dunia ya ajira. Akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa tuzo hizo, Adv. Ndomba-Doran alisema EYA imekuwa nguzo muhimu katika sekta ya ajira nchini kwa zaidi ya miaka 20 kwa kutambua taasisi zinazowekeza katika ustawi wa wafanyakazi, mazingira bora ya kazi na maadili ya biashara. “Leo si uzinduzi wa kawaida. Leo tunaandika ukurasa mpya katika historia ya EYA,” alisema. Alisema mwaka uliopita ATE ilisimamisha kwa muda utoaji wa tuzo hizo ili kufanya mapitio ya kina na kuhakikisha mfumo wake unaendana na mahitaji ya sasa ya waajiri na wafanyakazi. Kwa mujibu wa Adv. Ndomba-Doran, mapitio hayo yalihusisha wadau mbalimbali wakiwemo wanachama wa ATE, wataalamu na washauri wa sekta ya ajira, ambapo walipokea maoni yaliyotaka ...

TMA:JUNI HADI AGOSTI KUTAKUWA NA VIPINDI VYA BARIDI.

Image
  Timothy Marko DmNews Online                   DAR ES SALAAM.  MAMLAKA ya Hali ya Hewa Nchini Tanzania (TMA) imewatadharisha  Wananchi kuwa kutakuwa na Hali ya Baridi kwa kipindi cha Mwezi juni hadi Agosti mwaka huu. Akizungumza Leo Mei 25,2026 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  hali ya hewa Dkt.Ladislaus Chang'a amesema kuwa hali hiyo ya baridi itaambatana na Upepo mkali katika baadhi ya Maeneo ya nchi . "Mwelekeo wa Joto,hali ya baridi ya Wastani inatarajiwa katika Maeneo ya ziwa Victoria na kanda ya kusini ya nyanda za juu kusini, Nyanda za juu kusini ikijumuisha Mikoa ya Singida"Amesema Dkt.Chang'a  Dkt.Chang'a Ameongeza kuwa hali ya Joto kiasi na baridi ya wastani inatarajiwa kuikumba mikoa ya ukanda wa Pwani na Maeneo ya kaskazini sambamba na Maeneo ya Nchi kavu. Amesisitiza  kuwa Maeneo ya Nyanda za juu kaskazini ukanda wa Pwani kunatarajiwa kuwa na Baridi ya Wastani.  "Vipindi ...

JOWUTA YAZITAKA TAASISI,WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI KUWAANDIKISHA WANAHABARI WCF

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsTz Dar es salaam Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) kimezitaka taasisi na wamiliki wa vyombo vya habari nchini kuhakikisha wanawaandikisha wanahabari katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) pamoja na kuwapatia ajira zenye mikataba rasmi ili waweze kunufaika na haki na stahiki zao za msingi kazini. Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa mafunzo kuhusu fidia kwa wafanyakazi kwa wanachama wa JOWUTA, Mwenyekiti wa chama hicho, Mussa Juma Siwayombe amesema bado wanahabari wengi nchini wanafanya kazi bila ajira za kudumu wala mikataba, hali inayowanyima fursa ya kupata huduma muhimu za hifadhi ya jamii na fidia wanapopatwa na madhara yatokanayo na kazi zao. Amesema zaidi ya asilimia 70 ya wanahabari nchini hawana ajira rasmi jambo ambalo ni changamoto kubwa kwa ustawi wao na tasnia ya habari kwa ujumla, huku akisisitiza umuhimu wa umoja na mshikamano wa wafanyakazi katika kudai haki zao. Siwayombe amesema mafunzo hayo...

‘SIKU YA NYUKI DUNIANI’ YAADHIMISHWA KITAIFA TABORA

Image
             Na Allan Kitwe,DmNewsonline                 TABORA MAADHIMISHO ya Siku ya Nyuki Duniani yanayoyohusisha utundikaji mizinga, maonesho ya bidhaa na mazao nyuki yameanza leo katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Vita Mjini Tabora na kuvuta umati mkubwa wa wananchi. Wakizungumza kwenye maadhimisho hayo wakazi wa Tabora wameeleza kufurahishwa na tukio hilo kwa kuwa linawapa fursa wageni kutembelea Mkoa huo na kuonja utamu wa asali inayozalishwa katika misitu ya Mkoa huo. Daud Elisha, mjasiriamali mkazi wa Kata ya Kanyenye, Halmashauri ya manispaa ya Tabora ameeleza kuwa zao la asali ni miongoni mwa mazao ya kujivunia yanayozalishwa katika Mkoa huo na kuuzwa kwa bei kubwa ndani na nje ya nchi. ‘Haya maadhimisho ni fursa muhimu sana kwa wana Tabora kuuza asali yao na kupanua wigo wa uzalishaji zao hilo katika Wilaya zote za Mkoa huu, hivyo kuwaneemesha zaidi kiuchumi’, amesema. Amina Madereka, mjasiriamali anayeji...

MWENYEKITI WA SHIVYAWATA MATEMBA KUFUNGA NDOA JUNI 27,2026,ANAOMBA MCHANGO

Image
     Na Mwandiahi wetu,DmNewsOnline        DAR ES SALAAM  MWENYEKITI wa Shirikisho la Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Dar es Salaam (SHIVYAWATA),Charles Matemba anatarajiwa kufunga  ndoa  na  Fatuma  Ally Makame Juni 27,2026  katika Halmashauri ya Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam. Wanandoa hawa watarajiwa ni watu wenye ulemavu wameamua kuwa pamoja katika maisha yao ya ndoa jambo ambalo ni jema . "Tumeamua kufunga ndoa sisi wenye ulemavu kwani watu wenye ulemavu wana moyo wakupenda na hisia kama watu wengine"amesema Matemba. Bwana harusi Mtarajiwa Charles Matemba akizungumza na waandishi wa habari Mei 17,2026 katika kikao cha  kamati ya maandalizi ya harusi yao   Bwana harusi mtarajiwa Charles Matemba amesema ameguswa kumuoa Fatuma mlemavu mwenzake kwani wenye  ulemavu wamekuwa katika mazingira ya kunyanyapaliwa kutokana na ulemavu walionao kwamba hawawezi kuolewa ama kuoa Aidha, Matemba ametumia nafasi ...

MANISPAA TABORA YATOA MOTISHA KWA WALIMU

Image
  Na Allan Kitwe, DmNewsonline              TABORA  HALMASHAURI ya manispaa Tabora imetoa motisha kwa walimu na shule za sekondari zilizofanya vizuri zaidi katika masomo mbalimbali kwenye mitihani ya taifa ya kidato cha 4, 6na ule wa kujipima wa kidato cha 2 kwa mwaka 2025. Akitoa taarifa kwenye kikao cha baraza la madiwani, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Dkt John Pima, ameeleza kuwa wametoa motisha hiyo ili kuwatia moyo walimu na shule zao ili waendelee kufanya vizuri zaidi. Amefafanua kuwa kwa mwaka wa masomo 2025 halmashauri ya manispaa hiyo ilishika nafasi ya kwanza Kimkoa kati ya halmashauri 8 katika mitihani ya taifa ya kidato cha 6, 4 na upimaji wa kidato cha 2. Pima ameongeza kuwa kwa ujumla shule zote katika manispaa hiyo zilifanya vizuri katika mitihani hiyo ikilinganishwa na mwaka uliopita sababu kuu ikitajwa kuwa ni juhudi na weledi wa walimu katika kufundisha watoto hao. Amedokeza kuwa katika mitihani ya kidato cha 4 wal...

WAZIRI WA FEDHA AIPA KONGOLE BENKI YA CRDB KUHAMASISHA UWEKEZAJI NCHINI

Image
Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar akizungumza na Wanahisa.  Na Yusuph Mussa, DmNewsonline                ARUSHA  SETIKALI imeipongeza Benki ya CRDB kwa mkakati wake wa kuhamasisha uwekezaji nchini, hususan kwa vijana, kupitia elimu ya fedha, uwekezaji katika hisa na uwezeshaji wa kiuchumi unaolenga kujenga kizazi kipya cha wawekezaji wa Kitanzania. Pongezi hizo zimetolewa leo Mei 15, 2026 na Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omar kwenye Semina ya Wanahisa wa Benki ya CRDB ikiwa ni utangulizi kwa Mkutano Mkuu wa 31 wa Wanahisa wa Benki hiyo utakaofanyika kesho Mei 16, 2026, pia katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC) chini ya kaulimbiu ya Vijana na Uwekezaji kwenye Hisa. "Benki ya CRDB imeendelea kuwa mfano wa taasisi inayochochea ushiriki wa wananchi katika umiliki wa uchumi kupitia uwekezaji kwenye masoko ya mitaji. Kaulimbiu ya mwaka huu imebeba ujumbe mkubwa wa kimkakati kwa Taifa letu. Vijana hawapaswi ku...

TAKUKURU YAPAISHA MAPATO PWANI

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline Na Gustaphu Haule, Pwani  TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Pwani imeshiriki katika kupaisha makusanyo ya mapato ya Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha na kufikia kiasi cha zaidi ya Sh.bilioni 1.6. Fedha hizo ni makusanyo ya ushuru katika kipindi cha miezi mitatu ikiwa ni kuanzia Januari hadi Machi ambapo Takukuru ilifanya uzuiaji katika ukusanyaji wa mapato upande wa ushuru wa huduma. Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Ezekia Sinkala,ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika Mei 15/2026 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utendaji kazi katika kipindi cha Januari hadi Machi 2026. Sinkala ,amesema kuwa fedha hizo zilikuwa zinapotea kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kufuta stakabadhi za  mauzo na kutokuwa tayari kulipa ushuru wa huduma . Aidha,Sinkala amesema kuwa katika ufuatiliaji huo Takukuru Mkoa wa Pwani ilibaini mambo mbalimbali ikiwemo wafanyabiashara kufuta staka...