Posts

WADAU ZAIDI YA 200 SEKTA YA AFYA KUSHIRIKI MKUTANO WA KIMATAIFA WA SNOSSA 2026 DAR

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline      DAR ES SALAAM  TAASISI ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Kimataifa wa Society for Neuro-Oncology Sub-Saharan Africa (SNOSSA) 2026, utakaofanyika ijini Dar es Salaam. Mkutano huo  ukitarajiwa kukutanisha wataalamu, watafiti na wadau wa sekta ya afya zaidi ya 200 kutoka ndani na nje ya Afrika kujadili maendeleo ya tiba ya magonjwa ya mfumo wa fahamu, hususan saratani za ubongo na mfumo wa fahamu. Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Mhe. Balozi Dkt. Mpoki Ulisubisya, amesema mkutano huo utatoa fursa ya kujadili mbinu za kisasa za kugundua mapema magonjwa ya mfumo wa fahamu, matumizi ya teknolojia za kisasa katika uchunguzi wa radiolojia, pamoja na matibabu sahihi na ya wakati. Aidha, washiriki watajadili namna ya kuboresha upatikanaji wa huduma za afya, kuimarisha ushirikiano wa kitaaluma na kuendeleza tafiti zinazolenga kuboresha huduma kwa wagonjwa. Dkt. Mpoki ameongeza kuwa kupitia mkutano ...

WAZIRI ULEGA :HAKUNA SABABU YA KURUHUSU WATU WACHACHE KUVURUGA AMAN NA UTULIVU WA NCHI YETU.

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                    ARUSHA  WAZIRI wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amewataka Watanzania kuendelea kuilinda amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa hakuna sababu ya kuruhusu watu wachache kuitumia hali hiyo kwa maslahi yao binafsi au ya wengine. Akizungumza jijini Arusha wakati wa ukaguzi wa miradi ya miundombinu, Ulega amesema kuna baadhi ya watu wanaotamani kuona Tanzania ikiingia katika vurugu ili wapate hoja za kuwasilisha kwa wanaowaunga mkono, lakini akasisitiza kuwa hilo halitafanikiwa. "Kuna watu wanatamani tuwe na vurugu. Tusipokuwa na vurugu wanakosa cha kusema kwa mabwana zao. Amani tuliyonayo tusiikubali itumike vibaya kwa maslahi ya watu wachache," amesema Ulega. Ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha mazingira ya amani, utulivu na maendeleo yanadumishwa huku ikiendelea kutekeleza miradi ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi. Ulega pia ametoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikian...

TAZAMA UTABIRI WA HALI YA HEWA JUNI 29 2026

Image

TESHA AICHANGIA FFC MILIONI 10, ATAKA WANAKWAYA WAJIKOMBOE KIUCHUMI KUPITIA MIRADI

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline            DAR ES SALAAM  MWENYEKITI  wa Bodi ya Ofisi ya Hakimiliki Tanzania (COSOTA), Victor Tesha, amewataka wanakwaya wa Flying Family Choir (FFC) kuanzisha miradi ya maendeleo itakayokuwa chanzo cha kuongeza kipato na kuwasaidia kujikomboa kutoka katika umaskini. Tesha amesema hayo Juni 28,2026 katika tamasha la kwaya hiyo lijulikanalo FFC Corporate Encore 2026, lililofanyika katika Ukumbi wa Cardinal Rugambwa, Oysterbay, jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na watu mbalimbali, akiwemo Askofu wa Jimbo Katoliki la Morogoro, Lazarus Msimbe. FFC Kwaya inaundwa na wanakwaya kutoka madhehebu matatu ya Kikristo ambayo ni Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Kanisa la Anglikana na Kanisa Katoliki, wakishirikiana kupitia huduma ya uimbaji wa injili. Akizungumza katika tamasha hilo, Tesha ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Wadogo wa Madini Tanzania (FEMATA), amesema wana...

TUME YA PDPC YAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA MABADILIKO YA AKILI UNDE

Image
  Timothy Marko DmNewsOnline              DAR ES SALAAM.  TUME ya Udhibiti wa Taarifa Binafsi Nchini imesema moja ya Changamoto inayoikabili Taasisi hiyo niukuaji wa Teknolojia ya Akili unde(AI) bila kuzuia Maendeleo ya kiuchumi wa Kidijitali.  Akizungumza Leo  June 29,2026jijini Dar es Salaam kwenye Kongamano la kwanza la Ulinzi wa taarifa Binafsi Nchini Tanzania(1st Tanzania Annual Data Privacy Conference )Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nchini Dk.Switbetrt Mkama amesema kuwa Taarifa Binafsi ni Utambulisho wa mtu hivyo haina budi kulindwa,Taasisi zina umuhimu wa kuzilinda Taarifa hizo katika kuelekea Uchumi wa kigitali.  "Mamlaka ya Ulinzi wa taarifa Binafsi zinawajibu kushirikiana na Taasisi za kikanda Barani Afrika katika Ulinzi wa taarifa Binafsi katika kuelekea Uchumi wa kigitali "Amesema Naibu Waziri Dkt Mkama. Dkt.Mkama Ameongeza kuwa katika kuelekea Uchumi wa kigitali suala la Faragha Nimuhimu iliku...

VIJANA 10 WAFUZU FAINALI SHINDANO LA VIJANA UCHUMI CHALLENGE 2026

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                     PWANI  VIJANA  wapatao kumi (10) kutoka baadhi ya mikoa mbali mbali   wamefanikiwa kutinga katika kinyang'anyiro cha  shindano la Vijana uchumi Challenge kwa mwaka wa 2026 ambalo kilele chake kinatarajiwa kufanyika Julai 6 mwaka huu katika ukumbi   Mikutano wa Julius Nyerere International Convention Centre (JNICC), jijini Dar es Salaam. Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Jenifa Omolo  ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa  halfa ya kufunga kambi rasmi ya vijana wapatao 100 ambao walikuwa wameweka kambi ya siku nne katika shule yaa uongozi wa Mwalimu Julias Nyerere iliyopo Kibaha Mkoa wa Pwani. Katibu Oomolo amesema kwamba kambi hiyo ilikuwa na vijana wapatao 100 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania bara na visiwani ambapo wameweza kufanyiwa usahili na  kufanyiwa mchujo kutoka kwa majaji mahiri wap...

RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA SABA WA MADINI NOVEMBA 19,2026 DAR

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline       DAR ES SALAAM  RAIS   Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi. Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chachu ya Ukuaji wa Viwanda na Uchumi," inaakisi dira ya serikali ya kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha uchakataji wa madini barani Afrika. Kwa mujibu wa Mhe. Mavunde, amesema Tanzania tayari ina viwanda vinane vya kusafisha dhahabu, huku Mkoa wa Dodoma ukiwa na viwanda tisa vinavyojengwa na vinavyoendelea na uzalishaji pamoja na kiwanda kikubw...