MCHANGE AHOJI: DK. NCHIMBI ANAJUA MADHARA YA KAULI ZAKE AU ANATUTEGA?
Na Mwandishi Wetu,DmNewsTz Mchambuzi wa masuala ya siasa, jamii na maendeleo, Habibu Mchange, ametoa tafakuri kuhusu utata wa kauli za mara kwa mara za Makamu wa Rais, Dk. Emmanuel Nchimbi, akisema kutokana na nafasi yake ya kikatiba kama Msaidizi Mkuu wa Rais kwa mujibu wa Ibara ya 47(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kauli zake zinapaswa kupimwa kwa uzito mkubwa kwa kuwa zina athari kwa Serikali, mshikamano wa uongozi na imani ya wananchi kwa taasisi za dola. Katika tafakuri hiyo yenye kichwa "DK. NCHIMBI ANAJUA MADHARA YA KAULI ZAKE AU ANATUTEGA?", Mchange amechambua kauli ya Dk. Nchimbi kwamba "Katiba iliyopo ina mapungufu na inampa Rais madaraka yasiyo na maana," pamoja na wito wake wa "komaeni, pambaneni mpate Katiba mpya," akisema kauli hizo zimezua mjadala mkubwa wa kikatiba na kisiasa, hasa wakati Serikali tayari imeeleza kuwa mchakato wa Katiba mpya utaanza baada ya kukamilika kwa maridhiano ya kitaifa. Amehoji kuwa iwapo Serikali...