Posts

Showing posts from September, 2026

VIJANA WA DENMARK WASHIRIKI MSALAGAMBO KOROGWE

Image
Meneja wa TFCG Wilaya ya Korogwe Bettie Luwuge (katikati) akizungumza na wakulima wa Vugiri. Na Yusuph Mussa, DmNewsonline                KOROGWE  VIJANA sita kutoka nchini Denmark wameshiriki kilimo cha msalagambo (pamoja) na wakulima wa mahindi., maharage na mbogamboga wa Kijiji cha Vugiri, Kata ya Vugiri, Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga. Pamoja na mambo mengine, vijana hao kutoka vyuo na maeneo mbalimbali nchini Denmark kupitia kikundi chao cha Global Story Tellers, wanatembelea miradi yote Tanzania inayofadhiliwa na Shirika la kidini la Danmission, na kwa Wilaya ya Korogwe, taasisi hiyo kupitia Shirika la Uhifadhi wa Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), inafadhili Mradi wa Tunza Uumbaji (Care for Creation). Mradi huo kwa Wilaya ya Korogwe, unajishughulisha na uhifadhi wa misitu ya asili na mazingira.kwa kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa kuwapa elimu ya kilimo cha mbogamboga, maharage, mahindi, ufugaji wa nyuki, kuwapa vifaa kwa ajili ya ulinz...

MIL 360 ZA BAKAA KUTEKELEZA MIRADI VIPORO MANISPAA TABORA

Image
  Na Allan Kitwe,DmNewsonline                      TABORA MADIWANI wa halmashauri ya manispaa ya Tabora wameazimia fedha zote zilizotengwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ulioishia Juni 2026 na hazikutumika (bakaa) zisirudishwe TAMISEMI bali zitumike kukamilisha miradi viporo. Hayo yamebainishwa na Katibu wa Madiwani wa CCM Bahati Adam Ntiruhungwa (diwani wa Kata ya Ng’ambo) alipokuwa akitoa maazimio yao kwenye kikao cha robo ya nne ya baraza kilichoketi leo Mjini hapa. Ameeleza kuwa madiwani ndio wawakilishi wa wananchi katika Kata zao, hivyo wana dhamana ya kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa katika maeneo yao inakamilika kwa wakati kwa manufaa ya wananchi. ‘Madiwani wa CCM tumeazimia miradi viporo yote ikamilishwe, na fedha za bakaa, zaidi ya shilingi milioni 364 ziombewe kibali ili zitumike kumalizia miradi iliyoanza kutekelezwa katika msimu uliopita’, amebainisha. Ntiruhungwa ameitaka Ofisi ya Mkurugenzi kuhakikisha wak...

NJEDEMBI KUHUDHURIA KONGAMANO LA UCHUMI WA BULUU

Image
 Timothy Marko,DmNewsOnline         DAR ES SALAAM  MAKAMU Rais Deogratius Ndejembi, anatarajiwa kuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Tano la Kimataifa la Uchumi wa Buluu, litakalofanyika Septemba 7 hadi 9, mwaka huu katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.  Hayo yamesemwa mbele ya   waandishi wa habari jijini Dar es Salaam  leo na Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam, Tumaini Gurumo ambapo amesema kongamano hilo litawakutanisha washiriki kutoka Tanzania, Afrika na mataifa mbalimbali duniani. Amesema miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa ni namna ya kutumia rasilimali za bahari, mito, maziwa na vyanzo vingine vya maji kwa ufanisi, kuongeza ajira, kukuza ubunifu na kuchochea maendeleo endelevu.“Tunataka kupitia kongamano hili wadau mbalimbali waweze kufahamu kwa kina fursa zilizopo katika Uchumi wa Buluu na namna bora ya kuzitumia kwa maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla,” amesema Gurumo. Amesema...

TARURA YATENGA BIL. 1 KUKABILIANA NA EL NINO TABORA

Image
  Na Allan Kitwe,DmNewsonline                        TABORA  WAKALA wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoani Tabora wametenga zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo mbalimbali ili kukabiliana na wingi wa mvua za el nino. Hayo yamebainishwa jana na Afisa wa Wakala huo, Mhandisi Nehemia Chacha kwa niaba ya Meneja wa TARURA Mkoa wa Tabora alipokuwa akitoa taarifa ya hali ya barabara kwenye kikao cha madiwani wa halmashauri ya manispaa. Ameeleza kuwa ili kuhakikisha miundombinu ya barabara katika manispaa hiyo inapitika wakati wote wamekamilisha ujenzi wa madaraja makubwa 2 ya kimkakati katika kata za Ndevelwa, Misha na Kabila. Mhandisi amefafanua kuwa daraja la Ndevelwa ambalo lilikuwa kero kubwa sana kwa wananchi limegharimu zaidi ya shilingi milioni 460 na limekamilika kwa asilimia 100 na sasawananchi wameanza kulitumia, kero imeisha Daraja la pili ni lile linalou...

CCM YAPONGEZA MAFANIKIO MANISPAA TABORA

Image
.  Na Allan Kitwe,DmNewsonline                TABORA  HALMASHAURI ya Manispaa Tabora imepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana hadi sasa ambayo yamekuwa kichocheo kikubwa cha kuboreshwa huduma za kijamii katika kata zote 29. Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tabora Mjini Komredi Mohamed Katete alipokuwa akitoa salamu za chama kwenye kikao cha baraza la madiwani kilichoketi leo katika ukumbi mpya wa manispaa hiyo. Katete ameeleza bayana kuwa manispaa hiyo imepiga hatua kubwa kimaendeleo kutokana na kazi nzuri iliyofanyika kwenye miradi ya maendeleo, hali ambayo imepelekea kutatuliwa changamoto za wananchi. ‘Nakupongeza sana Mstahiki Meya, ndugu yangu Gullam-Hussein Dewj, Mkurugenzi wa Manispaa Dkt John Pima, Mkuu wa Wilaya Upendo Wella, Waheshimiwa Madiwani na Wataalamu wote, kwa kazi yenu njema’, amesema. Amebainisha wazi kuwa sasa hivi wananchi wanapata huduma bora za kijamii katika kata zote tofauti na hali ...

SHERIA 9 KUWABANA WASANII NA WATOA MAUDHUI MTANDAONI.

Image
  Timothy Marko DmNewsOnline               DAR ES SALAAM. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi amewataka Wasanii mbalimbali wa Bongo flavour na Watengeza maudhui Mtandaoni Kujiepusha na mikingano ya Sheria (9)za mitandaoni ikiwemo kutoa Lugha Chafu mitandaoni. Akizungumza Leo  September 2, 2026 Waziri Katambi amesema kuwa sheria  zingine  ambazo zimetajwa nipamoja na sheria ya makosa ya kutukana nakutoa Lugha Chafu za matusi na kudhalilisha  ya 89(1)a Mitandaoni adhabu yake nikifungo cha mwaka mmoja jela. "Sheria zingine nipamoja sheria ya makosa ya kupigana pamoja na mashambulio katika Eneo la Umma(affray) S.87ambapo kifungo chamiezi 6 au faini hadi Shilingi 1000,00, Vitisho vya  kumdhuru au kumpiga mtu S.89(2)"Amesema Waziri wa Mambo ya Ndani Patrobas Katambi.  Waziri wa Mambo ya Ndani Katambi Ameongeza kuwa kuonesha kitendo kisicho cha maadili uchafu hadharani S.176(f) Faini Shilingi 1000,00 ...

SHERIA 9 KUWABANA WASANII NA WATOA MAUDHUI MTANDAONI.

Image
  Timothy Marko DmNewsOnline               DAR ES SALAAM. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi amewataka Wasanii mbalimbali wa Bongo flavour na Watengeza maudhui Mtandaoni Kujiepusha na mikingano ya Sheria (9)za mitandaoni ikiwemo kutoa Lugha Chafu mitandaoni. Akizungumza Leo  September 2, 2026 Waziri Katambi amesema kuwa sheria  zingine  ambazo zimetajwa nipamoja na sheria ya makosa ya kutukana nakutoa Lugha Chafu za matusi na kudhalilisha  ya 89(1)a Mitandaoni adhabu yake nikifungo cha mwaka mmoja jela. "Sheria zingine nipamoja sheria ya makosa ya kupigana pamoja na mashambulio katika Eneo la Umma(affray) S.87ambapo kifungo chamiezi 6 au faini hadi Shilingi 1000,00, Vitisho vya  kumdhuru au kumpiga mtu S.89(2)"Amesema Waziri wa Mambo ya Ndani Patrobas Katambi.  Waziri wa Mambo ya Ndani Katambi Ameongeza kuwa kuonesha kitendo kisicho cha maadili uchafu hadharani S.176(f) Faini Shilingi 1000,00 ...