SHERIA 9 KUWABANA WASANII NA WATOA MAUDHUI MTANDAONI.
Timothy Marko DmNewsOnline
DAR ES SALAAM.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Patrobas Katambi amewataka Wasanii mbalimbali wa Bongo flavour na Watengeza maudhui Mtandaoni Kujiepusha na mikingano ya Sheria (9)za mitandaoni ikiwemo kutoa Lugha Chafu mitandaoni.
Akizungumza Leo September 2, 2026 Waziri Katambi amesema kuwa sheria zingine ambazo zimetajwa nipamoja na sheria ya makosa ya kutukana nakutoa Lugha Chafu za matusi na kudhalilisha ya 89(1)a Mitandaoni adhabu yake nikifungo cha mwaka mmoja jela.
"Sheria zingine nipamoja sheria ya makosa ya kupigana pamoja na mashambulio katika Eneo la Umma(affray) S.87ambapo kifungo chamiezi 6 au faini hadi Shilingi 1000,00, Vitisho vya kumdhuru au kumpiga mtu S.89(2)"Amesema Waziri wa Mambo ya Ndani Patrobas Katambi.
Waziri wa Mambo ya Ndani Katambi Ameongeza kuwa kuonesha kitendo kisicho cha maadili uchafu hadharani S.176(f) Faini Shilingi 1000,00 kifungo hadi miezi mitatu au vyote.
Amesisitiza kuwa Sheria zingine nipamoja na kujitangaza au kushawishi kwa madhumuni ya Uasherati S.176(g) Faini hadi Shilingi 1000,00 au kifungo cha miezi mitatu.
"Uasherati Prostution hadharanj S.176 (a)faini Shilingi 1000,00 kifungo miezi mitatu au vyote "Amebainisha Katambi.
Sheria Nyinginezo nipamoja Maonesho Machafu yanayopotosha Maadili S.175 kifungo cha miaka miwili au faini 200,000, Ushoga kati ya wanaume S.157 kifungo cha miaka mitano jela, Kuvunjia mwanamke heshima kwa maneno au ishara jela miaka 5 faini Shilingi 200,000 au vyote.

Comments
Post a Comment