FIBERHOME YAUNGA MKONO JITIHADA ZA SERIKALI KUBORESHA MAWASILIANO.
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline WAZIRI wa Mawasilano na Teknolojia ya Habari Angellah Kairuki alizindua awamu ya pili ya Mradi wa "Fiber mlangoni kwako"unaotekelezwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania(TTCL)ikiwa lengo ni kuongezea upatikanaji wa intaneti yenye kasi,bora na uhakika. Aidha Kairuki amesema mradi huo ni sehemu ya jitihada za Serikali za kuimarisha uchumi wa kidigitali kwa kuwa intaneti ya kasi inawezesha wananchi kupata fursa za elimu,ajira, biashara,ubunifu na huduma mbalimbali za kijamii na kiuchumi. Hivyo wadau wa Sekta ya Teknolojia ambao ni Kampuni ya mawasiliano ya FiberHome kutoka Nchini China imeunga mkono juhudi za Serikali kwa kueendesha kongamano (workshop)nchini Tanzania lililofanyika jijini Dar es salaam ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kuitangaza teknolojia yao Duniani na barani Afrika (World Tour). Ziara hiyo imelenga kuleta mapinduzi makubwa ya Teknolojia ya mawasiliano na akili...