DKT.NCHIMBI:NITAENDELEA KUWA RAIA MWEMA.

 Na Mwandishi wetu, DmNewsOnline 

MAKAMU  wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt.EmmanuelJohn Nchimbi amejiuzulu Leo. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya Makamu wa Rais mjini Dodoma  ili eleza kuwa Dkt. Nchimbi amejiuzulu kwa mujibu wa ibara 50(2)C pamoja na 149(2) ya katiba ya Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania. 

Katika Barua yake aliyomwandikia Rais, Agosti 28,2026 Dkt.Nchimbi amesema kuwa mnamo Agosti 27 Mwaka jana alimwaidi kushirikiana  na Rais Wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa uwezo wake na kwa Uaminifu mkubwa nakusisitiza kuwa  ataachia ngazi siku yoyote.

"Nitaachia nafasi hii nimejiridhisha kuwa Mheshimiwa Rais pasipo shaka anahitaji mabadiliko kwa hiyo nimetimiza Ahadi yangu" Amesema Dkt.Emanuel Nchimbi. 

Dkt..Nchimbi katika Barua yake aliyomwandikia Rais alieleza kuwa amekishukuru Chama chake kwa imani waliyonayo kwake nakusisitiza kuwa ataendelea kuwa Raia mwema Watanzania.

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

MWAKIPOSA ASHINDA NAFASI YA UWENYEKITI WA WENYEVITI WA SERIKALI YA MTAA MKOA WA DAR ES SALAAM

KILINDI BARABARA BADO NI CHANGAMOTO