JESHI LA POLISI KUENDELEA NA UCHUNGUZI MAUAJI MBEZI.
Timothy Marko, DmNewsonline
DAR ES SALAAM.
JESHI la polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema linaendelea na Uchunguzi wa kina juu ya Ramadhan Jafarry Muno (47) Baada kudaiwa kupotea huko Mbezi Wilaya ya Ubungo akiwa kwenye Nyumba yake.
Akizungumza Leo juni 23,2026 jijini Dar es Salaam Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam ( CP) Jumanne Murilo amesema kuwa tukio hilo lili tokea juni 16,mwaka huu huko Mbezi Kimara Wilayani Ubungo, Baada ya Jeshi hilo kutarifiwa kuwa mtu huyo amepotea katika Mazingira ya kutatanisha.
"Katika Uchunguzi wa awali Jeshi la polisi tulibaini kuwa aliye fanya tukio hilo ni Mtoto wa Marehemu huyo Juma Ramadhani(21) Ambapo alieleza kuwa Amemuuwa Baba yake" Amesema Kamanda Murillo.
Murilo Ameongeza kuwa Jeshi hilo linaendelea na Uchunguzi wa mtoto huyo kubaini chanzo halisi cha kumua Baba yake.
Amesisitiza Baada ya Uchunguzi wa tukio hilo hatua kali zitachukuliwa juu ya Mtuhumiwa huyo.
Katika Hatua nyingine Kamishna Murillo Amesema waendelea kufanya Uchunguzi wa taarifa zisizo rasmi kuwa kuna Baadhi ya watu wanataka kuandamana Julai 7 Mwaka huu na kusisitiza kuwa jeshi hilo linachunguza juu ya tukio hilo linalodaiwa kutajwa na Baadhi ya Wanaharakati.
Amebainisha kuwa linafanyia kazi juu ya mipango hiyo kwa weledi kabla ya kuwakamata Watuhumiwa wanaotaka kufanya maandamano hayo.
Amesema Suala la Upelelezi linahitaji Utulivu ,ushaidi unaokubalika Mahakamani.
"Hata suala la kuimarisha Ulinzi na Usalama kwenye Baadhi ya mikutano ya Kisiasa tunafanya kwa kuzingatia Weledi "Amesisitiza Kamanda murilo
Kamanda Murilo amewambia Waandishi wa Habari kuwa moja ya majukumu ya jeshi hilo mara baada ya kupata fununu za matukio ya Uvunjifu wa amani ni kufanya uchunguzi,kupeleleza na kukusanya Ushaidi ili kupeleka Mahakamani juu ya mashauri.
"Msemaji wetu wa Jeshi la Polisi Afande David Misime ameshasema juu ya msimamo wetu wa Julai 7 ,Mwaka huu sisi tumejipanga kuimarisha Usalama Amebainisha Kamanda Murilo.

Comments
Post a Comment