Posts

MWAKIPOSA ASHINDA NAFASI YA UWENYEKITI WA WENYEVITI WA SERIKALI YA MTAA MKOA WA DAR ES SALAAM

Image
  Na Angelina Mganga -DmNewsOnline     BDAR ES SALAAM  UCHAGUZI wa nafasi ya  Uwenyekiti na Katibu Mkuu wa Umoja wa Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Dar es Salaam umefanyika Leo Juni 20,2026,na umemalizika kwa amani na utulivu. Uchaguzi huo ulikuwa na wagombea watatu ambao  wamewania nafasi hiyo ya Uwenyeviti wa Wenyeviti wa Serikali ya Mtaa Mkoa wa Dar es Salaam   Wagombe wa nafasi ya Uwenyeviti ni Consolatha M.Rwiza Juma A.Mwingano na Razalous A.Mwakiposa  Katika uchaguzi huo Razalous A.Mwakiposa ameibuka mshindi wa nafasi hiyo ya  Uwenyekiti huku Peppino Sudi Peppino akishinda nafasi ya Katibu. Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya uchaguzi huo,Msimamizi wa Uchaguzi Kambi Sinde amesema kuwa kura zilizopigwa ni 37 na wagombea  walikuwa  Consolatha M.Rwiza (11),Juma A.Mwingano  (2 )na Razalous A.Mwakiposa ( 24 ) hakuna kura iliyoharibika.  Razalous A.Mwakiposa ameshinda Kwa kura 24 kati ya kura 37zilizopig...

JESHI LA POLISI LATOA ONYO KALI KWA WANAOHAMASISHA MAANDAMANO NA VURUGU.

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNewsonline               DODOMA JESHI  la Polisi Tanzania limetoa onyo kali kwa watu wanaotumia mitandao ya kijamii kuhamasisha vitendo vya uvunjifu wa amani, ikiwemo maandamano yasiyo halali na vurugu. Kupitia taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu Dodoma, jeshi hilo limesema linafuatilia kwa karibu shughuli zote za uhamasishaji huo kwa saa 24. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, awali watu hao walikuwa wakihamasishana kufanya maandamano nchini tarehe 7 Julai. Hata hivyo, ufuatiliaji wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa sasa wameondoka kwenye ajenda ya maandamano na kuanza kuhamasisha vitendo vya moja kwa moja vya uhalifu vinavyolenga kuhatarisha usalama wa raia na mali zao. Miongoni mwa vitendo vilivyotajwa kwenye taarifa hiyo ni kuhamasisha kufunga barabara, kuchoma moto shule ili kusababisha taharuki kwa wazazi, kushambulia wananchi, kukata vichwa, kuua watu, na kuharibu mali za umma na binafsi. Aidha,...

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUTOA ELIMU JUU YA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA.

Image
       Ti mothy Marko DmNewsOnline.          DAR ES SALAAM. WAANDISHI Habari wametakiwa kuwaelimisha Watumishi wa umma Nchini juu ya Maadili yao ili kuweza kufikia Dira ya Maendeleo 2050. Akizungumza Leo Mei 19 ,2026  katika Kongamano la Waandishi wa Habari na Wahariri wa  Vyombo vya Habari Nchini (TEF)Katibu msimamizi  wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma  Kassim Mkwawa amesema kuwa katika kukuza maadili ya Viongozi wa Umma, vyombo vya Habari vinamchango wakipekee wa kuwaelimisha Watumishi wa umma juu ya Maadili ya Utumishi wa Umma.  "Sektarieti ya Maadili ya Utumishi wa Umma imeundwa chini ya sheria namba (14) ya mwaka 1995 ya Maadili ya Utumishi wa Umma" amesema mkwawa  Ameongeza kuwa Taasisi hiyo imelenga kukuza Watumishi wa umma walio na weledi na Uzalendo kwa Nchi yao. Amesisitiza kuwa hivi karibuni kumekuwa na minongo'no ya kupungua kwa Uadilifu kwa Baadhi ya Watumishi wa umma huku c hanzo kikubwa kikita...

TAASISI ZATAKIWA KUIMARISHA KITEKNOJIA KUFIKIA DIRA 2050.

Image
  Timothy Marko DmNews Online             DAR ES SALAAM.KATIKA  KUHAKIKISHA Dira ya Maendeleo ya 2050 inatekelezwa ,Taasisi za Umma Nchini zimetakiwa kuwapa nafasi watumishi wa Umma  mafunzo na Ujuzi kwenye vyuo mbalimbali vya Utumishi wa Umma ili kuleta Ufanisi katika kazi zao. Akimwakilisha Makamu wa Rais wa Jamuhuri  Muunganowa Tanzania Dkt.Emanuel Nchimbi katika Kongamano la Watumishi wa umma Nchini Leo,Juni 18,2026 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwan Kikwete a mesema kuwa lengo la Kongamano hilo ni Utekelezaji wa Maazimio ya Dira ya Maendeleo ya 2050 yanayolenga kukuza Maarifa Uwajibikaji na  Ufanisi baina ya Watumishi wa umma Nchini.  "Kongamano hili pia linalenga kutathimini Utumishi wa Umma katika kutekeleza Dira ya Maendeleo ya 2050"Amesema Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwan Kikwete.  Waziri wa Utumishi wa Umma Kikw...

Msamaha wa VAT kwa Mafuta ya Kula Utachochea Uwekezaji wa Ndani

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsOnline  Msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa mafuta ya kula yanayozalishwa kwa kutumia mbegu zinazozalishwa ndani ya nchi unatarajiwa kuongeza uwekezaji, ushindani wa viwanda vya ndani na kuchochea uzalishaji wa mazao ya mafuta nchini. Hayo yamesemwa na mchambuzi wa uchumi, Marandu Marwa, akizungumzia hatua mpya za Serikali zilizotangazwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27. Amesema hatua hiyo itawapa motisha wawekezaji kutumia malighafi zinazozalishwa ndani ya nchi kwa kuwa zitawasaidia kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza faida. “Kila mwekezaji ataona kutumia mbegu zinazozalishwa ndani ya nchi kama njia rahisi ya kuongeza faida na kupunguza gharama za kodi. Hii itaongeza ushindani na kuwanufaisha wazalishaji wa ndani,” amesema. Marwa amesema kwa muda mrefu tofauti ndogo ya ushuru kati ya bidhaa zinazoagizwa kutoka nje na zinazozalishwa nchini imekuwa ikidhoofisha ushindani wa viwanda vya ndani na kupunguza hamasa ya uwekezaji mkubwa ...

CHALAMILA AWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI ZA MITAA KUDHIBITI MAJENZI KWENYE MAENEO YA MABALOZI.

Image
    Timothy Marko DmNewsOnline                  DAR ES SALAAM.  MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila Amewataka   Viongozi wa Serikali ya mtaa waliopo katika Maeneo ya Mabalozi kudhibiti kasi ya Majenzi ya Majengo,nakutaka kusitisha Vibali vya Majenzi katika Maeneo hayo. Akizungumza leo juni 15,2026 jijini Dar es Salaam katika Kongamano lililowakutanisha Watendaji wa Serikali za Mitaa na kata Albert Chalamila Amewataka Watendaji hao kusitisha vibali  kwa wanaomiliki Bar zilizozopo kwenye makazi ya watu na kuhakikisha Bar zote jijini Dar es Salaam kuwa na Vizibiti Sauti kwenye Makazi ya watu. '"iundwe timu Maalumu kasi ya Udhibiti Majenzi kwenye maene ya Diplomatic, Ninawaomba Ndugu wenyeviti wa Serikali za mitaa kutambua nafasi zenu"Amesema Chalamila.  Chalamila Ameongeza kuwa nivyema Wenyeviti wa Serikali za mitaa kufunga Bar zote ambazo hazina vidhiti sauti. Amesisitiza kuwa katika Takwimu zilizop...

WATUHUMIWA 215 WAKAMATWA KWA MAKOSA MBALIMBALI IRINGA

Image
   Na Eliasa Ally DmNewsonline                   IRINGA  JESHI  la Polisi Mkoa wa Iringa limefanikiwa kuwakamata jumla ya watuhumiwa 215 kwa makosa mbalimbali katika kipindi cha Mei 1 hadi Juni 9, 2026 na kuwafikisha Mahakamani.  Watuhumiwa hao walikamatwa kupitia misako, doria na operesheni maalumu zilizofanyika maeneo mbalimbali ya mkoa huo huku wakikutwa na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi zikiwemo magari, vifaa vya ujenzi, vifaa vya umeme, simu za mkononi, pikipiki pamoja na mali nyingine mbalimbali. Aidha, Juni 9, 2026 katika eneo la Igumbilo Manispaa ya Iringa, Polisi walimkamata mfanyabiashara mmoja kutoka Tunduma pamoja na wenzake watatu kutoka Dar es Salaam wakiwa na katoni 177 za vipodozi vilivyopigwa marufuku nchini, vilivyokuwa vikisafirishwa kwa basi kutoka Zambia kuelekea Dar es Salaam. Kwa upande wa usalama barabarani, Polisi walimkamata dereva aliyekuwa akiendesha kwa uzembe na kuhatarisha usalama wa wa...