VIJANA WA DENMARK WATEMBELEA MRADI WA NYUKI KOROGWE
Vijana sita wa Denmark na wenyeji wao, walipofika Shamba la Nyuki Kwamaraha. Na Yusuph Mussa, DmNewsonline KOROGWE VIJANA sita kutoka nchini Denmark wametembelea Mradi wa Nyuki wa Jimbo la Tambarare, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na kujionea maendeleo ya mradi huo wa wanawake na vijana. Pamoja na mambo mengine, vijana hao kutoka vyuo na maeneo mbalimbali nchini Danmark kupitia kikundi chao cha Global Story Tellers, wanatembelea miradi yote Tanzania inayofadhiliwa na Shirika la kidini la Danmission, na kwa Wilaya ya Korogwe, shirika hilo kupitia Shirika la Uhifadhi wa Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), imefadhili Mradi wa Nyuki kupitia FORLIVES. Akizungumza kwenye ziara hiyo iliyofanyika Septemba 5, 2026, Mwenyekiti wa Kamati ya Kiuchumi Jimbo la Tambarare, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Kanisa la KKKT, Betty Munuo alisema Danmission kupitia Mradi wa FORLIVES, baada ya kuwawe...