Posts

LUSHOTO WAMSHUKURU RAIS SAMIA MRADI WA SOKO NA STENDI

Image
WAZIRI wa TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe akizungumza na wananchi wa Lushoto. Na Yusuph Mussa, DmNewsonline                Lushoto WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Profesa Riziki Shemdoe, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kutoa sh. bilioni 6.4 kwa ajili ya ukarabati wa Soko Kuu na Stendi Kuu ya Mabasi Lushoto mjini. Ameyasema hayo Julai 22, 2026 kwenye hafla fupi ya utiaji sahihi wa mikataba ya miradi ya uboreshaji wa ujenzi wa Soko Kuu la mjini Lushoto na ujenzi wa Stendi Kuu ya Mabasi, na Msimamizi Mshauri wa Miradi ya ujenzi na uboreshaji wa soko pamoja na ujenzi wa stendi ya mabasi iliyofanyika pembezoni mwa soko hilo. "Tunamshukuru sana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia sisi wana Lushoto tuweze kupata sh. bilioni 6.4 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu mipya ya Soko la Lushoto pamoja na ujenzi wa stendi mpya ya Lushoto. Niushukuru sana uongozi wa M...

MEYA KIBAHA AHIMIZA UKAMILISHAJI WA UJENZI WA ZAHANATI YA VISIGA ILI IPANDISHWE HADHI KUWA KITUO CHA AFYA

Image
        Na Mwandishi wetu, DmNewsonline                                           KIBAHA  MSTAHIKI  Meya wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Mawazo, amemtaka Mganga Mkuu wa Manispaa Dkt. Catherine Saguti kuhakikisha ujenzi wa majengo mbalimbali katika Zahanati ya Visiga unakamilika kwa haraka ili zahanati hiyo ipandishwe hadhi na kuwa Kituo cha Afya, hatua itakayowasogezea wananchi huduma bora za afya karibu na makazi yao. Dkt. Mawazo ametoa wito huo jana alipokuwa katika ziara ya Kamati za Kudumu za Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Kibaha zilizotembelea miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo tofauti ya manispaa hiyo. Amesema ni muhimu kukamilisha kwa wakati mradi wa ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) pamoja na miundombinu mingine ya msingi ili kukidhi vigezo vya kuipandisha hadhi Zahanati ya Visiga kuwa Kituo cha Afya. "Uje...

KATELE ACHAGULIWA TENA MWENYEKITI WA TUGHE MKOA WA PWANI

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                     PWANI    HATIMAYE  Chama Cha wafanyakazi wa Serikali na afya  (TUGHE) Mkoa wa Pwani kimefanya uchaguzi wake mkuu na kuweza kumchangua kwa kishindo Mwenyekiti  aliyekuwa anatetea  kiti  chake  Catherine Katele  ameibuka na ushindi wa kura 33 dhidi ya mpinzani wake ambaye amejinyakulia kura  18 kati ya kura halali 51 ambazo zimepigwa. Katika uchaguzi huo ambao  ulifanyika  katika ukumbi wa Mkuu  wa Mkoa wa Pwani ulihudhuliwa na wajumbe mbali mbali kutoka Wilaya zote saba za Mkoa wa Pwani zikiwemo, Kibaha, Rufuji, Bagamoyo , Mkuranga, Mafia,Kisarawe, pamoja na Kibiti ulikuwa na amani na utulivu katika kipindi chote cha uendeshaji wa  zoezi  zima la upigaji wa kura.      Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi  Metta Nahonyo  amesema kwamba uchaguzi umekwenda vizuri bila ya kuwa n...

ASILIMIA 80 KUFIKIWA NA NISHATI SAFI IFIKAPO 2034

Image
  Timothy Marko Dm Newsonline         DAR ES SALAAM.  KATIKA kuhakikisha Malengo ya kuhakikisha  Asilimia 80 ya Watanzania wanakuza matumizi ya Nishati safi yakupikia ifikapo 2034 Serikali imezitaka Asasi za kirahia pamoja na Vyombo vya Habari kukuza  Uelewa wa Umuhimu wa Nishati hiyo.   Akizungumza na Waandishi wa Habari Julai 14,2026jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Wafanyabishara wa mitungi ya kuhifadhi Gesi ya LPG Nchini (Tanzania LPG Association) Amos Jackson amesema hadi sasa  watanzania milioni 14.8 ndio wanaotumia Nishati hiyo huku adhima  ya Serikali kufikia 2034 zaidi ya Asilimia 80 wawe watumiaji wa Nishati hiyo. "Hadi Sasa Nchi ya China ndio inayoongoza kwa matumizi ya Nishati safi yakupikia ikiwa na watu takriban Bilioni 1.5 wanaotumia Nishati Safi,ikifuatiwa na Nchi ya India "Amesema Mkurugenzi wa TZLPGA) Jackson.  Mkurugenzi Jackson Ameongeza kuwa  katika Bara la Afrika Nchi zinazoon...

18 WANASWA NA POLISI KWA MAKOSA YA UHALIFU

Image
  Na Allan Kitwe DmNewsonline            TABORA  JESHI la Polisi Mkoani Tabora limefanikiwa kunasa watuhumiwa 18 waliokuwa wakijihusisha na vitendo mbalimbali vya kihalifu ikiwemo mauaji na kuwafikisha mahakamani, miongoni mwao sita wamehukumiwa kunyongwa hadi kufa. Hayo yamebainishwa leo na Kamanda wa Polisi Mkoani hapa ACP Twaha Lulengelule alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Polisi wa Elangwa Shahidi kwenye hafla maalumu ya kujitambulisha kwa wanahabari.   Amefafanua kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa katika kipindi cha mwezi Juni na Julai 2026 kutokana na oparesheni, doria na misako mbalimbali iliyofanywa na Jeshi hilo katika Wilaya zote za Mkoa huo ili kukabiliana na vitendo vya uhalifu. Katika msako wa Juni 18, 2026 majira ya saa 8:00 mchana huko Wilayani Sikonge walikamatwa watuhumiwa 4 wakiwa na silaha 1 aina ya Rifle Model 70-458 isiyo na namba ikiwa na risasi 3, wakiwa katika Pori la Nkomango, tarafa ya Kiwe...

BALOZI DKT NCHIMBI : UJUZI WA RASIRIMALI WATU NI NGUZO MUHIMU KATIKA TAASISI ZA AFYA.

Image
  Timothy Marko | DmNewsOnline          DAR ES SALAAM TAASISI  za afya nchini zimetakiwa kuendelea kujenga uwezo wa rasilimali watu ili kuimarisha uwezo wa taasisi na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma za afya. Wito huo umetolewa leo, Julai 16, 2026, na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt  Emanuel Nchimbi, wakati wa maadhimisho ya miaka 20 ya Taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation. Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Nchimbi amesema afya ni nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa, kwani rasilimali watu yenye afya ndiyo msingi wa ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu. Amesema Hayati Rais Benjamin Mkapa alitambua umuhimu wa kuimarisha sekta ya afya kama njia ya kujenga rasilimali watu na kuleta mageuzi ya kiuchumi nchini. "Taasisi ya Benjamin Mkapa imefanikiwa kukuza na kuwekeza katika maendeleo ya rasilimali watu, jambo lililochangia kuimarisha uwezo wa taasisi mbalimbali za afya," amesema Dkt. Nchimbi. Amesisitiza kuwa il...

WANASWA KWA TUHUMA ZA KUPANGA KUTAPELI BENKI

Image
   Na Allan Kitwe,DmNewsonline                                   TABORA JESHI la Polisi Mkoani Tabora limekamata watuhumiwa watatu kwa tuhuma za kupanga njama ya kufanya utapeli katika benki za CRDB na NMB zilizoko Mjini Tabora. Kamanda wa Polisi Mkoani hapa ACP Twaha Lulengelule amethibitisha kukamatwa watuhumiwa hao Julai 10 mwaka huu majira ya saa 3:50 asubuhi walipokuwa wakijiandaa kuvamia benki hizo. Ameeleza kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa na askari waliokuwa doria katika maeneo ya benki wakati wakijiandaa kutekeleza azma yao ya kuingia na kupora wateja waliokuwa ndani ya benki hizo. Watuhumiwa waliokamatwa ni Shabani Nyambi (36), mkazi wa Kimara Korogwe, Dar es salaam, Saidatu Masoud (52) na Veronica Richard (40), wakazi wa Kimara Temboni, Wilaya ya Ubungo Jijini Dar es Salaam. Kamanda amefafanua kuwa baada ya kupekuliwa walikutwa na dola 7 za kimarekani, madaftari madogo 6, bahash...