RC TABORA KUPELEKA MASHABIKI WA SOKA UWANJA WA TAIFA
Na Allan Kitwe, DmNewsonline TOBORA MKUU wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha ameahidi kukodi mabasi ya kutosha ili kupeleka mamia ya mashabiki wa soka wa Mkoa huo uwanja wa Taifa ili kushangilia timu ya taifa (Taifa Stars) kwenye ufunguzi wa michuano ya CHAN. Ametoa ahadi hiyo jana alipokuwa akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo alieleza kuwa Mkoa huo ni miongoni mwa Mikoa yenye hamasa kubwa na mashabiki wengi wa soka hapa nchini. ‘Mashindano haya yapo nchini kwetu, ni lazima tupeleke mashabiki wengi zaidi kuliko Mikoa mingine ili kuiongezea hamasa timu yetu ya taifa, nitakodi mabasi ya kutosha ya kupeleka mashabiki bure uwanja wa taifa na kuwarudisha’, amesema. ‘Mheshimiwa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ameahidi kutoa zawadi nono kwa vijana wetu wakitwaa ubingwa, na sisi tutamuunga mkono kwa kuipa hamasa kubwa timu yetu ya taifa ili ifanye vizuri na kutwaa ubingwa ’, amesema...