CHAUMMA WAPOKEA MAPENDEKEZO KWA KAMATI JINSI YAKUPATA WANAWAKE WAWAKILISHI




Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline

           DAR ES SALAAM 

KATIBU Mkuu wa Chama cha Umma(CHAUMA),Salim Mwalimu amepokea maependekezo ya sifa na vigezo vya wanawake wanaotarajiwa kupata nafasi ya uongozi wa Viti Maalum kwa nafasi ya Udiwani,Wawakilishi wa Ubunge.

Mapendekezo hayo  yamewasilishwa Leo Julai 24,2025 Katika Ofisi za Chama Jijini Dar es Salaam na Katibu wa Kamati ,Moza Ally wa kamati aliyoiunda kama mtendaji Mkuu wa Chama.

Akizungumza  na waandishi wa habari mara baada yakupokea mapendekezo hayo Katibu Mkuu CHAUMMA Salim Mwalimu amewata wanawake kutojielekeza kwenye Viti Maalum kwani wanawake Wanauwezo wakushinda kwenye majimbo hivyo wajitokeze kushindana kwenye majimbo kwani CHAUMMA wameweka utaratibu kwa wanawake kufikiriwa.

"Katika Kamati iliyoundwa kutoa mapendekezo iliangalia utaratibu, sifa  na vigezo vya udiwani wa Viti Maalum anaetoka CHAUMMA,Uwakilishi wa Viti Maalum na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Viti Maalum anaetoka CHAUMMA",amesema

Aidha,amesema kwamba kamati ilikuwa na wanawake ambao walishawahi kuwa Wabunge na  Madiwani katika nafasi mbalimbali za kisiasa.

Pia amesema kwamba Uteuzi wa Viti Maalum unatakiwa kuwa wa wazi,Shirikishi na jumuishi kama jambo linawahusu wanawake hivyo wapewe nafasi wanawake wenyewe kwa mapendekezo pamoja na kutoa ushauri kwa Chama namna ya kupata wagombea kwa nafasi za wanawake   

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

MWAKIPOSA ASHINDA NAFASI YA UWENYEKITI WA WENYEVITI WA SERIKALI YA MTAA MKOA WA DAR ES SALAAM

KILINDI BARABARA BADO NI CHANGAMOTO