MANARA:TUJIULIZE TANZANIA IMETOKA WAPI.
Timothy Marko DmNews online
DAR ES SALAAM
DIWANI wa kata ya Karikoo Jijini Dar es Salaam Haji Sunday Manara amewataka Vijana Kudumisha Amani nakusisitiza kuwa Suala la Amani nikipaumbele cha kwanza katika misingi ya kitaifa.
Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo Oktoba 19,2025 Manara amesema enzi ya Miaka ya 1980 Tanzania ilikuwa inapitia Changamoto Ikiwemo ukosefu wa Chakula Watu walikuwa Wakipanga foleni kwaajili ya unga na Sukali .
,,
Nchi hii imepitia wakati mgumu sana, lakini kipindi chote hicho Haki haikudaiwa kwa Maandamano, Changamoto za Ajira ni Changamoto za kidunia ,, Amesema Manara .
Manara akisisitiza Suala la Amani utaitwa Chawa lakini ukweli tumekula unga wa njano na kuwa Katika Nchi ya Tanzania hakuna kitu cha kudaiwa isipokuwa Amani.
,,
Kabla ya Kuandamana Nilazima tujiulize Mwaka 1980 Tanzania ilikuwaje Mwaka 1987Ndio tulikuwa nasera za kuleta Bidhaa,Hakuna kitu cha kudaiwa isipokuwa Chakula ,, Amebainisha Manara.

Comments
Post a Comment