Posts

Showing posts from September, 2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA TEMEKE AAHIDI UJENZI WA KITUO CHA KISASA STENDI YA DALADALA TEMEKE MWISHO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline              DAR ES SALAAM  MGOMBEA Ubunge Jimbo la Temeke kupitia  Chama Cha Wakulima(AAFP),Yusuph Rai amesema kwamba endapo atapata ridhaa ya kuwa Mbunge katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29,2025 atahakikisha Temeke Mwisho kunajengwa kituo kikubwa Cha daladala chenye hadhi na thamani ya Wilaya ya Temeke pamoja na  kituo kitakachounganisha magari yanayokwenda Mikoa ya  Kusini ili kuongeza thamanj ya mapato ya Jimbo  Hilo. Amezungumza hayo leo Septemba 15,2025 katika uzinduzi wa kampeni za Jimbo la Temeke zilizofanyika katika Viwanja vya Tandika Sokoni kata ya Tandika Jijini Dar es Salaam. Aidha ,amesema kwamba soko la Tandika ndio kariakoo ya Temeke,hivyo akipata nafasi ya kuwa mbunge atahakikisha soko hilo kuwa kubwa na liwe la kimataifa pamoja na kuishawishi serikali ili Soko hilo liwe kitovu cha biashara. Pia amesema kwamba Tandika imekuwa na changamoto ya maji safi na salama  kwa siku nying...

“Doyo. Sitavumilia Mfumo wa Stakabadhi Ghalani, Madini ya Tanzanite Yawanufaishe Wananchi wa Manyara”

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                   BABATI ,MANYARA MGOMBEA  Urais kupitia Chama cha NLD, Mhe. Doyo Hassan Doyo, leo tarehe 15 Septemba 2025, ameendelea na ziara yake ya kampeni mkoani Manyara katika vijiji vya Bonga, Hala, Nakwa, Sigino na Posta (Singu), na kukamilisha mkutano wake wa kampeni Babati mjini. Akihutubia wananchi mjini Babati, Mhe. Doyo alilalamikia mfumo wa stakabadhi ghalani unaotumika katika zao la mbaazi, akisema kuwa mfumo huo hauwanufaishi wakulima wadogo wa Manyara na Tanzania kwa ujumla. Alifafanua kuwa wakulima hulima kwa gharama zao, hununua pembejeo kwa fedha zao na hulinda mashamba yao kwa gharama kubwa, lakini wanapofika sokoni hulazimishwa kuuza mazao yao kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani kwa bei ya chini.  “Wakati mnapouza kilo kati ya shilingi 700 hadi 1,700 tu, wapo wanunuzi binafsi waliokuwa tayari kulipa hadi shilingi 3,500 kwa kilo. Hii ni dhuluma kwa mkulima. Nikipewa ridhaa ya...

NJAMA AAHIDI MAKUBWA KOROGWE NDANI YA SIKU 100 AKIPATA RIDHAA YA WANANCHI

Image
Mgombea Mwenza wa urais Balozi              Dkt. Nchimbi (kushoto) akimnadiCPA Njama. Na Yusuph Mussa,DmNewsonline                            Korogwe MGOMBEA ubunge Jimbo la Korogwe Mjini mkoani Tanga CPA Charles Njama ameahidi makubwa ndani ya siku 100 za uongozi wake kwa kuhakikisha kuwa Mradi wa Maji wa Miji 28, na Mradi wa Maji kwa kutumia chanzo cha Mto Ndemaha itakuwa imekamilika, na wananchi wa Korogwe shida ya maji itabaki historia kwao. Pia,  barabara inayojengwa kwa kiwango cha lami kutoka barabara kuu hadi Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Magunga yenye kilomita 2.7, na ile ya kutoka Kibo, Mtonga- Mgombezi- Bagamoyo, njiapanda ya Handeni yenye urefu wa kilomita 6.7, ndani ya siku 100 za uongozi wake, Mkandarasi atakuwa kazini. Ameyasema hayo Septemba 15, 2025 mbele ya Mgombea Mwenza kiti cha urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kwen...

MGOMBEA URAIS WA ADA-TADEA AAHIDI TANZANIA KUMILIKI SATELLITE YAKE ENDAPO ATAPATA RIDHAA YA KUWA RAIS

Image
   Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline          DAR ES SALAAM   MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha African Democratic Alliance (ADA -TADEA), Georges Bussungu amesema kwamba endapo atapata ridhaa ya kuwa  Rais atahakikisha Tanzania inamiliki Satellite yake Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni za Chama hicho Leo Septemba 14,2025 katika Viwanja vya Zakhem Mbagala Jijini Dar es Salaam amesema kwamba vipaumbele vya Ilani ya chama  itahakikisha inajenga kituo maalum cha teknolojia nchini kitakachoitwa Bongo Selcom City ambacho kitasimamia  masuala yote yahusuyo Teknolojia kwani teknolojia ndio inayotumika sana duniani  Aidha amesema wataleta mapinduzi ya kifikra kwa watanzania  kwa kuanzisha elimu ya kujitegemea kuanzia elimu ya chekechea hadi chuo kikuu kwa kujifunza elimu ya nadhalia ili kuwapatia elimu iliyobora na yakujitegemea na namna  yakujiari wenyewe Pia amesema atahakikisha kuweka...

NJAMA ANATAKA USHIRIKIANO KOROGWE KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI.

Image
Njama akizungumza na wananchi wa Korogwe. Na Yusuph Mussa,DmNewsonline                      KOROGWE MGOMBEA  ubunge Jimbo la Korogwe Mjini mkoani Tanga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) CPA Charles Njama amesema atashirikiana na madiwani wenzake kuona wanaleta maendeleo kwa makundi yote ya wananchi. Na katika kuleta maendeleo hayo, atahakikisha makundi ya mamalishe, babalishe, wanawake wauza mahindi, mbogamboga, bodaboda, bajaj, maguta, na ujasiriamali mwingine, wanafanya shughuli zao za kujipatia kipato kwa kuwaboreshea mazingira na kupata mitaji isiyokuwa na riba ikiwemo fedha za asilimia 10 kutoka halmashauri. Ameyasema hayo Septemba 11, 2025 wakati wa Uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Korogwe Mjini uliofanyika Uwanja wa Sokoni mjini Korogwe, ambapo amesema changamoto kwake ni fursa, hivyo anataka kuona wananchi wa jimbo hilo wanapata maendeleo bila kuogopa changamoto zilizopo mbele yao. Njama amesema akipata ridhaa ya kuw...

WATU 33000 HUFARIKI DUNIA KUTOKANA NISHATI CHAFU .

Image
  Timothy Marko DmNewsonline                             DAR ES SALAAM  WATU  33000 hufariki Dunia kutokana na Matumizi ya Nishati Chafu kupikia Barani Afrika. Hayo yamebainishwa na KATIBU Mkuu wa WIZara ya Nishati Felician Mramba katika kongamano la Uhamasishaji wamatumizi Nishati safi ya kupikia Jijini Dar es Salaam Ambapo Amesema kuwa Matumizi ya Nishati chafu ya kupikia nikichocheo cha Uharibifu wa Mazingira. "Zaidi hekta za misitu46000 hupotea hupotea kutokana na Ukataji  miti kwa Ajili ya Mkaa"Amesema KatibuMkuu wa Wizara  ya Nishati Felician Mramba. Mhandisi Mramba Ameongeza kuwa katika kuweza kutokomeza Matumizi ya Nishati Chafu ya kupikia ikiwemo Kuni , Serikali  imeanzisha Mpango Maalum 2024-2034 kuhakikisha kila mtanzania anatumia Nishati safi ya kupikia. Amesisitiza kuwa Katika Mpango huo unalenga kupunguza Matumizi ya Nishati Chafu kutoka kaya 10 Hadi 8 zinaondokana na N...

SERIKALI YAWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA UFUGAJI WA NGURUWE.

Image
 TimothyMarko, DmNewsonline .             DAR ES SALAAM  SERIKALI imewataka Vijana kukukimbilia fursa ya Ufugaji wa Nguruwe ilikuweza kujipatia kipato kitakacho wakwamua kiuchumi. Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu wa wizara ya Mifugo na Uvuvi  Agnes Meena Jijini Dar es Salaam kwenye kongamano la Kimataifa la fursa za ufugaji wa Nguruwe Barani Afrika (The Africa international Pig conference Expo 2025)  Amesema kuwa Sekta ya Nguruwe imekuwa ikuwa kwa Kasi Ambapo Tanzania inakadiriwa kuwa na Nguruwe milioni 4.1 na kusababisha ajira kwa vijana  "Pamoja na ukuwaji wa Sekta hii ,Sekta hii ya Ufugaji wa Nguruwe inakabiliwa na Changamoto ya homa ya Nguruwe, Ukosefu wa Masoko kutoka Nje,"Amesema Katibu Mkuu wa wizara ya Mifugo Agnes Meena. Meena ameongeza kuwa Pamoja na kuwepo kwa Changamoto hizo serikali imejipanga kuimarisha Sekta hiyo . Amesisitiza kuwa Nivyema wadau wa Sekta binafsi kuweza kushirikiana serikali ili kuwekeza Sekta hiyo. N...

MWENYEKITI WA NLD ARUDISHA FOMU YA KUGOMBEA URAIS ZANZIBAR

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsOnline                  ZANZIBAR MWENYEKITI wa Chama cha NLD na mgombea urais wa Zanzibar, Mhe. Mfaume Khamis Hassan, leo amerejesha fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar. Hafla ya kurejesha fomu hizo imefanyika mbele ya Tume Huru ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), ambapo viongozi, wanachama na wafuasi wa chama hicho walihudhuria kwa wingi. Katika hotuba yake fupi baada ya kurejesha fomu, Mhe. Khamis Hassan alisisitiza dhamira yake ya kuleta mabadiliko chanya Zanzibar endapo atapata ridhaa ya wananchi. Alibainisha kuwa vipaumbele vyake vikuu vitahusisha kukuza uchumi wa visiwa kwa kuimarisha sekta ya utalii na biashara ndogondogo, kuboresha huduma za afya na elimu, pamoja na kuongeza fursa za ajira kwa vijana. Aidha, aliahidi kuendeleza mshikamano wa kitaifa kwa kuhakikisha kila raia anashirikishwa katika mchakato wa maamuzi ya kitaifa, bila kujali itikadi za kisiasa. Kwa mujibu wa chama cha NLD, s...

KONGAMANO LA KITAIFA LA WADAU WA UCHUMI WA BULUU LAFANYIKA JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline       DAR ES SALAAM  KONGAMANO la Kitaifa la Wadau wa Uchumi wa Buluu limeanza leo Septemba 10 ,2025  Jijini Dar es Salaam nw linatarajiwa kufanyika kwa siku mbili mfululizo hadi Septemba 11, 2025. Mgeni rasmi katika Kongamano Hilo ni Naibu Katibu Mkuu (Muungano) kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais,  Abdallah Mitawi  amesema  kwamba Serikali imedhamiria kutumia ipasavyo rasilimali za bahari na maji ya ndani kwa maendeleo endelevu ya Taifa. “Uchumi wa buluu ni injini mpya ya maendeleo ya Tanzania. Ukitumiwa kwa ufanisi unaweza kuongeza ajira, kukuza biashara na kuimarisha ustawi wa wananchi,” amesema Mitawi. Naye mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchukuzi, Mhandisi Shomari Shomari, amesema maboresho ya miundombinu ya bandari, reli na vyombo vya usafiri majini ni nguzo muhimu za kukuza uchumi wa buluu na kuongeza ushindani wa biashara kitaifa na kimataifa.  Aidha,ametoa wito ...

NORWAY NA HLRC WAINGIA MAKUBALIANO KATIKA KUKUZA DEMOKRASIA NCHINI.

Image
Timothy Marko DmNews online                  DAR ES SALAAM  KITUO cha Haki za binadamu Nchini LHRC kimeingia Makubaliano na Ubalozi wa Norway kuimarisha msaada wa kisheria, Haki jinai na kuimarisha wa Utawala Bora. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam Kaimu Mkurugezi wa Kituo cha Sheria na Haki za Bindamu Nchini LHRC   Fulafulue Masawe amesema kuwa Mkataba huo Wenye thamani ya Sh. bilioni 61.9 unalenga kukuza Haki za Bindamu Nchini. "Nchi ya Norway imekuwa mdau Muhimu wa ukuzaji wa Demokrasia Nchini na Haki za binadamu na kukuza Misingi ya Utawala Bora Nchini"Amesema  Masawe.  Masawe Ameongeza kuwa Nchi ya Norway pia imekuwa mstari wa mbele katika Masuala Haki jinai, Mchakato wa Uchaguzi,Utetezi wa Haki za makundi Maalum ikiwemo Wanawake na watoto. Kwaupande wake Balozi wa Norway Nchini Tanzania Tone Tinnes amesema Mkataba huo unalenga kukuza Msaada wa kisheria, Demokrasia na Haki za Bindamu. Amesem...

MKURANGA, KUMEKUCHA ULEGA MTU WA WATU,MAMA CHATANDA AZINDUA KAMPENI RASMI.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                      MKURANGA  JIMBO la Mkuranga kumekucha ambapo Mgombea ubunge Jimbo hilo Alhaj Abdallah Hamis Ulega  amezindua rasmi kampeni za uchaguzi  wilayani humo Mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni umefanyika katika Viwanja vya shule ya msingi  Mwandege ambapo mgeni rasmi  wa uzinduzi huo wa kampeni alikuwa Mwenyekiti wa Umoja wa wanawake (UWT) CCM  Taifa Mary Chatanda   

MARY CHATANDA :ATEMA CHECHE UFUNGUZI WA KAMPENI MKURANGA

Image
Na Mwandishi wetu.DmNewsonline                      MKURANGA  MWENYEKITI wa UWT CCM Taifa Mary Chatanda amesema kuwa Chama hicho  kimewateua wagombea wanaokubalika Kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Urais ,ubunge na Udiwani wa mwaka huu Amesema kuwa kutokana na Chama kupeleka wagombea wanaokubalika Jukumu kubwa la wananchi kuhakikisha wanawachagua wagombea wa Chama hicho kwa kuwapa kura nyingi za ndio ifikapo otoba 29,mwaka huu Chatanda ameyasema hayo leo katika uzinduzi wa kampeni Jimbo la mkuranga ambapo yeye ndie alikuwa mgeni rasmi nakwamba katika kipindi Cha uongozi wake Dkt .Samia  Suluhu Hassan ameweza kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ambayo kimsingi iliachwa na mtangulizi wake Hayati Dkt .John Magufuli Chatanda amesema kuwa mkoa wa Pwani kupitia Wabunge katika majimbo yaliyopo ndani ya mkoa huo wamefanya kazi nzuri sana na wengi wao wameweza kuteuliwa kuwa mawaziri kutokana na uchapakazi wao . Kada huyo pi a...

ULEGA: KATIBA MPYA UHAKIKA KWA DKT SAMIA

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                 MKURANGA  MGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Jimbo la mkuranga Alhaj Abdallah Ulega amewataka watanzania kama wanataka katiba mpya basi wanapaswa kumchagua Dkt Samia Suluhu Hassan kwani yeye alikuwepo katika machakato wa katiba . Amesema hata katika uzinduzi wa kampeni kitaifa zilizofanyika jijini Dar es salaam Agost 27,2025 katika Viwanja vya Tanganyika perkas amesema ametamka kuwa katika siku 100 za mwanzo atahakikisha anafufua mpya mchakato wa katiba mpya. Ulega amesema maneno haya leo Septemba 6,2025 katika uzinduzi wa kampeni Jimbo la mkuranga ambapo amesema Dkt .Samia ni muumini wa mariadhiano na akitamka anatenda huyo ndio daktari Samia . Amesema kuwa jambo Moja tu kwa watanzania na wananchi wa Jimbo la mkuranga ni kuhakikisha wanampigia kura za kutosha mgombea wa Chama Cha Mapinduzi CCM ili aweze kutimiza mambo makubwa  kwa ajili ya maendeleo ya wananchi . Pia...