Posts

Showing posts from September, 2025

HUNGARY KUWEKEZA UPATIKANAJI WA MAJI ZIWA VICTORIA .

Image
  Timothy Marko DmNewsonline         DAR ES SALAAM. KATIKA kuhakikisha Sekta ya Maji inaimarika serikali  kwa Kushirikiana na Nchi ya Hungary imeingia makubaliano ya kuboresha Maeneo ya Ukanda wa Ziwa Victoria. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam Mara baada makubaliano hayo Jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabiti Kombo amesema Makubaliano hayo ya Dola milioni 55 za kimarekani yanalenga kukuza Sekta ya Maji Uwekezaji wafedha hizo kutawezesha Makampuni mbalimbali kutoka Hungary kuwekeza Nchini Tanzania. "Makubaliano haya ya Leo yatawezesha Makampuni kutoka Hungary kuja kuwekeza Nchini Tanzania"  AmesemaWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi  Mahamoud Thabiti Kombo.  Balozi Thabiti Kombo Ameongeza kuwa Sambamba na Makubaliano ya Uwekezaji wa Makampuni kuwekeza Nchini Tanzania pia Nchini hiyo imeingia makubaliano na Nchi ya Tanzania Ku...

Mkurugenzi STAMICO Afanya Mazungumzo na Wanawake Wachimbaji wa TAWOMA

Image
‎ Na ‎Richard Mrusha,DmNewsOnline Geita ‎  Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Bw.  CPA Venance Mwase amekutana na kufanya mazungumzo na wanachama wa Chama cha Wanawake Wachimbaji Madini Tanzania (TAWOMA) katika Maonesho ya Nane ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini yanayoendelea mkoani Geita. ‎ ‎Katika mazungumzo hayo, CPA Venance Mwase  aliwapongeza wanawake hao kwa kazi nzuri wanayoifanya katika sekta ya madini huku akisisitiza dhamira ya STAMICO kuendelea kuwaunga mkono kwa vitendo. ‎ ‎“Kushukuru ni jambo jema, lakini niwaambie kuwa mnafanya kazi nzuri sana. Ukiona Salma anakuja kwangu na anatoka na kitu, jua nahamasishwa na mnachokifanya. Ahadi yangu kwenu ni kuendelea kuwashika mkono kwa sababu hamjawahi kuniangusha,” alisema CPA Mwase ‎ ‎Aliongeza kuwa serikali kupitia STAMICO itaendelea kuwapa fursa zaidi wanawake wachimbaji, hasa wale wanaojitokeza na kuonyesha juhudi. Alitaja kuwa STAMICO imejipanga kuwasaidia zaidi, ikiwa ni...

TASAC Yawataka Wachimbaji Kutotumia Kampuni Binafsi Kusafirisha Kemikali na Vilipuzi

Image
Richard Mrusha,DmNewsOnline GEITA  Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limepiga marufuku kwa kampuni binafsi kujihusisha na usafirishaji wa kemikali na vilipuzi vinavyotumika katika shughuli za uchimbaji migodini, likisisitiza kuwa jukumu hilo ni la TASAC pekee. Mkurugenzi wa Huduma za Shirika hilo, Hamid Mbegu ameyasema hayo  katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofanyika mkoani Geita.  Amesema kwa mujibu wa Sheria ya Uwakala wa Meli, Sura ya 415, TASAC imepewa mamlaka ya kusimamia kwa ukamilifu usafirishaji na uondoshaji wa shehena zote hatarishi zikiwemo baruti na kemikali.  "Baadhi ya shehena hizi ni sumu na zina madhara makubwa."  Serikali kupitia TASAC ndiyo yenye mamlaka ya kusimamia hatua zote za uondoshaji wake. Makampuni yanayopitisha kemikali hizi kupitia kampuni binafsi yanakiuka sheria," alisisitiza Mbegu. Ameongeza kuwa baadhi ya makampuni yamekuwa yakisafirisha kemikali hatarishi kama Sodium Cyanide kupitia njia z...

MWINGIRA : TBA KUENDELEA KUTEKELEZA MIRADI MIKUBWA YA MAENDELEO

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline GEITA Afisa Habari wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Adam Mwingira, amesema TBA inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo ikiwa ni sehemu ya maboresho katika sekta ya ujenzi wa miundombinu ya umma. Ameyasema hayo leo wakati akizungumza katika Banda la TBA kwenye Maonesho ya Madini ya Geita, alipokuwa akipokea ugeni wa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko. Akielezea mafanikio na mwelekeo wa taasisi hiyo, Mwingira amesema TBA ina mradi mkubwa unaotarajiwa kuanza kutekelezwa hivi karibuni, na kushukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mazingira bora ya utekelezaji wa miradi hiyo kupitia mabadiliko ya sheria ya Majengo, GN Na. 595 ya mwaka 2023. "Marekebisho haya yameruhusu TBA kushirikiana na sekta binafsi pamoja na taasisi za kifedha, jambo ambalo litaongeza kasi ya utekelezaji wa miradi kwa ubora na kwa wakati," amesema Mwingira. Aidha, amewakaribisha wawekezaji wote...

BoT YAWATAKA WACHIMBAJI WA MADINI KUJIUNGA KWENYE MFUMO RASIMI

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline GEITA: BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imewataka wachimbaji wa madini, hususan wa dhahabu, kujiunga katika mfumo rasmi wa kifedha kwa kuuza dhahabu zao moja kwa moja kwa Benki Kuu ili kusaidia kukuza akiba ya fedha za kigeni na kuimarisha uchumi wa taifa. Meneja wa Uhusiano wa Umma na Itifaki wa BOT,  Victoria Msina, amesema hayo alipokuwa akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko alipotembelea banda la benki hiyo katika Maonesho ya Nane ya Madini yanayomalizika leo, Septemba 28, 2025. Msina amesema BoT kwa sasa imejikita katika kununua dhahabu kutoka kwa wachimbaji wadogo na wa kati, na kuwaelimisha kuhusu matumizi sahihi ya mifumo ya kifedha, ikiwemo uwekezaji katika dhamana za serikali. Amesema Elimu hiyo inatolewa katika vituo mbalimbali vya BoT nchini pamoja na kwenye maonyesho na mikutano ya sekta ya madini. Pia amesema katika maonesho hayo wachimbaji mbalimbali wamejitokeza katika banda la BOT kupata ufad...

*Othman Masoud: Uchumi wa Zanzibar Utapanuka Tukitumia Rasilimali za Bahari kwa Ufanisi*

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline       ZANZIBAR MGOMBEA Urais wa Chama cha ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman, ameahidi kuligeuza zao la bahari, hususan biashara ya dagaa, kuwa sekta rasmi na yenye mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Zanzibar. Akizungumza na wavuvi na waanikaji wa dagaa katika eneo la Mangapwani, Wilaya ya Kaskazini B, Unguja, Othman alisema rasilimali za bahari za Zanzibar zimesalia kuwa wimbo wa kisiasa bila utekelezaji, jambo linalowanyima wananchi fursa ya kufaidika moja kwa moja. “Dagaa ni biashara kubwa sana inayoweza kuingiza kipato kikubwa kwa wananchi wetu na kusaidia kukuza uchumi wa nchi. Lakini kutokana na mifumo mibovu, wageni ndio wanachukua nafasi huku wavuvi wetu wakiendelea kunyanyaswa,” alisema Othman. Mgombea huyo aliongeza kuwa Serikali ya ACT Wazalendo itahakikisha wavuvi na waanikaji wa dagaa wanawekewa mazingira bora ya kufanya kazi zao, ikiwemo mabanda ya kisasa ya uanikaji, miundombinu ya kuhifadhi mazao ya baharini, pamoja na u...

JAMII IMETAKIWA KULEA WATOTO KATIKA MISINGI BORA YA IMANI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline             DAR ES SALAAM  JAMII imetakiwa kulea watoto katika misingi ya Imani pamoja kuzingatia haki za binadamu hii inawajenga watu wote  katika misingi bora yenye hofu ya Mungu bila kujali dini. Masuala ya malezi katika misingi ya kidini ni eneo muhimu  linaloanzia katika familia,tulee watoto wetu katika misingi ya Imani itawajenga watoto kutambua uwepo wa watu wengine lakini pia kuwa na ufahamu wa kutambua mipaka yake namna anavyoabudu lakini pia malezi ni msingi muhimu sana wa kuleta amani katika jamii. Hayo yamebainishwa   Septemba 27,2025 na  Mwenyekiti  Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ,Mathew Mwaimu (Jaji Mstaafu) wakati wa kutoa mada ya Haki za binadamu katika Mkutano Mkuu wa 54 wa Jumuiya ya Waislamu wa Ahmadiyya Tanzania unaoendelea Kitonga Kata ya Msongola Manispaa ya Ilala Jijini Dar es Salaaam , Amesema kwamba jukumu la msingi la  Tume ya Haki za Binadamu na Utawa...

MHIFADHI MDOE ATOA ELIMU KUHUSU UHIFADHI WA MAZINGIRA KATIKA MAONESHO YA MADINI GEITA

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline GEITA Mhifadhi Mwandamizi kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Juma Mdoe amesema kuwa wachimbaji wa madini ni miongoni mwa wadau wakuu wa rasilimali za misitu kutokana na shughuli zao kuhusisha matumizi makubwa ya miti, hivyo wana wajibu wa kushiriki katika juhudi za uhifadhi wa mazingira kwa kurudisha uoto wa miti wanaoiharibu. Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika mkoani Geita, Mdoe alisema kuwa wameamua kushiriki kwenye maonesho hayo ili kutoa elimu kwa wadau mbalimbali, hususan wachimbaji, kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira. Alisema kuwa wachimbaji wengi hutumia miti kutengeneza maboksi ya kuzuia udongo kusitiririka kwenye migodi, na hivyo wanapaswa kutambua kuwa wanalo deni la kuhakikisha uoto wa asili wa miti unarejeshwa.  “Wanapaswa kutambua kuwa wana wajibu wa kurudisha uoto wa miti na kuendelea na juhudi za uhifadhi kwa kupanda miti kwa wingi. Wao ni watumiaji wakubwa wa m...

ELIMU YAENDELEA KUTOLEWA KWENYE BANDA LA BoT

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline Geita Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Zena Ahmed Said, ametembelea Banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika mkoani Geita. Akiwa kwenye Banda la BoT, ameshuhudia wananchi wakipewa elimu kuhusu masuala ya fedha, ikiwemo jinsi ya kuwekeza fedha zao. Amesema kuwa kuna watu wengi wenye fedha, lakini hawajui jinsi ya kuziwekeza. Hata hivyo, kupitia maonesho haya wanapata fursa ya kufundishwa namna ya kuwekeza kwenye dhamana za Serikali ambazo huwapatia faida kubwa, tofauti na kuwekeza sehemu zisizo rasmi. Ameongeza kuwa wananchi watembelee banda hilo ili wafundishwe jinsi ya kujiepusha na utakatishaji wa fedha, kwa sababu ni suala linaloweza kuiingiza nchi kwenye matatizo makubwa. Amesema kuwa elimu inayotolewa hapo inalenga masuala ya kifedha pamoja na mengine mengi ya kifedha, na inatolewa bure. Hivyo, wananchi wanapaswa kufika kwa wingi ili wasikose fursa hiy...

DC KOMBA AIPONGEZA BoT

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline GEITA Mkuu wa wilaya ya Geita Hashim  Komba Ameipogeza  BoT kwa namna ambavyo wameendelea kuelimisha Umma kuhusu taasisi yao kwa wananchi wanaotembelea Banda Hilo ndani ya viwanja vya Samia Suluhu Hasan kwenye maonesho ya nane ya Teknolojia ya Madini Mkoani geita. Komba amepata Fursa ya ya kuzungumza na watumiahi wa Benki na Miongoni mwa akitengo alichotembelea ni kitengo cha usimamizi wa masuala ya fedha ,usimamizi wa masusla ya benki na mikopo Amesema Kumekuwa na changamoto kubwa sana kwenye maeneo yetu juu ya uwepo wa taasisi ambazo hazijasajiliwa na kutoa mikopo kwa riba kubwa Zaidi ,zinawafilisi wananchi kwa kutofuata taratibu Amesema  BoT wanancho kitengo maalum ambacho kazi yake ni kuhakikisha kwamba kunakuwa na taasisi zinazotoa mikopo kwa wananchi zikiwa zimesajiliwa na zikiwa zinazingatia sera za kifedha za Taifa letu kwa ujumla. Amesema Moja ya jambo kubwa lililomfurahisha nikuona namna ambavyo BoT inazibiti   taasisi zi...

KOMBA ATO RAI KWA DIB KUENDELEA KUPANUA WIGO

Image
Na Richard Mrusha,DmNewsOnline Geita Mkuu wa Wilaya ya Geita, Hashim Komba, ametoa rai kwa Bodi ya Bima ya Amana kuendelea kupanua wigo wa huduma zake ili kuhakikisha mitaji ya Watanzania, hususan katika vikundi vidogo vya kifedha kama SACCOS na VICOBA, inabaki salama.  Hayo ameyaema Leo Sep 26,2025 wakati wa Ziara ya kutembelea Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini Mkoani geita   amesaema Watanzania wengi bado wanawekeza fedha katika maeneo ambayo hayajasajiliwa rasmi, hali inayowaletea hasara kubwa pale vikundi hivyo vinapovunjika. Amesema   kuwa katika ofisi za wakuu wa wilaya, mara kwa mara wananchi wamekuwa wakifika kulalamikia kupoteza akiba kubwa walizowekeza Unampokea mwananchi anakwambia amewekeza milioni 30 kwenye kikundi cha kifedha lakini zote zimepotea. Tunaanza kuhangaika kumtafuta kiongozi wa kikundi bila mafanikio. Ni wakati sasa wa kuongeza kasi ya kuhakikisha mitaji ya Watanzania inalindwa. Ameongeza kuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inapaswa...

WAKAZI UKUMBISIGANGA WAFURAHIA UJENZI KITUO CHA AFYA

Image
Na Allan Kitwe, Tabora WAKAZI wa Kata ya Ukumbisiganga Wilayani Kaliua wameeleza kufurahishwa na hatua ya serikali ya awamu ya sita kupeleka zaidi ya shilingi milioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya ili kuboresha huduma za afya. Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wananchi wameeleza kuwa Kata yao ni miongoni mwa kata zilizokuwa na changamoto kubwa ya upatikanaji huduma za afya, lakini serikali imesikia kilio chao na kuanza ujenzi wa kituo hicho. Mohamed Ramadhan (57) mkazi wa Kijiji cha Usinga katika kata hiyo, ameishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea kituo hicho ambacho kitasaidia kuokoa maisha ya akinamama, wajawazito, wazee na watoto. Ameeleza kuwa wakazi wa kata hiyo yenye vijiji vinne vya Ukumbi-Siganga, Lumbe, Usinga na Ukumbi-Kakoko wamekuwa wakipata huduma za afya kwenye zahanati lakini wanapohitaji huduma za matibabu makubwa hawazipati. ‘Vijiji vyetu vipo umbali wa zaidi ya km 90 kutoka Makao Makuu ya Wilaya, hali inayopeleke...