HUNGARY KUWEKEZA UPATIKANAJI WA MAJI ZIWA VICTORIA .
Timothy Marko DmNewsonline DAR ES SALAAM. KATIKA kuhakikisha Sekta ya Maji inaimarika serikali kwa Kushirikiana na Nchi ya Hungary imeingia makubaliano ya kuboresha Maeneo ya Ukanda wa Ziwa Victoria. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam Mara baada makubaliano hayo Jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabiti Kombo amesema Makubaliano hayo ya Dola milioni 55 za kimarekani yanalenga kukuza Sekta ya Maji Uwekezaji wafedha hizo kutawezesha Makampuni mbalimbali kutoka Hungary kuwekeza Nchini Tanzania. "Makubaliano haya ya Leo yatawezesha Makampuni kutoka Hungary kuja kuwekeza Nchini Tanzania" AmesemaWaziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahamoud Thabiti Kombo. Balozi Thabiti Kombo Ameongeza kuwa Sambamba na Makubaliano ya Uwekezaji wa Makampuni kuwekeza Nchini Tanzania pia Nchini hiyo imeingia makubaliano na Nchi ya Tanzania Ku...