TABIO NA ENVIROCARE YAWAPIGA MSASA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MBEGU ZA ASILI
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline.
TAASISI isiyokuwa ya kiserikali ya Tanzania Allience for Biodiversity (TABIO) chini ya uwezeshwaji wa shirika la Afrikani Biodiversity Network (ABN) na ENVIROCARE leo Disemba 18, 2023 wameendesha mafunzo Kwa waandishi wa habari wanaondika Habari za kilimo hai Kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu mbegu za asili.
Akizungumza katika warsha hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam Leo Disemba 18 ,2023 , mkurugenzi na mratibu wa Tabio Abdallah Mkindi Amesema kuwa waandishi wa habari ni watu muhimu sana hivyo wao kama taasisi wameona nimuhimu kuwapa elimu hiyo.
Amesema Kwa kutumia kalamu zao na vyombo vingine vya habari wanauwezo mkubwa wa kuwafikia wadau mbalimbali hasa katika kujua umuhimu wa mbegu za asili
"Kimsingi mbegu za asili zimetoka katika uasili wake ambao mi polini na wao kama Taasisi kazi yao ni kuziweka kwenye mfumo mzuri ."Amesema
Kwaupande wake David Manongi mtaalamu wa mbegu tafiti ,uzalishaji na sera kutoka Tabio,Amesema mafunzo hayo yataendelea kuwajengea uwezo waandishi juu ya mbegu za asili..




















Comments
Post a Comment