TIRA YAWAKUTANISHA WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI ,WAJIPANGA BIMA UWE WIMBO WA WATANZANIA WOTE.
Na Mwamdishi wetu,DmNewsonline DODOMA AHADI ya serikali ya kutoa Bima ya Afya kwa wote ikiwa mbioni kuelekea kutimizwa, Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) nayo imeapa kudhibiti soko la bima nchini ili kuimarisha usalama na uchumi wa nchi. Akizungumza kwenye semina ya siku mbili iliyofanyika Novemba 18-19 mwaka huu, katika ukumbi wa mikutano wa jengo la ofisi za Mamlaka hiyo maarufu TIRA BIMA HOUSE lililopo Njedengwa, Kamishna wa TIRA, Dkt. Baghayo Saqware amesema hatua hiyo itaondoa kabisa udanganyifu katika soko la bima. Sambamba na hilo itawajengea ufahamu wananchi ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwajibikaji katika sekta ya bima. "Malengo ya semina hii kwenu wahariri, tushirikiane kufikisha elimu ya bima kwa wananchi, hilo likifanyika ipasavyo dhana potofu kuhusu bima zitaisha."amesema "Wanahabari mkichochea elimu ikaenea kwa watanzania wote, uhitaji wa bima utaongezeka hata ufahamu kw...