Posts

MLAWA AWATAKA VIJANA WILAYANI RUFIJI _ PWANI KUSIMAMIA MAADILI

Image
            Na Eliasa Ally DmNewsOline                   PWANI  MDAU  wa Maendeleo Wilaya ya Kilolo, Aidan Mlawa, amewataka vijana kushirikiana na serikali katika kulinda maadili ya jamii na kujikita katika shughuli za ujasiriamali kwa jail ya kujikwamua kiuchumi. Akizungumza februari 25,2025  katika Kanisa la KKKT  Usharika wa Ikwiriri, Dayosisi ya Pwani, wilaya ya Rufiji wakati wa uzinduzi wa albamu ya kwaya ya vijana, ya lkwirri Mkoa wa pwani wilaya ya Rufiji Mlawa alichangia shilingi laki tano (500,000) na kuahidi kununua mashine ya kusaga ili kusaidia kukuza kundi hilo. Katika mchango wake kwa kanisa, Mlawa pia ameahidi kugharamia ujenzi wa jengo la choo kwa asilimia 75, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya jamii na wadau wa maendeleo katika kuboresha miundombinu ya taasisi za kidini. Aidha, amewataka vijana kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu...

KADA CCM ATOA TUHUMA KWA MWENYEKITI CCM RORYA,MWENYEWE AJIBU MAPIGO.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsonline                  DAR ES SALAAM  KADA wa Chama cha Mapinduzi CCM kutoka wilayani Rorya mkoani Mara Baraka Peter Otieno amekiomba  chama hicho kuunda chombo  maalumu cha kuchunguza mwenendo wa kisiasa unaoendelea wilayani humo.  Ombi hilo linatokana na uwepo wa taarifa zinazomtuhumu mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilaya ya rory  Ongujo wakibara pamoja na mbunge wa jimbo hilo jafar chege kuwa wamekuwa wakikivuruga chama hicho kwa maslahi yao binafsi. Akizungumza leo februri 25,2025 jijini Dar es salaam waandishi  wa habari  otieno amedai viongozi hao wamekuwa wakitumia fedha na nafasi zao kuvunja katiba ya chama hicho na kuondoa utulivu uliopo .   Akieleza zaidi  februri 21 mwaka huu chama hicho taifa kiliandaa mafunzo maalumu kwa watendaji wa chama ngazi ya tawi na kata kwa gharama za chama lakini cha kusikitisha viongozi hao walitoa fedha sh 50000 kwa kila mjum...

RAIS SAMIA ASIKIA KILIO CHA WANANCHI BARABARA YA SONI- BUMBULI-KOROGWE

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                   TANGA  RAIS , Dkt. Samia  Suluhu Hassan amesikia kilio cha wananchi wa Bumbuli, mkoani Tanga kuhusu ujenzi wa barabara ya Soni - Bumbuli - Korogwe (km 77), kwa kiwango cha lami ambapo ameeleza kuwa ujenzi wa barabara hiyo utajengwa kwa awamu. Akihutubia wananchi wa Wilaya ya Lushoto mkoani humo katika mkutano wa hadhara leo tarehe 24 Februari, 2025 Rais Samia  ameeleza kuwa  tarehe 06 Machi, 2025 Serikali itafungua zabuni ya kumtafuta Mkandarasi wa kujenga barabara hiyo. Dkt. Samia amesisitiza kuwa  ujenzi wa barabara hiyo utaanzia  Soni- Bumbuli (km 22) na  Kwameta - Kwashemsi (Km 9.3). “Barabara hii mwanangu January (Mbunge wa Bumbuli) amekuwa akiililia sana, baada ya kusikia kilio chake basi nikasema tangazeni, tarehe  6 mwezi ujao tunafungua tenda kutafuta mkandarasi”, amesema Dkt. Samia Aidha, Dkt. Samia ameeleza kuwa Serikali inaendelea  kuteke...

DEREVA WA LORI ALIYESAFIRISHA WAHAMIAJI HARAMU AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA MITANO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline IRINGA MAHAKAMA  ya Hakimu mkazi mkoa wa Iringa imemuhukumu kwenda jela miaka  mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 20 dereva wa gari aina ya lori  scania namba T 631 CNF Boniface Mwanjokolwa kwa kosa la kusafirisha wahamiaji  haramu 62 raia wa Ethiopia kinyume na sheria. Akisoma hukumu hiyo hakimu mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya mkoa wa Iringa  Honorios Kando alisema kuwa mshtakiwa amekutwa na hatia ya kusafirisha wahamiaji haramu kinyume na sheria no. 46 kifungu kidogo  cha 1 C cha uhamiaji no 54 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2016. Akirejea kusoma kesi namba 24260 ya mwaka 2024 iliyokuwa inamkabili mfungwa Boniface Mwanjokola hakimu Kando alisema kuwa mfungwa  alitenda kosa hilo august 2I mwaka 2024  katika eneo la sabasaba Mafinga barabara kuu ya Iringa-Mbeya akiwa anasafirisha wahamiaji haramu 62 raia wa Ethiopia wakielekea Kyela mkoani Mbeya kwa kutumia gari aina ya Lori scania aliyokuwa akiliendesha. Hak...

CHAMA CHA MAKINI KIMEWATAKA WATANZANIA KUDUMISHA AMANI NA UTULIVU TUNAPOEKEA UCHAGUZI MKUU

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline            DAR ES SALAAM  MWENYEKITI  wa Chama Cha Makini (Taifa) Coaster Jimmy Kibonde amewataka watanzania kudumisha amani,utulivu na mshikamano tunapoelekea katika kipindi cha Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Akizungumza na Mwandishi wa DmNewsOnline  leo Februari 24,2025  Mwenyekiti wa Chama hicho amesema kuwa dira ya Chama ni kuwahimiza,kuwashawishi na kuwawezesha watanzania kupata Elimu na hasa elimu ya Sayansi na Teknolojia. Kibonde amesema vyama vya siasa vipo 19 kikiwemo Chama Cha Makini kwahiyo tunawaomba watanzania kukiunga mkono Chama cha makini popote alipo kwa kusikiliza sera za chama hicho kwani kinaongozwa na viongozi makini. "Sisi Chama Cha Makini tutashiriki  kikamilifu uchaguzi na tutasimamisha wagombea  wenye sifa kwa nafasi ya Urais,Wabunge na Madiwani Tanzania Bara na Zanzibar",amesema Kibonde. Ameongeza kuwa wanatarajia kufanya Mkutano Mkuu wa Kamati Kuu...
Image
ENDELEZENI MAFUNZO YA DINI -MAJALIWA   Asema ushiriki wa Rais Dkt. Samia kwenye tuzo hizo ni kielelezo cha namna anavyothamini na kuiishi Imani ya Dini ya Kiislam na uhifadhi wa Qur’aan_   Asema tuzo hizo zinaimarisha imani ya dini na uwezo kwa vijana. Na Mwandishi wetu,DmNewsonline               DAR ES SALAAM    WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kufundisha na kuimarisha elimu ya dini ili kutoa fursa kwa watoto na vijana kupata elimu hiyo na kuwaandaa kuwa watu wema.   Ametoa wito huo leo Jumapili (Februari 23, 2025) alipomwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha Tuzo za 33 za Kimataifa za Kuhifadhi Qurani Tukufu. yanayofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.   “Jukumu la kuhakikisha maadili bora ni la kwetu sote, madhehebu ya dini yakiwa na mchango mkubwa. ”   Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amehimiza madhehebu yote ya din...

NLD HAWATASHIRIKIANA NA VYAMA VINGINE VYA SIASA

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline                  DAR ES SALAAM  CHAMA Cha National League for Democracracy kimetangaza rasmi kutoshirikiana na chama chochote kile Cha siasa ila kitashiriki uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025. Maamuzi hayo yametokana na kwamba NLD ni mhanga wa mashirikiano yaliyofanywa mwaka 2015 walipoingia kwenye mashirikiano na vyama vya siasa nchini yaliyopachikwa jina la UKAWA. Hayo yamebainishwa Leo Februari 23,2025 na Katibu Mkuu Doyo Hassan Doto  wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kamati Kuu ya chama hicho iliyokutana  Buguruni Jijini Dar es Salaam. Katibu Mkuu huyo amefafanua kwamba kufuatia tamko la Mwenuekiti Taifa wa CHADEMA Tundu Lisu alilolitoa hivi karibuni"No reform,no election",hii ni agenda ya Chadema siyo ya Vyama vya siasa. "NLD hatujaunga mkono msimamo huo,tutaingia kwenye uchaguzi kwa kuwaeleza wananchi sera kwa ajili ya kupata nafasi mbalimbali za uongozi",amesema Doyo Aidha ,Do...