Posts

KAMPUNI YA ORYX YAWAKUMBUKA VIONGOZI WA DINI KILIMAJARO , YAWAPATIA MITUNGI YA GESI 1000

Image
Na Mwandishi Wetu, DmNewsOnline KILIMANJARO KAMPUNI ya Oryx Gas kwa kushirikiana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Kilimanjaro Shally Raymond wamekabidhi mitungi ya gesi ya kupikia 1000 pamoja na majiko yake bure kwa viongozi wa madhehebu ya dini mbalimbali pamoja na wajasiriamali mkoani Kilimanjaro ,lengo likiwa kulihusisha kundi kulinda na kutunza mazingira kwa kutotumia kuni na mkaa. Akizungumza katika hafla ya ugawaji wa mitungi hiyo ya gesi iliyofanyika katika Chuo cha Polisi(CCP) mkoani Kilimanjaro, Naibu Waziri wa Nishati Judith Kapinga ambaye alikuwa mgeni rasmi ameeleza kwa kina kuhusu umuhimu wa viongozi wa dini kushiriki katika kuihamasisha jamii kutumia nishati safi ya kupikia. Amefafanua kuwa viongozi wa dini  ni watu wa thamani sana na  watu wanawathamini na  kuwasikiliza, hivyo  viongozi wetu wa dini wanayo nafasi kubwa ya kushiriki katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupika sambamba na kuendelea kuiambia jamii isiendelee kutumia k...

TEMBO AONGOZA MIGONGANO BINADAMU,WANYAMAPORI

Image
Selemani Msuya,DmNewsOnline  BAGAMOYO IMEELEZWA kuwa asilimia 80 ya migongano baina ya binadamu na wanyamapori nchini inahusisha mnyama tembo, huku simba, boko, mamba, fisi na nyati wakichangia asilimia 20. Hayo yamesemwa na Ofisa Uhifadhi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Isaack Chamba wakati akiwasilisha mada kwenye semina ya waandishi wa habari wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira Tanzania (JET), mwishoni mwa wiki wilayani Bagamoyo mkoani Pwani. Mafunzo hayo yameandaliwa na JET kwa ufadhili wa Mradi wa Kupunguza Migongano Baina ya Binadamu na Wanyamapori unaotekelezwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa niaba ya Serikali ya Ujerumani (MBZ). Ofisa huyo amesema katika matukio zaidi ya 11,633 yaliyotokea kuanzia mwaka 2016 asilimia 80 yamehusisha tembo, ambapo ameweka wazi kuwa wananchi wameingia katika makazi ya wanayama. Chamba ametaja wanyama wengine ni Simba asilimia 6, Kiboko asilimia 5, Nyati asilimia 4, Mamba asilimia 3 na...

DKT. BITEKO ASISITIZA UMUHIMU WA EREA SEKTA YA NISHATI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline          NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amekutana na kuzungumza na Katibu Mtendaji wa Taasisi ya Udhibiti wa huduma za Nishati kwa nchi za Afrika Mashariki (EREA) Dkt. Geoffrey Mabea leo tarehe 26 Februari, 2024 jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimejadili masuala mbalimbali ya nishati kwa nchi wanachama na umuhimu wa kujenga uwezo wa Wataalam katika Sekta ya Nishati ili kuongeza tija na huduma bora kwa wananchi.   Kikao hicho  kimehudhuriwa na Waziri wa Maji, Nishati na Madini wa Zanzibar Mhe. Shaib Kaduara na Wataalam kutoka EREA.

KASSIM MAJALIWA APIGILIA MSUMARI,AWATAKA TANAPA KUSIMAMIA SHERIA KAMA ZILIVYOPITISHWA NA BUNGE

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) amewataka Makamanda wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kuratibu maeneo yao vizuri na kusimamia sheria za uhifadhi kama zilivyopitishwa na Bunge ili maliasilia zilizomo ziendelee kuleta tija kwa taifa, ameyasema hayo jana Februari 25.02.2024 aliposimama kuwasalimia wananchi wa kijiji cha Sitalike akiwa    katika safari ya kikazi kuelekea kijiji cha Mpimbwe kilichopo Jimbo la Kavuu Mkoani Katavi. Akiwa amesimama kusikiliza kero katika kijiji hicho cha Sitalike kilichopo mpakani mwa Hifadhi ya Taifa Katavi, wananchi walimuomba aseme neno ili wapate fursa ya kuvua samaki mto Katuma ambao unategemewa kwa zaidi ya asilimia 80 kiikolojia na uhai wa wanyama kama vile viboko na Mamba ambao maisha yao yote hutegemea maji ya mto huo. Baada ya kusikiliza maombi hayo mhe. Majaliwa alisema,  "Niwashukuru Makamanda wa TANAPA kwa kufanya maboresho katika eneo la mto...

BODI YA MAJI KIJIJI CHA SINGA YATAKIWA KUVUNJWA.

Image
Na Ashrack Miraji,DmNewsOnline  KILIMANJARO KUKOSEKANA Kwa huduma ya Maji safi na salama Kwa wananchi zaidi ya 400 wa Kijiji cha Singa Wilayani Moshi mkoa wa Kilimanjaro wameitaka bodi ya Maji Kijijini hapo kuvunjwa kutokana na adha kubwa ya Maji wanayoipata wananchi. Changamoto ya Maji katika Kijiji cha Singa imekuwa kubwa nakusababisha wananchi kuhangaika Kwa ajili ya kutafuta huduma hiyo huku mabomba ya Maji ambayo yaliyopo yakiwa hayatoi Maji. Wananchi wa Kijiji hicho Kwa nyakati tofauti wamesema  licha ya kuchangia Sh162,000 kwa ajili ya kuunganishiwa  huduma ya maji mwaka 2018 lakini  hawajawahi kufaidi  huduma hiyo na kwamba wanalazimika kunywa maji  ambayo sio salama kwa matumizi ya binadamu . Mdau wa maendeleo Kijijini hapo  Joseph Mushi Amesema kutokana na changamoto hiyo imefikia atua  ya kuwasaidia wananchi hao kuwalipia gharama za Maji kwa Mwaka mzima nakwamba  amechukua hatua hiyo baada ya kuona wananchi wa kijiji hicho  wa...

WANANCHI KIJIJI CHA SINGA -KIBOSHO MOSHI WALIA CHANGAMOTO YA MAJI SAFI

Image
Na Ashrack Miraji,DmNewsOnline  SAME KILIMANJARO  WANANCHI wa Kijiji cha Singa Kata  ya kibosho Mashariki ,Wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro inadaiwa wanalazimika kunywa Maji machafu yanayotoka mto Karanga hali ambayo inatishia usalama wa Afya zao. Wamesema wanakunywa maji hayo kutokana na mgao mkubwa wa maji uliopo katika kijiji hicho  kwani Kwa  mwezi wanapata mgao wa maji mara moja au kukosa kabisa.  Wakizungunza na Mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki wamesema  kuwa licha ya kila mwananchi kuunganishiwa maji kwa gharama ya Sh162,000 mwaka 2018 changamoto ya maji imeendelea kuwepo katika kitongoji hicho hali ambayo imekuwa ikisababisha kero kwa wananchi hao  Akizungumza kwaniaba ya wananchi wake Mwenyekiti wa kijiji hicho, Aloyce Chuwa, alisema awali wananchi wa kijiji hicho walikuwa na mradi wao wenyewe wa maji na kwamba baadaye maji yale yalitawanywa maeneo ya vijiji vingine, hali ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa wananchi hao kukosa...

MAMA KOKA AGAWA DOTI ZA VITENGE KUELEKEA SIKU YA MWANAMKE DUNIANI

Image
Na Victory Masangu,DmNewsOnline  KIBAHA  MKE wa Mbunge wa  Jimbo la Kibaha Mjini Selina Koka  amegawa doti za  sare 125 za vitenge  kwa ajili ya sherehe za maadhimisho ya siku ya  Mwanamke Duniani zilizogharimu kiasi cha shilingi milioni 2. Sare hizo ambazo zimegawiwa katikka makundi mbali mbali ikiwemo Jumuiya ya wazazi, Wajumbe wa Baraza la UWT Kibaha Mjini, Wajumbe Wanawake wa Baraza la Wazazi la Wilaya, Wajumbe wanawake wa Baraza la UVCCM Kibaha Mjini Pamoja na Wajumbe Wanawake wa Halmashauri kuu ya CCM Wilaya Kibaha Mjini.  Akikabidhi sare hizo kwa niaba ya Mama Selina Koka Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mji Method Mselewa  amesema huu ni Utaratibu wa Ofisi ya Mbunge kupitia kwa Mama Koka kugawa sare kwa wanawake kila mwaka na kila zinapofika Sherehe hizo pamoja na Makongamano mbalimbali.  Kwa Upande wake Mama Selina Koka akizungumza katika mahojiano maalumu kwa njia ya simu alisema kwamba ameamua kutoa sare hizo kwa lengo la k...