COMPASSION YAFADHILI WATOTO ZAIDI YA 115000 KUPATA ELIMU NA KUWAKOMBOA NA UMASIKINI
Na Benny Kingson,DmNewsOnline TABORA. ZAIDI ya watoto 115,000 wamefadhiliwa na shirika la maendeleo ya huduma ya mtoto na kijana nchini COMPASSION (CIT)kupata elimu ya dini,jamii na kukombolewa kiuchumi ambao wametoka katika familia zenye hali duni ya maisha. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa nishati Dkt.Dotto Biteko akiwakilishwa na Naibu Waziri wa afya Dkt.Godwin Mollel katika kilele cha maadhimisho ya miaka 25 ya COMPASSION kitafa Mkoani Tabora yaliyofanyika kwenye uwanja wa chipukizi mjini humo alihimiza wazazi,walezi na jamii kujitolea kuwasaidia watoto na vijana kupata malezi bora badala ya kuchangia fedha nyingi za harusi na misiba. Biteko alisema kuwa shirika hilo limefankisha kujenga vituo vingi vya kujifunzia watoto na vijana na kuwapatia ujuzi wenye kupatia vipato vya halali na kujihakikishia maendeleo yao na ya familia zao pamoja na ya taifa ambapo wamewezesha kuokoa fedha zilizokuwa zitumiwe na serikali kuvijenga na s...