Posts

KOKA AWASHUKURU VIONGOZI NA WANACHAMA WA CCM KWA USHIRIKIANO

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline KIBAHA MBUNGE  wa Jimbo  Kibaha mjini Silvestry Koka kwa dhati wanachama wa ccm pamoja na wananchi wa Kata ya Pangani kwa kuweza kumchagua Yohana Gunze kuwa  diwani wa Kata ya Msangani katika uchaguzi mdogo uliomalizika hivi karibuni. Koka ameyasema hayo machi 26 ,2024 wakati wa kikao màalunu  cha Halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mji chenye lengo la kujadili agenda mbali mbali kimaendeleo  pamoja na kujiandaa na chaguzi mbali mbali ikiwemo uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Amesema Koka aliwapongeza viongozi mbali mbali kuanzia ngazi zote za chini hadi ngazi za juu kwa ushirikiano wao wa  dhati katika kipindi chote cha kampeni za uchaguzi wa udiwani hadi uchaguzi mwenyewe.  Koka amesema kwamba amefarijika sana kuona wanachama na wananchi kukiamini chama cha mapinduzi na kumchagua kwa kishindo  mgombea udiwani wa kata ya Msangani kwa kushinda kwa kishindo kwa asilimia 99.20 "N...

DC SHAKA AWASHA MOTO UJENZI WA ICU KILOSA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline MOROGORO MKUU wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro, Shaka Hamdu Shaka, ameagiza kufanyika kwa  uchunguzi wa   mradi wa ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Wilaya hiyo lililogharimu Sh. milioni 278 ambalo ujenzi wake umeonekana kuwa chini ya viwango kabla ya kuanza kutumika.  Akizungumza na watumishi na viongozi wa Hospital hiyo mara baada kutembelea na kukagua jengo hilo kwa mara ya pili mwishoni mwa wiki, Shaka alisema ameshangazwa kukuta mradi huo umejengwa chini ya viwango ukiwa na mapungufu mengi  na kuagiza marekebisho yafanyike mpaka sasa wameshindwa kukamilisha kwa wakati bila sababu za msingi. “Fedha zimeletwa zaidi ya Sh. milioni 200 katika mradi huu lakini cha kusikitisha viongozi mmeshimdwa kujitambua, umakini na kusimamia jukumu hili, pamoja na yote mnaniambia hata mjenzi wa awali mliyempa kazi na kuharibu hamumjui mtampata wapi, mambo ya ajabu sana, haiwezekani kabisa ndio maana ninataka vyomb...

BALOZI DKT. NCHIMBI - USHAURI WA VIONGOZI WASTAAFU UTAENDELEA KUENZIWA.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline ZANZIBAR                KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt .Emmanuel John Nchimbi, amesema ushauri na maelekezo ya Viongozi Wastaafu wa Chama na Serikali, pamoja na Wazee wa CCM kuhusu umuhimu wa kuendelea kukiimarisha Chama, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwatumikia watu vizuri, yatafanyiwa kazi kwa uzito unaostahili. Katibu Mkuu Balozi Dkt. Nchimbi amesema hayo Jumapili, Machi 24, 2024, wakati wa mazungumzo na viongozi wastaafu wa Chama na Serikali, wakiwemo Marais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Wenyeviti wa Baraza la Mapinduzi (wastaafu), Dk. Salmin Amour Juma na Dkt. Ali Mohamed Shein, nyakati tofauti katika makazi yao, pamoja na Wazee wa CCM kwenye mikutano yao ya mabaraza, Pemba na Zanzibar. “Asanteni. Waambie pia nawasalimia. Simamieni Chama…chama kijengwe, kisimamiwe kupata ushindi mzuri,” amesema Dkt. Salmin Amour, baada ya kufikishiwa salaam za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya ...

DOLA ZA MAREKANI BILIONI 1.31 MAPATO KUTOKA SEKTA YA UTALII NDANI YA MIAKA MITATU

Image
“Katika kipindi cha miaka mitatu idadi ya Watalii Nchini imeongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 walioipatia Nchi mapato dola za Marekani bilioni 1.31 hadi Watalii 1,808,205 mwaka 2023 walioingiza dola bilioni 3.37” - Mobhare Matinyi, Msemaji Mkuu wa Serikali   

DKT. NCHIMBI AKOSHWA NA MISIMAMO THABITI YA WANA-CCM PEMBA

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline PEMBA ,ZANZIBAR KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amesema anawaheshimu na kuwakubali wana-CCM wa Pemba kwa misimamo yao thabiti katika kuilinda na kuitetea CCM, bila kuyumba.  Dkt. Nchimbi pia amewapongeza kwa jinsi ambavyo wameendelea kuwa imara kuifanya Pemba kuwa moja ya ngome za Chama Cha Mapinduzi nchini, akiwasisitiza wanaCCM kuendelea kuwa wamoja, chini ya Uongozi wa Mwenyekiti wa CCM, ambaye pia ni Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.  Katibu Mkuu wa CCM Balozi Dkt Nchimbi amesema hayo leo Machi 23, 2024, alipokuwa akizungumza na baadhi ya viongozi na wanachama wa CCM wa Pemba, waliofika kumlaki katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume, Pemba, mara tu baada ya kuwasili uwanjani hapo, tayari kuanza ziara ya kikazi ya siku moja, katika Kisiwa cha Pemba.  “Kati ya wanaCCM ninaowaheshimu na kuwakubali sana kwa jinsi wanavyoipenda CCM, wanavyoilinda, kuitetea na kuisemea ni wanaCCM wa Pemba....

RAIS SAMIA ATOA LESENI 37 ZA UCHIMBAJI MADINI KWA WACHIMBAJI WADOGO SONGWE

Image
  Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline SONGWE Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan  imetekeleza ombi la siku nyingi la Wachimbaji Wadogo Wilayani Songwe kwa kuwatengea eneo la uchimbaji na kuwakabidhi jumla ya Leseni ndogo 37 zilizopo eneo la Kata ya Saza kutoka Leseni hodhi namba RL0009/2014  iliyokuwa ya Kampuni ya Bafex Tanzania Limited. Hayo yamesemwa  leo  Machi 23, 2024 na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde alipofika eneo la Saza Wilayani Songwe kukabidhi leseni 19 kwa wachimbaji wadogo wa Kikundi cha Songwe Gold Family (*SGF*) na wachimbaji wengine wadogo wadogo 18 huku mchakato wa kuendelea kutoa Leseni zaidi ukiendelea. "Nimefika hapa leo kwa maelekezo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amenielekeza nije kuwakabidhi leseni zenu za wachimbaji wadogo mlizomuomba na  kuwa mnakwenda kuwekeza mitaji mikubwa sasa na kuongeza mzunguko wa fedha zitokanazo na shughuli za madini kufikia zaidi ya Trilioni moja," amesema Mavunde. Waziri Mavunde amesema pamoja na kwamba...

AMUUA MKEWE NA KUMZIKA NDANI YA CHUMBA,KILOSA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline JESHI la Polisi mkoani Morogoro  linamshikilia mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la  Mohamedi Omari  mkazi wa kijiji cha Kimamba A wilayani  Kilosa  kwa tuhuma za  kumuua mkewe  na kumzika ndani ya chumba chao. Mohamedi Omari mkazi wa kijiji cha Kimamba A  wilayani Kilosa mkoani Morogoro kamuua mkewe na kisha kumzika ndani ya chumba wanacho lala ambapo tukio hilo  limeonekana kushangaza wengi. Ni tukio la kuhuzunisha  tukio ambalo kabla ya kifo chake inadaiwa kuwa alipata  kipigo kikali  kutoka kwa mumewe huyo  mama alilia kwa uchungu akimsisitiza  kutunza watoto wake ambao hakuzaa nae. Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Shaka Hamdu Shaka amesema kuwa baada ya kufanya mahojiano na watoto wa mama huyo aliyetambulika kwa jina la Beatrice Haiyasi wameeleza jinsi walivyopitia unyanyasaji mpaka kupelekea kukosa huduma muhimu za kielimu kutokana na kufungiwa ndani. Pia ameeleza ku...