MBUNGE LUTEVELE :MARUFUKU WALIMU KUFANYA BIASHARA ZA KACHORI DARASANI
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline
IRINGA _MAFINGA
Mbunge wa Jimbo la Mafinga Dickson Lutevele (Villa), amepiga marufuku walimu kujihusisha na biashara ndogondogo darasani na kulazimisha wanafunzi kununua bidhaa hizo
Hatua hiyo imekuja kufuatia malalamiko ya baadhi ya wazazi wa mtaa wa Lutalawe kata ya Changarawe, waliodai kuwa baadhi ya walimu wamekuwa wakiendesha biashara ndani ya maeneo ya shule hali inayosababisha kero kwa wazazi ya kutoa fedha kwa Watoto kila siku.
Walimetaka mbunge kuingilia kati suala hilo ili kupunguza mzigo wa kifedha kwa familia kwani wanalazimika kutoa fedha kiasi cha shilingi 200 hadi 500 kila siku ili mtoto akanunue kachori kwa mwalimu,
Akijibu malalamiko hayo, mh. Lutevele alitoa agizo kwa maafisa elimu na watendaji kuhakikisha wanakomesha mara moja vitendo hivyo nakueleza kuwa serikali tayari imepiga marufuku michango holela mashuleni, hivyo walimu wanaolazimisha wanafunzi kununua bidhaa zao wanafanya kitendo kinachofanana na mchango usio halali.
Afisa elimu wa kata ya Changarawe Shaban Nyigo ameahidi kulifanyia kazi suala hilo mara moja huku akibainisha kuwa walimu hawaruhusiwi kufanya biashara shuleni na yeyote atakayebainika atachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu za kazi.
Mbunge Dickson Lutevele amehitimisha ziara ya siku tatu jimboni kwake, ambapo alipata fursa ya kusikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi kwa kushirikiana na wataalamu kutoka katika halmashauri yam ji Mafinga na wilaya ya Mufindi.






Comments
Post a Comment