JAMII YATAKIWA KUSHIRIKIANA NA POLISI KUFICHUA UHALIFU.

  Na Eliasa  Ally,DmNewsonline

                    IRINGA

   KAMANDA  wa Polisi Mkoa wa Iringa, SACP Allan Bukumbi, ameitaka jamii kuacha tabia ya kuficha wahalifu na badala yake kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa mapema ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza.

Kamanda Bukumbi ametoa wito huo Februari 27, 2026  akisisitiza kuwa ushirikiano wa wananchi ni nguzo muhimu katika kupambana na vitendo vya uhalifu na kudumisha usalama wa jamii.

Aidha, Kamanda Bukumbi anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara kesho Februari 28, katika uwanja wa Shule ya Msingi Mawelewele, Kata ya Mwangata. 

Lengo la mkutano huo ni kutoa elimu kwa wananchi kuhusu mapambano dhidi ya uhalifu pamoja na kusikiliza changamoto zao ili kuimarisha usalama na ulinzi wa raia na mali zao.

Jamii inahimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki mkutano huo muhimu. 

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.