SERIKALI IMEFANYA MAGEUZI MAKUBWA KWA VIJANA KATIKA UONGOZI WA RAIS SAMIA
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
Dar es Salaam
MRATIBU wa Taasisi ya Together for Samia Gulatone Masiga amesema kwamba katika kipindi cha miaka mitano ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan serikali imefanya mageuzi makubwa ya kuwanufaisha vijana wa Kitanzania katika sekta za ajira,ujuzi na elimu pamojana uwezeshaji wa kiuchumi.
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Januari 26,2026 Jijini Dar es Salaam wakati wa kumbukizi ya maadhimisho ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais Samia yaliyoandaliwa na taasisi ya Together for Samia,amesema Rais ametoa fursa nyingi kwa vijana zenye mafanikio.
Aidha amesema kwamba Rais Samia amewekeza kwa vijana katika kizazi cha Sasa na kijacho hasa katika ujenzi wa vyuo vya ufundi na ujuzi katika wilaya zaidi 62 nchini jambo lilopelekea vijana kupata fursa ya kujiajiiri na kushinda katika soko la ajira.
Aliendelea kwamba Rais Samia amewekeza kwa vitendo,kwani vyuo ni chachu ya kuwaapatia vijana ujuzi unaohitajika katika maisha ya Sasa na baadae.
"Rais Samia amefanya mageuzi makubwa katika sekta ya elimu kwa kuja na mtaala mpya unaaolenga kuhakikisha wanafunzi wanaomaliza elimu ya msingi na sekondari wanakuwa na maarifa na stadi zitakazowawezesha kujiajiri na kujikwamua kiuchumi
Aliongeza kwamba Rais amewekeza katika sekta ya Nishati safi hatua inayochochea maendeleleo ya viwanda na biashara kwa kuwainua vijana waweze kujiajiiri na kujikwamua kiuchumi.
Kwa upande wa Mwanzilishi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Vijana Innovations,Dorcas Mshiu amesema ameungana na Watanzania kuadhimisha siku ya kumbikizi ya kuzaliwa Rais Samia kwa kutambua mchango wake wa kufungua fursa kwa vijana.
Mshiu amesema kupitia Wizara ya Viwanda na biashara vijana wengi wamesajili biashara zao kutokana na mazingira kuwa rafiki nchini na mipaka ya uwekezaji ndani na nje imekuwa rafiki kiuwekezaji.
Mkurugenzi Dorcas amesema Rais ameweka mpango mkakati maalum wa mikopo yenye riba ya asilimia 4 kwa vijana na umekuwa msaada mkubwa kwa vijana
Naye Mshiriki Nathaniel Samson amewaomba watanzania kumuombea Rais Samia kwani akiahidi jambo lolote lile yeye anatekeleza kwa vitendo 





Comments
Post a Comment