PROFESA LIPUMBA, AWATAKA WATANZANIA KUTOGAWANYIKA.
Timothy Marko,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM.
MWENYEKITI wa Chama Cha Civil United Front (CUF) Professa Ibrahim Lipumba amewataka Watanzania kutorubuniwa kwa Migawanyiko inayochochewa na Baadhi ya Wanasiasa,Nakusisitiza kuwa Taifa la Tanzania litajengwa kwa Misingi ya Amani na Umoja nasio Misingi ya Migawanyiko.
Akizungumza Katika Maadhimisho ya kumbukukizi ya Machafuko yaliyotokea 27 January 2001 Zanzibar Ambapo zaidi wafuasi 71 wachama hicho waliopoteza Maisha, Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuwa nivyema kukapatikana Mfumo mzuri wa Uchaguzi unaozingatia haki na Umoja wa kitaifa.
"SsiI ni Chama tunachosimamia misingi ya Umoja wa kitaifa,tusikubali kugawanyika kwa misingi ya uzanzibari na Utanganyika" Amesema Mwenyekiti wa Chama Cha CUF Professa Ibrahim Lipumba.
Professa Lipumba Ameongeza kuwa nivyema kutatua Matatizo yetu kwa Misingi ya Amani.
"Watu wapate kura nyingi kwa misingi ya Uhuru na haki" Amesisitiza Professa Ibrahim Lipumba.






Comments
Post a Comment