MWENYEKITI TUME HURU YA UCHAGUZI AWATAKA WARATIBU NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI KUZINGATIA SHERIA.
Na Eliasa Ally,DmNewsonline
IRINGA
MWENYEKITI wa Tume huru ya taifa ya uchaguzi Jaji Jacob Mwambegele amewakumbusha wasimamizi na waratibu wa uchaguzi kuzingatia weredi Sheria na kanuni za uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha sita ibara ya kwanza na utendaji kazi kwa kuzingatia uzoefu wao bila kupendelea
Jaji Mwambegele ameyabainisha hayo wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi ngazi ya mkoa Jimbo na kata yanayofanyika mkoani Iringa kwa siku tatu katika ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Iringa
Mafunzo hayo yanahusisha waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo na kata maafisa uchaguzi,maafisa ununuzi na uhasibu kwa lengo la kukumbushana masuala muhimu kuhusu usimamizi uratibu na uendeshaji mdogo wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na udiwani katika kata ya shiwinga.
Pia amewasisitiza kuheshimu viapo vyao kwa nafasi walizoteuliwa kutekeleza majukumu yao Kwa kuzingatia katiba ya nchi ,sheria za uchaguzi na kanuni zake kanuni za maadili ya uchaguzi pamoja na maelekezo yanayotolewa na tume katika kipindi cha uchaguzi.
Mbali na hayo Mh.Mwambegele amewataka wasimamizi na maafisa hao ambao wanauzoefu katika uendeshaji wa uchaguzi kuhakikisha wanazingatia maelekezo waliyopewa na tume badala yakufanya kazi kwa mazoea.
Pia amewasihi wasimamizi hao kufanya utambuzi wa vituo vya kupigia kura mapema ili kubaini mahitaji ya vituo husika na kuhakikisha kila mkuu wa kituo anapata vifaa vyote vya uchaguzi vinavyohitajika mapema
Akizungumza mratibu wa uchaguzi kutoka Ruvuma Salumu katenda amewataka wasimamizi kusimamia viapo kwa mujibu wa kanuni na amewataka wananchi kushiriki kampeni za uchaguzi kwa vyama vyote kwa usawa ili waweze kusikiliza sera za wagombea na kuwapa nafasi ya kuchagua kiongozi aliye bora
Msimamizi wa uchaguzi kutoka Mbozi Dani mteve amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katikanuchaguzi 




Comments
Post a Comment