DIWANI MALILO ATOA MSAADA KWA WATOTO WASIOJIWEZA SHULE YA MSINGI BONYOKWA
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline
Dar es Salaam
DIWANI wa Kata ya Bonyokwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhe.Tumike Malilo ametoa msaada wa sare za shule ,kalamu na daftari kwa watoto wasiojiweza katika shule ya msingi Bonyokwa
Akizungumza na waandishi wa habari Leo Januari 29,2026 mara baada ya kukabidhi msaada huo amesema kwamba ameamua kutoa msaada kwa watoto hao kuonyesha upendo na kujitoa kwa ajili ya jamii inayomzunguka katika Kata hiyo.
"Nimeona ni vema kuwasaidia watoto wasiojiweza kwa kuwapatia msaada wa sare za shule ili nao watambue kuwa tunawapenda na kuwathamini",amesema Mh.Tumike
Aidha,amesema tunaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Afya,elimu na miundombinu ya Barabara.
Sekta ya Elimu
Akizungumzia sekta ya elimu Diwani huyo amesema kwamba katika Kata ya Bonyokwa Ina shule Mbili za msingi ambazo ni Shule ya Msingi Kifuru na Bonyokwa ,Hali ya shule ya msingi Bonyokwa tumeongeza madarasa sita,matundu 15 ya vyoo na changamoto iliyopo kwa sasa shule inahitaji uzio pamoja na madawati.
Watoto waliojiunga na darasa la kwanza shule ya msingi Bonyokwa ni 212 ambapo kifuru ni 250 kwa matokeo ya wanafunzi wa darasa la nne wamefanya vizuri katika mitihani yao.
Kata ya Bonyokwa ipo shule Moja ya Sekondari na High School ambayo ujezi wake unaendelea na ujenzi wake umefikia asilimia 95 na Ina madarasa 53,Ina maabara zote tatu za fizikia,biolojia na kemia na imejitosheleza Kwa Kila kitu.
Akizungumzia sekta ya Afya Mhe.Diwani Tumike amesema ipo Zahanati katika Mtaa wa Kisiwani na Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kujenga jengo la kupumzikia wagojwa,wajawazito na kupimia watoto.
"Tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kutuwezesha katika kata yetu na kwa mwaka wa fedha 2025/26 tayari zimeshatengwa milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya.
Pia amesema kwamba kata ya Bonyokwa imeendelea kuimarisha ulinzi shirikishi na mpaka sasa ujenzi wa kituo cha Polisi cha kata umefikia asilimia 75 ujenzi unaendelea vizuri uko katika hatua za mwisho kukamilika
Hali ya miundombinu ya Barabara katika Kata ya Bonyokwa kulikuwa hamna barabara zenye kiwango cha lami lakini tunamshukuru Rais Samia na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa Tarura hasa kwa mtaa wa Msingwa kulikuwa na changamoto ya daraja lakini kwa sasa daraja limejengwa kwa kiwango cha zege lakini pia mkandarasi anaendelea na ujenzi wa Barabara ya Segerea Bonyokwa kwa mita mia saba anaendelea na ujenzi kwa kiwango cha lami na taa za barabarani. 




Comments
Post a Comment