MSAMA: TUWAPUUZE WANAOLIPWA KUVURUGA AMANI YETU
Na Mwandishi Wetu,DmNewsonline
DAR ES SALAAM
MKURUGENZI wa Msama Promotions na Mfanyabiashara malufu nchi Tanzania Alex Msama amewataka Watanzania kuwapuuza watu ambao wanalipwa ili kuvuruga amani ya nchi yetu ya Tanzania.
Amesema maranyingi watu wanaofanya hivyo sio Watanzania na baadhi yao ni Watanzania wanaoishi nje ya nchi kama vile nchi jirani na Tanzania pamoja na mataifa mengine ya nje.
"Watanzania wenzangu, nawasihi kwa moyo mmoja tuwapuuze watu wanaotaka kuvuruga amani yetu, maana watu hawa wanalipwa Mamilioni ili kuvuruga amani yetu tuliyo nayo."amesema
" Miongoni mwa watu hawa hawaishi hata hapa nchini bali wanaishi nje ya nchi na wengi sio Watanzania na wanalipwa na baadhi ya Watanzania na watu wengine wa nje ya nchi ili wavuruge amani yetu iliyoasisiwa na wazee wetu."amesisitiza
Nakuongeza kuwa, watu wanaofanya hivi furaha yao nikuona amani yetu inavurugika ili watuibie rasilimali zetu, pia furaha yao ni kuona tunagombana, tunauana na kuchukiana, tuwapuuze" 








Comments
Post a Comment