MACHUMU, ANG'ATUKA TEF, MGONGANO WA MASLAHI WA WADHIFA NDIO CHANZO.

Na Mwandishi wetu,DmNewsonline

                 DAR ES SALAAM


MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejijuzulu nafasi ya makamu mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kwa kile alichodai kwa nafasi yake mpya anaona kutakuwa na mgongano wa masilahi na wadhifa huo.

Machumu ambaye hivi karibuni ameteuliwa na Rais Dtk.Samia Suluhu Hassan kuwa mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu amekabidhi barua ya kujiuzulu kwake kwa Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, leo  Novemba 26, 2025 alipokutana na wahariri kwenye kikao cha ndani, Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa TEF Deodatus  Balile amepokea baruahi hiyo na kukubali kujiuzulu kwa Machumu na kuwa Kamati ya Utendaji ya TEF itakutana baadaye leo kujadili suala hilo.


Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.