MGOMBEA URAIS KUNJE NA MGOMBEA MWEZA WAKE AAFP KUZINDUA KAMPENI KIHOMBOHOMBO MOROGORO AGOSTI 31

Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline

         DAR ES SALAAM 


CHAMA cha Wakulima(AAFP) kinapenda kuwataarifu wananchi na wanachama wake,vyombo vya habari kuwa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 zitafanyika  Kihombohombo Vijijini Mkoa wa Morogoro Agosti 31,,2025 kuanzia saa nne  asubuhi hadi saa 12:00 Jioni

Katika uzinduzi huo,Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kunje Ng'ombale Mwiru  pamoja na mgombea Mwenza Chumu Abdallah Juma wanatarajiwa kuhutubia wananchi na kueleza kwa kina sera na vipaumbele vya Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha AAFP kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu.

Aidhaa ,viongozi wakuu wa chama,wagombea ubunge ,na wagombea wa udiwani kutoka mikoa mbalimbali nchini watashiriki katika tukio hilo kubwa la kihistoria na la kisiasa pamoja na wasanii mbalimbali wa bongo fleva watakupo

Wakazi wote wa Mkoa wa Morogoro na mikoa ya Jirani  mnakaribishwa kuhudhuria kwa wingi katika uzinduzi huo wa kampeni ili kupata nafasi na fursa ya kusikiliza sera zinazolenga kuleta maendeleo ya nchi na kwa ustawi wa Mtanzania

Taarifa hii imetolewa kwa njia ya simu Leo Agosti 30,2025 na Naibu Mkuu wa AAFP  Mark Isdory Mhemela  akiwa sehemu ya tukio pia amewatakia Kila la heri wagombea wote wa AAFP nchi kushiriki  kampeni za amani na utulivu.

Sanjari na hayo ,amesema katika kampeni hizo wapo wanachama wapya watakaojiunga na Chama hicho .

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.