HALMASHAURI YA MJI KIBAHA IMEVUNJA RASMI BARAZA LA MADIWANI JUNI 17,2025.

Na Mwandishi wetu,DmNewsonline KIBAHA HALMASHAURI ya Mji kibaha limevunja Baraza Rasmi leo,Juni 17,2025 na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa Wazazi wa Wilaya kibaha , Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mh, Nickson Saimon Pamoja na Wakuu wa Idara wa Halmashauri. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Musa Ndomba akizungumza katika kikao hicho amesema kuwa Kibaha Mjini imepata mafanikio makubwa yaliyopelekea Kibaha kuwa na Maendeleo. Ndomba ,amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano tangu 2020 hadi 2025 Kibaha Mjini cha madiwani hao wamefanikiwa kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani kutoka Sh.bilioni 3.8 ya Mwaka 2020 mpaka kufikia bilioni 14 ya Mwaka 2024. Ameongeza kuwa,katika kipindi cha mwaka 2024 /2025 mapato hayo yameongezeka zaidi ambapo mpaka sasa tayari wamekusanya kiasi cha Sh.bilioni 20 sawa na asilimia 200. Aidha,Ndomba amesema kuwa kupitia mapato hayo Halmashauri kupitia Baraza la Madiwani wamefan...