Posts

Showing posts from June, 2025

HALMASHAURI YA MJI KIBAHA IMEVUNJA RASMI BARAZA LA MADIWANI JUNI 17,2025.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline               KIBAHA HALMASHAURI  ya Mji kibaha limevunja Baraza Rasmi leo,Juni 17,2025 na kushuhudiwa  na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu wa Wazazi wa Wilaya kibaha , Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Mh, Nickson Saimon Pamoja na Wakuu wa Idara wa Halmashauri. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Musa Ndomba akizungumza katika kikao hicho amesema kuwa Kibaha Mjini imepata mafanikio makubwa yaliyopelekea Kibaha kuwa na Maendeleo. Ndomba ,amesema kuwa katika kipindi cha miaka mitano tangu 2020 hadi 2025 Kibaha Mjini cha madiwani hao wamefanikiwa kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani  kutoka Sh.bilioni 3.8 ya Mwaka 2020 mpaka kufikia bilioni 14 ya Mwaka 2024. Ameongeza kuwa,katika kipindi cha mwaka 2024 /2025 mapato hayo yameongezeka zaidi ambapo mpaka sasa tayari wamekusanya kiasi cha Sh.bilioni 20 sawa na asilimia 200. Aidha,Ndomba amesema kuwa kupitia mapato hayo Halmashauri kupitia Baraza la Madiwani wamefan...

WATAALAMU MANISPAA TABORA WAPONGEZWA

Image
Na Allan Kitwe, DmNewsonline            TABORA  WATAALAMU wa Halmashauri ya Manispaa Tabora wamepongezwa kwa usimamizi mzuri wa fedha za miradi ya maendeleo na kuandaa vizuri na kwa usahihi taarifa za matumizi ya fedha zote zilizopokelewa na za mapato ya ndani. Pongezi hizo zimetolewa jana na Mkuu wa Wilaya ya Igunga Sauda Mtondoo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Paul Chacha kwenye kikao cha mwisho cha baraza la madiwani wa manispaa hiyo. Amesema kuwa usimamizi mzuri wa fedha za maendeleo umepelekea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kuipa halmashauri hiyo hati safi (unqualified opinion). ‘Nawapongeza sana Mstahiki Meya, Naibu Meya, Madiwani, Mkurugenzi Mtendaji na Wataalamu wote wa halmashauri ya manispaa kwa kufanya kazi kwa ushirikiano mkubwa na usimamizi thabiti wa fedha za maendeleo’, amesema. Mtondoo amefafanua kuwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta mbalimbali ndani ya manispaa hi...

DKT. YONAZI AMEONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA TAIFA YA USHAURI YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA MWAKA 2022

Image
NA MWANDISHI WETU ,DMNEWSONLINE                 DAR ES SALAAM  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi (mwenyekiti wa kikao) cha Kamati ya Taifa ya Ushauri ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kilichofanyika tarehe 17 Juni, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere JIjini Dar es Salaam.   Kikao hicho kimeudhuriwa na Matibu Wakuu wa Wizara za Kisekta, Makamisaa wa Sensa pamoja na baadhi ya wakuu wa Taasisi.Lengo la kikao hicho ni kupokea na kujadili ripoti mbalimbali za utekelezaji wa Awamu ya Tatu na ya Mwisho ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022.   Aidha miongoni mwa ripoti hizo ni pamoja na ile ya Utekelezaji wa Mwongozo wa Kitaifa wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 kwa kipindi cha kuanzia Desemba 2024 hadi Mei 2025, na Hali ya Utekelezaji wa Anwani za Makazi.   Pia kikao kimejadili na kupokea Rasimu za Ripoti Tano za kina za Matokeo ya ...

MJUMBE KAMATI YA UTEKELEZAJI YA UMOJA WA WANAWAKE TAIFA (UWT) FATMA REMBO AWAPA WAZAZI/WALEZI SOMO

Image
    Na Eliasa Ally DmNewsoline IRINGA  WAZAZI na Walezi wametakiwa kuangalia matendo ambayo yako kinyume na utamaduni wa Kitanzania kwa kuwa ni moja ya vyanzo vikubwa ya makuzi ya watoto nchini. Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Fatma Rembo Organization' ya mjini Iringa, ambaye pia Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Wanawake Taifa (UWT) na mjumbe wa baraza Kuu UWT  mkoa wa Iringa, Fatma Rembo wakati akizungumza siku ya maadhimisho ya Mtoto wa Afrika Watoto iliyofanyika katika viwanja vya Mwembetogwa. Rembo alisema kuwa watoto wamekuwa wepesi kuiga matendo ya wazazi na walezi yaliyo mazuri na mabaya hivyo ni wakati ambao wanahitaji sana kuwa makini katika malezi ili kupata kizazi ambacho kina maadilli ya Kitanzania. Alisema kuwa kuna baadhi ya wazazi walezi wanashindwa kuzingatia maadili ya kitanzania katika mambo mbalimbali kama mavazi yasiyo na stara, unywaji wa pombe hivyo kufanya watoto kuiga yale wanayoona kuliko kusikia. Aliongeza kuwa maisha ya sasa yam...

DKT. DELILAH KIMAMBO BOSS MPYA MUHIMBILI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali., Katika uteuzi huo Dkt. Samia amemteuwa Dkt. Delilah Kimambo kuwa  Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, akichukua nafasi ya Prof. Mohamed Janabi aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani ( WHO ) Kanda ya Afrika.

ASASI YA KIRAIA YAAZIMISHA SIKU YA MAZINGIRA KWA KUFANYA USAFI FUKWE YA BAHARI YA HINDI

Image
  Na Mwandishi wetu DmNewsonline          DAR ES SALAAM  KATIBU wa Asasi ya kiraia ya Sustainable alliance Tanzania Paul Matonya amesema , Asasi hiyo ya kiraia inayoongozwa na vijana waliomaliza Vyuo vikuu hapa Nchini shughuli zake kubwa ni kuwezesha vijana na kuhusisha kwenye mambo mazima ya kupambana na Kuhamasisha  kuleta afya Bora ya bahari . Amesema yeye kama kiongozi na Mwanasayansi kwa upande wa  bahari na katika kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani amewaongoza vijana wezake  kufanya usafi wa Mazingira katika eneo la fukwe ya bahari ya hindi jijini Dar es salaam. Akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la fukwe bahari Salenda mara baada ya kufanya usafi huo wa Mazingira ya bahari.Matonya amesema lengo la kufanya usafi sio kwa ajili ya kusafisha bahari pekee lakini pia wanajulisha ulimwengu au umma nini ambacho kinakuwa kinatokea kwenye fukwe ya bahari. "Siku hii ya leo tunaitumia kufanya usafi na kukusanya taka zote zikiwe...

CCM YAWAONYA WATIA NIA WANAOTUMIA LUGHA ZA KASHFA.

Image
   Na Eliasa Ally DmnewsOline IRINGA  CHAMA cha Mapinduzi  mkoa wa Iringa kimetoa onyo kwa baadhi ya watia nia nafasi ya udiwani na ubunge Mkoani hapo ambao wamekuwa wakitumia lugha ya zihaka na kashfa kwa washindani wao ili kujenga ushawishi wa kuchaguliwa katika uchaguzi Mkuu ujao wa Octoba 2025. Rai hiyo imetolewa leo hii Juni 16, 2025 na mjumbe wa kamati kuu ya CCM Taifa MCC Salim Abri Asas wakati akizingumza na wanahabari katika ofisi za chama hicho. MCC  amesema wapo baadhi ya watia Nia wa uongozi wanaita vyombo vya habari na kuanza kumsemea, kumkashifu na kumdhihaki diwani au mbunge aliye madarakani kwa kuyaanika madhaifu yake ili kujijengea ushawishi na imani ya kwa wanaomchagua akifafanua kuwa kufanya hivyo hakuna Tija na kunachafua Chama hicho. Akifafanua zaidi hoja hiyo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Iringa Daud Yassin amewaonya hata wale wapambe wa viongozi hao wanaotoka lugha za zihaka akisema lugha hizo zitawaathiri viongozi wao wanaowan...

RC KUNENGE ARIDHISHWA NA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATO HALMASHAURI YA KIBAHA TC

Image
Na Victor Masangu,DmnewsOnline,                   KIBAHA   Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Alhaji Abubakari Kunenge amempongeza kwa dhati Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Kibaha mjini Dkt.Rogers Shemwelekwa kwa kuweza kuweka mikakati madhubuti katika  kubuni vyanzo  vipya vya ukusanyaji wa mapato ya ndani ambayo yameweza  kuleta mabadiliko  chanya katika utekelezaji wa miradi mbali mbali ya kimaendeleo. Kunenge ameyasema hayo wakati wa kikao maalumu cha baraza la madiwani katika Halmashauri ya Kibaha mji kwa ajili ya kuweza kujadili taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa kipindi cha kuanzia mwaka  wa 2023  hadi 2024 ambacho kimeweza kuhudhuliwa na viongozi mbali mbali wa serikali, wakuu wa idara, wataalamu  pamoja na viongozi  mbali mbali  wa chama. Amesema kwamba Halmashauri ya Kibaha mji imeweza kupiga hatua kubwa hadi kuweza kupandishwa hadhi ya kuwa Manispaa k...

RAIS SAMIA APELEKA NEEMA YA MAJI KASULU

Image
       Na Allan Kitwe, DmNewsonline                  KASULU SERIKALI ya awamu ya 6 inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imepeleka zaidi ya sh bil 40 katika Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maji safi na salama ili kumaliza kero ya wananchi. Katika maeneo mengi ya Wilaya hiyo ikiwemo Kasulu Mjini huduma ya maji safi na salama imekuwa hairidhishi hali iliyopelekea kuwepo malalamiko ya mara kwa mara juu ya ubora wa maji yanayopatikana. Akiongea na Mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake jana, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Kasulu Mjini (KUWSSA) Nuru William Bagowe ameipongeza serikali kwa kusikia kilio cha wananchi. Amesema kuwa katika kipindi cha miaka 5 tangu aingie madarakani, Rais Samia ameleta neema kubwa kwa wakazi wa Wilaya hiyo kwa kupeleka mabilioni ya fedha ambayo yamesaidia sana kutatua kero ya maji katika maeneo mengi. Amebainisha kuwa kwa mwaka...

TANZANIA NA KONGO ZAKUTANA KUJADILI USALAMA KUHUSU UHAMIAJI ‎ ‎

Image
Na Angelina Mganga, DmNewsonline  ‎              ‎DAR ES SALAAM  ‎ ‎JAMHURI ya Muungano wa Tanzania na  ‎Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC); kupitia Idara ya Uhamiaji wamekutana  Jiji Dar es Salaam  katika kikao kujadili  hali ya  ulinzi na usalama katika mashirikiano ya nchi hizo. ‎ ‎Akizungumza katika Mkutano huo uliofanyika Juni 16,2025 Jijini Dar es Salaam,Kamisgina Jenerali wa Uhamiaji nchini,(CGI) Dk.Anna Makakala amesema kwamba kikao hicho kinajadili masuala ya kuimarisha mahusiano na mashirikiano mazuri ya kiuhamiaji kwa kuwa Kongo ni majirani zetu tunapakana. ‎ ‎Dk.Makakala amesema mahusiano haya  yataimarisha ulinzi na usalama lakini pia masuala ya kiuchumi kwani uhamiaji ni suala muhimu sana katika kuleta maendeleo lakini pia kukuza usalama lazina Sheria ,taratibu na kanuni zote zifuatwe. ‎ ‎Aidha,Dk.Makakala ameendelea kwamba  tupo kwa ajili ya kubadilishana ,kushirikiana na jinsi ya kuweza k...

MWENYEKITI WA BODI TPLB ABWAGA MANYANGA , KARIA AMSIMAMISHA KAZI KASONGO

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline Dar Es Salaam Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), imeelezwa kuwa Rais wa TFF Wallace Karia amemsimamisha kazi Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Almasi Kasongo. Sambamba na hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi TPLB, Steven Mnguto naye amewasilisha barua rasmi ya kujiuzulu nafasi yake, huku TFF ikipokea uamuzi huo. Taarifa hiyo imetolewa leo Juni 13, 2025 na Katibu Mkuu wa TFF, CPSP (T) Kidao Wilfred.

WAZIRI MKUU KUWA MGENI RAsMI KWENYE UZINDUZI WA "SAMIA LEGAL AID",

Image
          Na Angelina Mganga,DmNewsonline ‎            ‎DAR ES SALAAM ‎ ‎WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majali anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kampeni ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia itakayofanyika katika Viwanja vya Maturubai Mbagala Jijini Dar es Salaam. ‎ ‎Akizungumza na waandishi wa habari Leo Juni 13,2025 Jijini Dar es Salaam Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Albert Chalamila amesema kutokana na changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili wananchi hasa wa mkoa wa Dar es salaam,Wizara ya Katiba na Sheria kupitia kampeni hiyo  itaendesha zoezi la kutoa msaada wa kisheria kwa siku 10 mfululizo kuanzia Juni 16-25,2025 ‎ ‎ ‎RC Chalamila ametoa wito kwa wakazi wa Jiji hilo kuwa kampeni hii itazinduliwa siku hiyo na baada ya hapo itaendelea katika Halmashauri zote ndani ya mkoa huu ‎ ‎ Ametaja huduma  zitakazotolewa zinahusu msaada wa kisheria zikiwemo Mirathi,Migogoro ya adhi, uvunjifu wa hak...

HALMASHAURI YA JIJI LA DAR YATENGA BILIONI 6.2 BAKETI YA 2025/2026 IDARA Y ELIMU SEKONDARI

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline  ‎       ‎DAR ES SALAAM  ‎ ‎HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam wameketi katika kikao  kazi cha kutathimini miradi ya maendeleo ya Elimu Sekondari  ambapo mwaka 2025/2026 wametenga bilioni 6.2 kwenye bajeti katika ujenzi na uboredhaji wa miundo mbinu ndani ya Halmashauri. ‎ ‎Akizungumza katika kikao Leo Juni 12,2025  Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Jiji ,Elihuruma Mabelya amesema kwamba kikao hicho cha tathimini kinahusisha idara ya Elimu Sekondari ambapo tathimini hiyo imejikita katika kuhakikisha kwamba mapungufu ambayo yamejitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ndani ya mwaka wa fedha huu hayajitokezi mwaka wa fedha ujao. ‎ ‎"Tumejikita katika utekelezaji wa mwanzo mpya wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya elimu Sekondari",amesema ‎ ‎Amesema tumeshuhudia Idara ya elimu Sekondari imefanya vizuri kwenye michezo ya Umiseta ambapo wefanikiwa kupata vikombe vyakutosha na kuvikabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Il...

HALMASHAURI YA JIJI LA DAR YATENGA BILIONI 6.2 BAKETI YA 2025/2026 IDARA Y ELIMU SEKONDARI

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline  ‎       ‎DAR ES SALAAM  ‎ ‎HALMASHAURI ya Jiji la Dar es Salaam wameketi katika kikao  kazi cha kutathimini miradi ya maendeleo ya Elimu Sekondari  ambapo mwaka 2025/2026 wametenga bilioni 6.2 kwenye bajeti katika ujenzi na uboredhaji wa miundo mbinu ndani ya Halmashauri. ‎ ‎Akizungumza katika kikao Leo Juni 12,2025  Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Jiji ,Elihuruma Mabelya amesema kwamba kikao hicho cha tathimini kinahusisha idara ya Elimu Sekondari ambapo tathimini hiyo imejikita katika kuhakikisha kwamba mapungufu ambayo yamejitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ndani ya mwaka wa fedha huu hayajitokezi mwaka wa fedha ujao. ‎ ‎"Tumejikita katika utekelezaji wa mwanzo mpya wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya elimu Sekondari",amesema ‎ ‎Amesema tumeshuhudia Idara ya elimu Sekondari imefanya vizuri kwenye michezo ya Umiseta ambapo wefanikiwa kupata vikombe vyakutosha na kuvikabidhi kwa Mkuu wa Wilaya ya Il...