ACT WAZALENDO WAZINDUA OPERESHENI MAJI MAJI kWA NCHI NZIMA


    Na  Mwandishi wetu,DmNewsOnline
              ‎DAR ES SALAAM 
‎CHAMA cha  ACT Wazalendo kimezindua rasmi operesheni Maji Maji itakayoanza kuanzia  Julai 1 hadi 15,2025 ambayo ni kampeni maalum ya kuwaamsha watanzania kurejesha thamani ya kura zao na kampeni hiyo itakuwa kwa nchi nzima na  itaongozwa na Kiongozi wa Chama Dorothy Semu.
‎Hayo yamebainishwa leo Juni 29,2025 Jijini Dar es Salaam na Naibu Mwenezi ,Shangwe Ayo  wakati wa mkuatano na waandishi wa habari  amesema kwamba baada ya kazi kubwa ya uimarishaji wa chama katika mgazi za majimbo na kuwapokea watu mbalimbali wanaojiunga na chama .
‎Naibu Mwenezi Ayo amesema kwamba ACT Wazalendo inafanya kazi ya kuunganisha makundi yote ya jamii  katika kulinda Demokrasia Yetu kwa kuhakikisha kuwa thamani ya kira inalindwa ifikapo Mwezi Oktoba 2025.
‎Aidha ,ameeleza kwamba katika Operesheni hiyo kutakuwa na misafara miwili ambapo msafara WA kwanza utaongozwa na Kiongozi wa Chama na msafara mwingine utaongozwa na Kiongozi mstaafu Zitto Kabwe.
‎Pia amesema kwamba Kiongozi wa Chama ataongozana na  Makamu Mwenyekiti Bara,Isihaka Mchinjita na watakwenda majimbo yaliyopo kwenye Mikoa ya Kigoma,Simiyu,Shinyanga,Arusha,Kilimanjaro,Tanga na Dar es Salaam.
‎Sambamba na hayo msafara wa Kiongozi wa Chama Msataafu, Zitto Kabwe pamoja n Naibu Katibu Mkuu Bara Ester Thomas watakwenda kwenye majimbo yaliyopo kwenye mikoa ya Tabora,Katavi,Rukwa,Mbeya,Ruvuma,Selous,Mtwara,Lindi na Mwambao.
‎Amemalizia kwakusema kwamba ziara hii pia itaambatana na mikutano ya hadhara,viongozi watafanya vikao vya ndani vitakavyojumuisha wajumbe wa Mikutano Mikuu pamoja na watia Nia wa Ubunge na Udiwani
‎ 

Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA TATU WA KIMATAIFA WA WATU WENYE ULEMAVU UJERUMANI.