Posts

Showing posts from May, 2024

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAOMBA KUIDHINISHIWA BAJETI YA SHILINGI 348,125,419,000 KWA MWAKA WA FEDHA 2024/2025

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline Wizara ya Maliasili na Utalii imeomba kuidhinishiwa Bajeti ya jumla ya Shilingi Bilioni 348,125,419,000 (bilioni mia tatu arobaini na nane milioni mia moja ishirini na tano laki nne na elfu kumi na tisa) kwa matumizi ya Mwaka wa Fedha 2024/2025.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amesema hayo leo Mei 31/05/2024 wakati wa akiwasilisha Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii Bungeni jijini Dodoma. Amesema kati ya fedha hizo zilizoombwa, Shilingi 250,884,083,000 (bilioni mia mbili hamsini milioni mia nane themanini na nne na elfu themanini na tatu) ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Shilingi 97,241,336,000 (bilioni tisini na saba milioni mia mbili arobaini na moja laki tatu na elfu thelathini na sita) ni za Miradi ya Maendeleo. Fedha za Matumizi ya Kawaida zinajumuisha Shilingi 125,366,391,000 (bilioni mia moja ishirini na tano milioni mia tatu sitini na sita laki tatu na elfu tisini na moja) za Mishahara na Shilingi 125,517,6...

UMATI WA WANANCHI WAJITOKEZA KWA WINGI KUMZIKA BABA WA MBUNGE KOKA

Image
   Na Victor Masangu,DmNewsOnline    KILIMANJARO MAELFU  ya  wananchi,viongozi, wa serikali,wakiwemo mawaziri  wakuu wa Wilaya wakuu wa Mikoa,Wabunge  viongozi wa  dini,madiwani na viongozi wa mashirika wamejitokeza kwa kwa ajili ya kumzika aliyekuwa Baba mzazi wa Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini mzee Francis Koka  katika nyumba yake ya milele. Mazishi hayo ambayo yamefanyika nyumbani kwa marehemu  katika eneo la kijiji cha Mkolowonyi kata ya Mvienyi  mkoani Kilimanjaro  yameweza pia kuhudhuriwa  na mwakilishi wa Rais wa awamu ya sita Dkt.Samia Suluhu Hassan Felister Mdeme  pamoja na wawakilishi wa wabunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akitoa salamu za rambi rambi  kwa niaba ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  mwakilishi  wake Felister Mdeme ametoa pole kwa familia ya Mbunge Koka  kutokana na kufiwa na baba yake. "Nimeagizwa na Rais Samia kuja hapa Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya kuweza kuto...

WASHINDI WAWILI WA SHINDANO LA UUZAJI NA USAMBAZAJI VILAINISHI VYA ORYX KWENDA DUBAI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  DAR ES SALAAM KAMPUNI  ya Oryx Services and Specialties ltd  imeendesha shindano la wauzaji na wasambazaji wa vilainishi vya Oryx  Energies na kupata washindi wawili  ambao wamejishindia safari ya kwenda Dubai na Leo Mei 31 ,2024 wameweza kukabidhiwa tiketi zao. Hafla hiyo fupi ya makabidhiano tiketi imefanywa na Mkurugenzi Mkuu wa Oryx Energies Tanzania Kalpesh Mehta kwenye ofisi za Kampuni hiyo zilizopo Kinondoni _victoria ambapo pamoja na mambo mengine  amesema Kampuni ya Oryx Services and Specialties Ltd iliendesha shindano hilo la wauzaji (Mawakala)na wasambazaji  kati ya Maduka ya Oryx na wasambazaji wa Vilainishi vya Oryx.  Mehta amesema shindano hilo lilianza Januari na kumalizika Desemba 2023 na kwamba leo hii wametangaza washindi wa shindano hilo ambao ni Mbise Oil Shop iliyopo Arusha (Oryx Shop) na Lwimba Investment Company Ltd iliyopo Dar es salaam (Msambazaji). Ameongeza kuwa zawadi wa shindano hilo ame...

HII HAPA KAULI YA FCC KUHUSU MATUMIZI YA AKILI MNEMBA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline Tume ya ushindani (Fcc) imeomba serikali kupitia  mamlaka zake kuweka utaratibu wa kiudhibiti utakao wataka watoa  huduma kupitia mfumo  ya teknolojia kuweka bayana  changamoto zinazoweza kujitokeza kwa walaji wanapotumia teknolojia na namna wanavyoweza kuzitatua changamoto hizo. Pia amezitaka Mamlaka za usimamizi wa soko ikiwemo FCC na Mamlaka nyingine zinazosimamia mifumo ya teknolojia kukaa pamoja na kujadili ili kuja na mapendekezo ya namna bora zaidi ya kusimamia eneo hilo. Hayo ameyasema leo Mei 30 jijini Dar es salaam na  ,Mwenyekiti wa Tume ya  Ushindani (FCC), Dkt Aggrey Mlimuka wakati wa kongamano la matumizi ya akili mnemba yanayozingatia haki na uwajibikaji kwa mlaji   lililoenda sambamba na kauli mbiu isemayo 'Matumizi ya Akili mnemba yanayozingatia Haki na Uwajibikaji kwa Mlaji. "Sote tuna shauku ya kuboresha na kurahisisha utoaji wa huduma kwa ubora zaidi kwa walaji kwa kutumia teknolojia kama nyenzo m...

ATE YAZINDUA TUZO YA MWAJIRI BORA WA MWAKA 2024

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsTz CHAMA Cha Waajiri Tanzania -ATE kimezindua rasmi Tuzo ya Mwajiri Bora wa mwaka 2024 ambapo lengo la Tuzo hiyo ni kuhamasisha Waajiri  kuweka juhudi katika usimamizi wa rasilimali watu kwa kuweka  misingi, kanuni na mikakati yenye mahusiano bora mahala pa kazi Ili kuwezesha kufanya biashara zenye Tija kwa taifa. Akizungumza Jijini Dar es Salaam Leo Mtendaji Mkuu wa ATE Bi. Suzanne Ndomba  amesema Mwaka huu vigezo vitatu vimeongezwa kwenye orodha ya tuzo zitakazoshindaniwa ambapo vigezo hivyo ni pamoja na Afya na Usalama pahala pakazi, Mwitikio dhidi ya VVU na Ukimwi na Utengenezaji wa Ajira. Amesema katika kigezo Cha tuzo ya Mwitikio Dhidi ya VVU na Ukimwi lengo ni kuunga mkono juhudi na malengo ya serikali katika kupambana na maambukizi dhidi ya Ukimwi, kupinga unyanyapaa na vifo vitokanavyo na maambukizi ya Ukimwi. Aidha ameeleza kwamba vipengele vya utoaji tuzo kwa Mwaka 2024 vitakuwa 17 ambavyo ni Ubora katika Usimamizi wa Rasilimali watu, tu...

MRADI WA TASAF WALETA NEEMA KWA WAKULIMA BUHIGWE

Image
Na Allan Vicent,DmNewsOnline  KIGOMA WAKAZI wa Kijiji cha Songambele katika Kata ya Mnyegera, tarafa ya Muyama Wilayani Buhigwe Mkoani Kigoma wamepongeza serikali ya awamu ya 6 inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea miradi wezeshi ambayo imeleta neema kubwa miongoni mwa jamii. Wakizungumza na Waandishi wa Habari waliofika Kijijini hapo jana kujionea manufaa waliyopata walengwa wa TASAF katika kipindi cha miaka 3 ya Utawala wa Rais Samia wameeleza kufurahishwa na uamuzi huo kwani umewainua kiuchumi. Mariam Sogoti (50) mkulima mkazi wa Kijiji hicho ambaye ni mnufaika wa mpango huo ameeleza kuwa walibuni kujenga daraja la mbao linalounganisha vitongoji vya Kumsenga na Bulambila na serikali ikawaletea zaidi ya sh mil 10. ‘Huu mradi umetusaidia sana, kwanza tumepata kipato, pili wakati wa mvua tulikuwa tunashindwa kupita kwa sababu mto ulikuwa unajaa sana maji hivyo kukwamisha shughuli zetu za kilimo lakini sasa tunapita wakati wote’, amesema. Mzee Lulamye Midaho (80...

BREAKING NEWS : RAIS SAMIA AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI MBALIMBALI

Image

SUGU ASHINDA UWENYEKITI CHADEMA KANDA YA NYASA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu Sugu ametangazwa Mshindi kwenye uchaguzi wa kumtafuta Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa ambapo amemuangusha aliyekuwa anatetea kiti hicho, Mchungaji Peter Msigwa. Matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika leo May 29,2024 katika Mji wa Makambako Mkoani Njombe yametangazwa usiku huu baada ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CHADEMA Kanda ya Nyasa kupiga kura. Sugu ameshinda kwa asilimia 51 huku Mchungaji Msigwa akipata asilimia 49 ya kura zilizopigwa. Kwa upande wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Mshindi ni Frank Mwakajoka ambaye ni Mbunge wa zamani wa Tunduma.

AMENDI NA UBALOZI WA USWIS WAENDELEA NA MKAKATI WA KUPUNGUZA AJALI ZA BARABARANI.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  TANGA  SHIRIKA  la Amend kwa kushirikiana na Ubalozi wa Uswis wamefanikiwa kuweka miundombinu salama barabarani yenye lengo la kuhakikisha wanafunzi wanavuka salama katika safari ya kwenda na kurudi shuleni  Miundombinu hiyo salama ya barabara imefanyika katika Shule ya Msingi Makorora pamoja na Shule ya Msingi Azimio kwa kuwekewa vivuko vya Pundamilia, njia za watembea kwa miguu pamaja na alama muhimu za usalama barabarani. Akizungumza mara baada ya kuweka miundombinu hiyo Mkurugenzi wa Shirika la Amend Tanzania Simon Kalolo amefafanua mradi huo umehusisha ujenzi wa njia za watembea kwa miguu, vivuko 4 vya pundamilia, matuta saba ya kupunguza mwendo kasi, alama 15 za barabarani, na michoro 16 ya usalama barabarani. Pia wametoa elimu ya usalama barabarani  kwa wanafunzi 1,694 na walimu wa shule za msingi Makorora na Azimio ndani ya mwezi tano, 2024 Tanga na Tanzania kwa ujumla. Kalolo amesema mpango wa kuboresha miundombinu salama...

MAAFISA UNUNUZI WAASWA KUTUMIA MIFUMO YA UNUNUZI KIELETRONIKI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Chande (Mb.) amewaasa maafisa ununuzi wa taasasi za Serikali kuhakikisha kuwa shughuli zote za ununuzi wa umma zinafanyika katika mfumo wa ununuzi wa umma kieletroniki (NeST) ikiwa ni pamoja na kutumia moduli ya kuwasilisha malalamiko kieletroniki. Agizo hilo limetolewa na Mhe. Chande wakati wa ufunguzi wa mafunzo siku mbili Jijini Dar es Salaam kuhusu moduli ya uwasilishaji wa malalamiko/rufaa kwa njia ya kieletroniki yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Rufani ya Zabuni za Umma (PPAA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa mikoa ya Dar es Salaam, Tanga Morogoro na Pwani. Pamoja na mambo mengine, Mhe. Chande amezielekeza Taasisi zote za serikaali kutumia mfumo wa ununuzi kieletroniki bila kuwa na kisingizio chochote kile. “Napenda kuzielekeza taasisi nunuzi zote nchini kuhakikisha wanatumia mfumo wa NeST na endapo yatatokea malalamiko basi mshikamane kwa pamoja kati ya mlalamikaji, mtoa haki na mla...

MWENYEKITI ADC ATANGAZA KUACHIA NGAZI ,KUGOMBEA URAIS 2025.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM MWENYEKITI wa Chama cha Allience For Democratic Change ADC Hamad Rashid  Mohamed  ametangaza kung'atuka rasmi kwenye nafasi ya mwenyekiti wa Chama hicho taifa huku akitoa raia Kwa wanachama kujitokeza kugombea. Amesema Juni 27,mwaka huu Chama hicho kinatarajia kufanya uchaguzi mkuu baada ya kukamilika Kwa chaguzi za ndani ambapo pia ametumia nafasi hiyo kuutangazia umma hususani wanachama wa Chama hicho kwamba Yeye hatagombea tena nafasi hiyo badala yake Yuko tayari kugombea urais uchaguzi ujao kwasababu bado ana nguvu. Hamad ameyasema hayo Leo Mei 29 ,2024 jijini Dar es Salaam katika Makao makuu ya Chama hicho  Buguruni wilayani Ilala wakati akizungumza na waandishi wa habari  ambapo pia amesema yupo tayari kugombea urais mwaka 2025 kupitia Zanzibar kama wanachama wataridhia. "Chama hiki ni Chama ambacho kinafuata Demokrasia na Kuna utaratibu wa miaka kumi ya kukaa madaraka Kwa maana vipindi viwili vya miaka mitano na mim...

EMIRATES UNVEILS THE EXCLUSIVE FINE WINE

Image
DmNewsOnline,Dubai Emirates is offering an unparalleled fly better experience to wine enthusiasts and connoisseurs, launching even more rare vintages in the sky this summer - a remarkable collection of the most acclaimed wines of their respective regions, all onboard at the same time. In First Class, customers on routes from Dubai to the UK and Americas will now be treated to complimentary Dom Pérignon Rosé 2008, exclusively served onboard Emirates.  This luxury rosé champagne is a rare release of exceptional quality with very limited stock, expected to be onboard for just three months.  The superb 2008 vintage of Dom Pérignon rosé has a bold assemblage created with Pinot Noir grapes.  The fruit element and superb structure balance the tension between the precision and natural radiance of the rosé, giving it more body and weight.  The 2008 bouquet bursts forth with raspberries and wild strawberries, and powdery notes of iris and violet immediately meld with the fruit...

MTENDAJI WA KATA JELA MIAKA 3 KWA KUOMBA RUSHWA

Image
Na Allan Vicent, DmNewsOnline  KALIUA  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilayani Kaliua Mkoani Tabora imemhukumu kifungo cha miaka 3 jela Mtendaji wa Kata ya Nh’wande na mwenzake wa Kijiji cha Imagi baada ya kutiwa hatiani kwa kuomba na kupokea rushwa ya sh. mil 3. Akitoa hukumu hiyo juzi Hakimu Mkazi Mwandamizi Felix Ginene amesema kuwa ametoa hukumu hiyo ili iwe fundisho kwa watumishi wengine wenye tabia kama hizo katika Wilaya hiyo na mahali pengine. Ametaja Mtendaji wa Kata hiyo aliyehukumiwa kuwa ni Laurent Isaya Sendu na mwenzake Richard Mpagama wa Kijiji Cha Imagi kilichoko katika kata hiyo ambao waliomba rushwa ya sh mil 3 kwa mkazi wa Kijiji hicho. Amebainisha kuwa ni kosa kwa Kiongozi yeyote kutumia madaraka yake vibaya dhidi ya wananchi anawaongoza kwani kufanya hivyo ni kuwanyima haki zao kisheria. ‘Rushwa ni adui wa haki, inapobainika Kiongozi katumia madaraka yake kuomba au kupokea rushwa, sheria itachukua mkondo wake, vitendo vya rushwa havikubaliki mahali popote kwa k...

RC TABORA AONYA WALIMU WANAOGOMEA UHAMISHO

Image
  Na Allan Kitwe,DmNewsOnline TABORA  MKUU wa Mkoa wa Tabora, Paul Matiko Chacha, amewaagiza walimu 2 wa shule ya Msingi Mabatini iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Tabora waliogoma kuripoti katika vituo vyao vipya vya kazi kuripoti haraka iwezekanavyo. Ametaja walimu hao kuwa ni Juma Mahundi na Rose Mgaya ambao walipewa uhamisho Mei 6 mwaka huu na kutakiwa kuripoti katika vituo vipya vya kazi vilivyopo katika manispaa hiyo lakini wakagoma kufanya hivyo. RC ametoa agizo hilo jana alipotembelea Shule ya Msingi Mabatini iliyopo katika manispaa hiyo ili kujionea maendeleo ya shule hiyo kitaaluma na kuzungumzia na walimu juu ya masuala mbalimbali yahusuyo maendeleo ya shule hiyo. Amesema kuwa Mwalimu Rose Mgaya alihamishiwa katika Shule ya Msingi Farm Nyamwezi na Juma Mahundi alihamishiwa katika Shule ya Msingi ya Ndevelwa, katika halmashauri ya Manispaa hiyo lakini hawajaripoti hadi sasa. Amebainisha kuwa walimu hao licha ya kutakiwa kuondoka katika kituo chao cha zamani w...

MWENEZI MRAMBA KUSHUSHA MICHUANO YA MBIO ZA SAMIA ONE MARATHON PWANI

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline   PWANI KATIBU  wa Siasa na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani ndugu David Mramba katika kuunga mkono juhudi za Rais wa awamu ya sita Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kukuza sekta ya michezo anatarajia kuanzisha mashindano maalumu ya mbio za miguu zitakazojulikana  kwa jina la Samia One Marathon ambazo zitazishirikisha taasisi mbalimbali zinazofanya shughuli zake ndani ya Mkoa wa Pwani. Akizungumza na waandishi wa habari Ofisi kwake Leo Mei 29,2024  kuhusiana na maandalizi hayo Mwenezi alisema kwamba lengo kubwa la kuanzisha mashindano hayo ni kwa ajili ya kuweza kukuza mchezo huo wa riadha, kubadilishana mawazo na wadau mbali mbali  wa Mkoa wa Pwani ili kuweza kuimarisha mahusiano  baina ya chama cha mapinduzi (CCM)  pamoja na  wadau  na taasisi ikiwa sambamba  na kujenga afya zao. Mramba amesema kwamba katika mashindano  hayo ambayo yanatarajiwa kufanyika Juni mwaka  2024...

SAMIA AKAMILISHA AHADI MANYONI, KATIBU MKUU CCM DKT.NCHIMBI AKABIDHI.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  MANYONI  MWENYEKITI  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan leo Mei 29,2024  kupitia Katibu Mkuu wa chama hicho Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekipatia chama wilaya ya Manyoni zaidi ya shilingi millioni 18 kwa ajili ya kuezeka jengo lake la kitega uchumi. Katibu Nchimbi  ameyasema hayo mbele ya Kamati ya Siasa ya Wilaya, mjini Manyoni, ikiwa ni mwanzoni mwa ziara yake ya siku mbili mkoani Singida. Amesema fedha hizo zimetokana na  ahadi ya Mwenyekiti ambaye ni  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Hassan Suluhu  aliyoitoa kupitia kwa Katibu Mkuu wa zamani Daniel Chongolo.