SAMIA AKAMILISHA AHADI MANYONI, KATIBU MKUU CCM DKT.NCHIMBI AKABIDHI.



Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline 
MANYONI 

MWENYEKITI  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu Hassan leo Mei 29,2024  kupitia Katibu Mkuu wa chama hicho Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amekipatia chama wilaya ya Manyoni zaidi ya shilingi millioni 18 kwa ajili ya kuezeka jengo lake la kitega uchumi.

Katibu Nchimbi  ameyasema hayo mbele ya Kamati ya Siasa ya Wilaya, mjini Manyoni, ikiwa ni mwanzoni mwa ziara yake ya siku mbili mkoani Singida.

Amesema fedha hizo zimetokana na  ahadi ya Mwenyekiti ambaye ni  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Hassan Suluhu  aliyoitoa kupitia kwa Katibu Mkuu wa zamani Daniel Chongolo.



Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025