KATIBU MKUU WA CCM DKT. NCHIMBI AFIKA MSIBANI KWA MKE WA GACHUMA,TARIME NA KUTOA POLE.



Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline
TARIME

KATIBU  Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amewasili wilayani Tarime, Mkoa wa Mara, kushiriki mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Jimbo la Mara Kaskazini, Francisca Mwita Gachuma.

Francisca ni mke wa wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Christopher Mwita Gachuma 

Dkt .Nchimbi baada ya kuwasili msibani nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Bomani, Tarime Mjini, leo Ijumaa, Machi 29, 2024, amepokelewa na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Katibu Balozo Dkt Nchimbi ametoa pole Kwa  wafiwa, wakiongozwa na Familia ya Mzee Gachuma, pamoja na kushiriki ratiba ya awali ya msiba, kabla ya mazishi yatakayofanyika Machi 30, 2024, huko Komaswa,  Mjini Tarime






Comments

Popular posts from this blog

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE TAMISEMI YAKOSHWA NA UBORA WA MIRADI YA MAENDELEO KIBAHA TC

MAMBO 10 MAZITO YANAYOIANGAMIZA NA KUIZAMISHA CHADEMA 2024/2025