Posts

Showing posts from December, 2023

Emirates Yashinda Tuzo ya Kampuni Bora ya Usafiri na Vifaa vya ugavi katika Tuzo za Biashara za Gulf 2023

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline  Kampuni ya Emirates inayojulikana kwa ubora wake katika huduma, dhamira ya kuboresha uzoefu wa wateja, na juhudi zake za mara kwa mara katika uvumbuzi, imeshinda tuzo ya Kampuni Bora ya Usafiri na Vifaa vya ugavi katika Tuzo za Biashara za gulf 2023. Tuzo hii inathibitisha tena azma ya ndege hii ya kutoa uzoefu usio na kifani angani na ardhini, katika madaraja yote ya ndege. Heshima hii ilikabidhiwa kwa Sheikh Majid Al Mualla, Makamu wa Rais Mwandamizi wa Masuala ya Kimataifa wa Emirates, katika sherehe iliyofanyika katika hoteli ya Palazzo Versace. Tuzo za Biashara za Gulf ni tuzo muhimu katika kutambua mafanikio kwa biashara, viongozi, na wajasiriamali katika tasnia mbalimbali kuanzia benki, fedha na uwekezaji, ujenzi na mali isiyohamishika, huduma za afya, usafiri na vifaa vya ugavi, teknolojia, mauzo ya rejareja, na ukarimu katika eneo la Gulf. Vigezo vya kutathmini wawaniaji vinajumuisha ubunifu, ukuaji, matokeo ya kifedha, ubora wa bidhaa, utoa...

EMIRATES DOMINANCE AT 2023 WORLD TRAVEL AWARDS SETS NEW INDUSTRY BENCHMARKS.

Image
Emirates, the renowned aviation giant, continues to solidify its global supremacy, clinching an impressive five prestigious accolades at the esteemed 2023 World Travel Awards Grand Final. The airline’s victories across multiple categories, from inflight entertainment to brand excellence, reaffirm Emirates’ unwavering commitment to elevating the travel experience for its customers. In a remarkable feat, Emirates secured the coveted title of World’s Leading Airline for the Middle East for the third consecutive year, alongside accolades for Leading Airline Inflight Entertainment, Leading Airline Brand, and Leading First Class. The airline’s loyalty program, Emirates Skywards, also claimed its dominance as the World’s Leading Rewards Programme, marking an astonishing 10 wins out of 12 ceremonies. Investing in Unmatched Customer Experience: Emirates’ ethos, that travel transcends beyond mere destinations, underscores the airline’s ongoing investments in enriching the customer journey. A com...

DKT. BITEKO AWASILI MKOANI SHINYANGA

Image
NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati,  Dkt. Doto Biteko amewasili mkoani Shinyanga akitokea jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi leo Disemba 29, 2023. Alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kahama, Dkt. Biteko alipokelewa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Chama cha Mapinduzi mkoani Shinyanga  akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Johari Samizi, Mbunge wa Ushetu, Mhe. Emanuel Cherehani na Mbunge wa Kahama Mjini, Mhe.Jumanne Kishimba.

WAKULIMA WATAKIWA KUMUUNGA MKONO RAIS DKT SAMIA - MAJALIWA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  RUANGWA WAZIRI  Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka msisitizo katika kuendeleza Sekta ya kilimo kwenye mazao ya chakula na Biashara. Amesema lengo ni kuhakikisha nchi inajitosheleza kwa chakula na kila Mtanzania anayejishughulisha na kilimo aweze kukuza kipato chake na uchumi na  taifa kwa ujumla. Majaliwa ameyasema hayo leo Disemba 29,2023 wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Juhudi B kwenye kata ya Chinongwe, Ruangwa mkoani Lindi. "Rais Dkt. Samia wakati wote amedhamiria kuhakikisha Tanzania inakuwa kimbilio la wengine wanaohitaji mazao “ Nakuongeza kuwa "Tumuunge mkono Rais wetu kwenye mapambano yake ya kukuza sekta ya kilimo, amefanya makubwa kwenye sekta ya kilimo ikiwemo kuagiza kutengwa kwa maeneo ya kilimo kwa ajili ya vijana”amesema Majiliwa

VINGOZI WA DINI WATAKA TIP ISAMBAZE ELIMU DHIDI YA UKATILI WA KIJINSIA VIJIJINI

Image
Na  Paul Kayanda,DmNewsOnline  KAHAMA VIONGOZI wa madhehebu ya Dini Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga,wamebainisha changamoto mbalimbali zinazokwamisha juhudi za kusambaza Elimu dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia vijijini ikiwemo  shida ya usafiri ili kuwafikia walengwa hao. Viongozi hao wamesema kuwa,mara nyingi vitendo vya ukatili wa kijinsia hufanyika katika maeneo ya vijijini ambako hakuna msaada wowote tofauti na maeneo ya mijini ambako ambako pia matukio hayo yameshamiri hivyo viongozi wametumia fursa hiyo kuliomba Shirika la TIP pamoja na Serikali kuhakikisha kuwa wanasambaza Elimu  katika maeneo ya Vijijini. Ally Athumani Ally pamoja na viongozi wengine wamesema hayo  Leo Disemba 28,2023 kwenye kikao cha uwasilishaji wa taarifa za kupinga na kuzuia ukatili wa kijinsia kilichojumuisha viongozi wa madhehebu mbalimbali katika makundi ya viongozi wa dini Kwa maana  Taassisi za TEC, CPCT, BAKWATA pamoja na CCT kilichofanyika katika Manispaa hiyo....

WASIOENDELEZA LESENI ZAO ZA MADINI KUFUTIWA KWA MUJIBU WA SHERIA- WAZIRI MAVUNDE

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  WAZIRI wa Madini Anthony Peter Mavunde amewataka wamiliki Leseni  za madini nchini kuziendeleza leseni husika kwa mujibu wa sheria inavyoelekeza kwa kuwa zipo leseni nyingi ambazo hazifanyiwi kazi na hivyo kuzorotesha ukuaji wa kasi wa sekta ya madini. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Disemba 28 ,2028  Wilayani Ruangwa, mkoani Lindi wakati alipotembelea Mgodi wa Madini Kinywe wa Lindi Jumbo ambao unatarajia kuanza uzalishaji mwishoni mwa mwezi Machi,2024. Akitoa taarifa ya Mradi,Meneja Msimamizi wa Mradi  Mhandisi Chediel Mshana amesema ujenzi wa mgodi huo umefikia 90% na kwamba ifikapo mwezi Machi,2024 mgodi utakuwa umeanza uzalishaji rasmi wa madini ya kinywe. “Ninawapongeza Lindi Jumbo kwa hatua kubwa ya ujenzi ulipofikia na ahadi ya kuanza uzalishaji rasmi wa madini mkakati haya mapema mwaka 2024."amesama Huu utakuwa kati ya miradi michache mipya ya uchimbaji wa madini mkakati ya kinywe nchini Tanzania ambao utakuwa umeanza hivi k...

WAZIRI MAVUNDE ATEMBELEA MRADI WA LINDI JUMBO

Image
 Na Mwandishi Wetu, DmNewsOnline  LINDI WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Desemba 28, 2023 ametembelea mradi wa Lindi Jumbo Limited uliopo Wilaya ya Ruangwa Mkoa wa Lindi kwa lengo la kufuatilia maendeleo ya ujenzi wa mgodi wa madini ya kinywe (graphite) Awali akielezea maendeleo ya ujenzi wa mgodi huo, Meneja wa Mradi, Chediel Mshana ameeleza kuwa mradi huo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mtambo wa uchenjuaji umefikia zaidi ya asilimia 90 ambapo uzalishaji wa   madini ya kinywe unatarajia kuanza mapema Machi, 2024. Ziara hii ni sehemu ya ziara za Waziri Mavunde zenye lengo la kukagua shughuli za uchimbaji wa madini nchini sambamba na kutatua changamoto mbalimbali. Katika ziara yake ameambatana na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Migodi na Mazingira, Mhandisi Henry Mditi kutoka Tume ya Madini na Kaimu Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Lindi, Dickson Joram

TAMASHA LA KILIMANJARO CULTURAL FESTIVAL KUKUZA UTALII MKOANI KILIMANJARO

Image
Na Happiness Shayo, DmNewsOnline  KILIMANJARO  WAZIRI  wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki (Mb) amesema Tamasha la Kilimanjaro Cultural Festival linalohusisha utamaduni wa vyakula ,ngoma na lugha za asili za jamii ya Wachaga, Wapare na Wamaasai litasaidia kukuza utalii wa Mkoani Kilimanjaro endapo litaendelezwa na kutumika ipasavyo. Amesema lengo la Tamasha hilo ni kukuza na kuhamasisha utalii wa malikale  ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro sambamba na kuenzi mila na desturi za  jamii za Mkoa huo zinazojumuisha Wapare, Wachaga na Wamaasai.  Ameyasema hayo leo Desemba 28,2023 alipokuwa akifunga tamasha hilo lililofanyika katika viwanja vya Kili Home Garden, Moshi Mjini Mkoani Kilimanjaro. “Nimeshuhudia vyakula vya kiasili vya jamii za Mkoa wa Kilimanjaro vilivyoandaliwa kwa ustadi mkubwa,  tukio hili limenikumbusha masuala ya afya kuhusu umuhimu wa vyakula vya asili ikiwa  ni pamoja na kukinga miili yetu na  kujenga nguvu mwilini na hii ndiyo s...

RAIS DK.MWINYI AZINDUA UWANJA MPYA WA AMAAN COMPLEX

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline RAIS  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imedhamiria kujenga  uwanja mpya mwingine wa kisasa ambao utatumika katika mashindano ya AFCON mwaka 2027. Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo akizindua rasmi Uwanja mpya wa Amaan Complex Desemba 27, 2023, Mkoa wa Mjini Magharibi.  Pia Rais Dkt.Mwinyi ameeleza kuwa Serikali imelenga kujenga miundombinu ya michezo kila wilaya kwa viwanja vipya vya kisasa.  Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika la maendeleo GIZ  imefunga mkataba wa makubaliano kwa ajili ya ujenzi wa viwanja vitano vya michezo midogomidogo ikiwemo mpira wa kikapu, mpira wa wavu , mpira wa mikono na mpira wa pete. Viwanja hivyo vinatarajiwa kujengwa Kangani Wilaya ya Mkoani, Mchangamdogo Wilaya ya Wete, Tumbatu na Mkokotoni Wilaya ya Kaskazini A na Haile Selasie Wilaya ya Mjini pamoja na viwanja vitatu vya Tennis Chakechake, Chuo kikuu...

UMOJA WA MABALOZI WA AFRIKA WAKABIDHI MSAADA HANANG

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline UMOJA wa Mabalozi wa nchi za Afrika wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania wamekabidhi msaada wa mifuko 1,000 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa nyumba kwa wananchi waliokumbwa na mafuruko na maporomoko ya udongo katika eneo la Katesh Wilayani Hanang mkoa wa Manyara. Akikabidhi msaada huo kwa Serikali, Kiongozi wa Mabalozi hao na Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed amesema kundi la Mabalozi wa nchi za Afrika wanaowakilisha nchi zao Tanzania lina mabalozi 24 ambao wameonesha kuguswa na mafuriko yaliyotokea Katesh na kuona ni vyema kuwasaidia wananchi hao pamoja na Serikali kwa ujumla kwa kuchangia mifuko 1,000 ya saruji. Dkt. El Badaoui Mohamed amesema umoja wa Mabalozi wa Afrika nchini wameguswa na mafuriko yaliyotokea Katesh na kwa umoja wao wamechangia  mifuko 1,000 ya saruji kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa eneo la Katesh ili kurejesha makazi ya wananchi hao. “Tunaendelea kuomba Mungu awajalie subira na kwa wal...

KESI YA PAULINE GEKUL YAFUTWA,BABATI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  MAHAKAMA ya wilaya ya Babati imeifutilia mbali kesi ya ukatili iliyokuwa inamkabili mbunge wa jimbo la Babati Mjini, Pauline Gekul kuhusu tuhuma za unyanyasaji kwa kijana Hashim Ally. Uamuzi huo umetolewa leo Desemba 27, 2023, na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya Babati, Victor Kimario na kusema ameifuta baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kuwasilisha taarifa ya kutokuwa na nia ya kuendelea na kesi hiyo. Kesi hiyo ilifunguliwa kupitia kwa wakili Peter Madeleka chini ya kifungu cha 128(2) na (4) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2022. Ambapo kwa upande wake Wakili Madeleka amesema hawajakubaliana na maamuzi hayo na kwamba watakata rufaa.  Kesi hiyo dhidi ya Mbunge Paulina Gekul ilifunguliwa na wakili huyo kwa kushirikiana na wenzake wakidai alimfanyia kitendo cha ukatili kijana huyo kwa kumuingizia chupa sehemu ya haja kubwa.

KARAFUU FURSA MPYA KWA WAKULIMA MOROGORO ,TANGA

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNews MOROGORO  MIKOA ya Morogoro na Tanga imepewa kipaumbele cha kulima zao la karafuu katika mpango wa pamoja wa serikali na wadau wa kilimo kutoka sekta binafasi na taasisi zisizo za kiserikali. Ongezeko la Mkoa wa Tanga katika ulimaji wa karafuu kitaifa limetangazwa katika Mkutano wa Wadau wa Kilimo na Mazingira waliokutana jijini Dar es Salaam. Wadau hao wamesema zao la karafuu limeonesha kustawi katika mikoa hiyo miwili, hivyo waamini ikipewa kipaumbele itaongeza uzalishaji.   "Morogoro ndiyo iliyotangulia na mwaka jana tu ilizalisha tani 2,000 sawa na nusu ya uzalishaji wa Zanzibar wa jumla ya tani 4,000, hivyo ongezeko la Tanga ni wazi Tanzania itakuwa mzalishaji mkubwa wa karafuu," wamesema wadau. Ulimaji wa karafuu Tanzania Bara umetokana utafiti na ushauri wa  Kituo cha Kuendeleza Kilimo Nyanda za Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), taasisi inayowashirikisha wadau katika sekta binafsi katika kulima mazao na kuendeleza minyororo ya thaman...

MTANDAO WAPONGEZA ZUIO LA KUINGIZA MBEGU NCHINI

Image
Na Mwandishi Wetu, DmNewsOnline  DAR ES SALAAM MTANDAO na Muungano wa Mashirika ya Kiraia na Vikundi vya Wakulima vinayounda Kikosi Kazi cha Mbegu Tanzania wamepongeza uamuzi wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), kuzuia ingizaji mbegu za mahindi na maharage ya Soya kutoka nchini Malawi. Pongezi hizo zimetolewa mtandao huo, kupitia Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha Mbegu cha Tanzania, Abdallah Mkindi ambapo amesema dhamira yao ni kutetea  haki na ustawi wa wakulima wadogo katika sekta ya mbegu.  Amesema kikosi hicho kinalenga kuendeleza mifumo ya mbegu inayosimamiwa na wakulima, ambayo inategemea kanuni za kilimo ikolojia, bioanuai, na uhuru wa chakula. “Sisi wanachama wa Kikosi Kazi cha Mbegu cha Tanzania, tunatoa pongezi zetu za dhati kwa juhudi za zilizochukuliwa na Wizara ya Kilimo na TPHPA kwa kuhakikisha maslahi ya wakulima wa Kitanzania na uadilifu wa mfumo wetu wa mbegu na kilimo cha kitaifa,” amesema. Amesema wanapongeza uamuzi wa kishujaa wa kuz...

CCM MAGOMENI DAR ES SALAAM YAJIPANGA KIMKAKATI KUWATUMIKIA WANANCHI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  DAR ES SALAAM MWENYEKITI wa Chama  Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Magomeni Mohamed Mwinyi amesema katika kuendelea kujiweka vizuri kiutendaji na kutatua baadhi ya changamoto za wananchi  kimeweza kufanya vikao mbalimbali kuanzia kwa viongozi wa Mabalozi hadi wale wa Matawi lengo likiwa ni kujua uhai wa chama na hasa kinapoelekea mwishoni mwa mwaka. Hayo yalitanabaishwa na Mwenyekiti wa Chama hicho wakati akizungumza na Mwandishi wa Habari hizi Jijini Dar es Salaam uku akisema wako vizuri na wamejipanga kwa ajili ya chaguzi zijazo. Amesema Chama kimekuwa karibu na wananchi wake lakini kubwa zaidi likiwa ni kujua changamoto wanazokabiliana nazo ikiwa ni pamoja na kufanya vikao kwa ajili ya kujua uhai wa chama. "Lakini pia kujiandaa na chaguzi za Serikali  za Mitaa, kuweka mahusiano mazuri kati ya Wananchi na viongozi wao kwani bila kufanya hivyo mnaweza kuambulia matokeo msiyo yatarajia," alisema Mwenyekiti Mwinyi. Kiongozi huyo  alise...

MABONDIA WAONESHANA UBABE TABORA

Image
Na Allan Ntana, DmNewsOnline TABORA MABONDIA zaidi ya 20 kutoka Mikoa ya Tabora, Morogoro, Kigoma, Mwanza na Shinyanga wameoneshana ubabe katika mashindano maalumu ya kusherehekea sikukuu ya krismas yaliyofanyika Mjini Tabora jana. Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Chama Cha Ngumi Mkoa wa Tabora kwa lengo la kuinua vipaji yameleta hamasa kubwa kwa vijana na mashabiki wa mchezo huo Mkoani humo. Akifungua mashindano hayo Afisa Utamaduni na Michezo wa Mkoa huo Hassan Katuli amepongeza ubunifu wa Viongozi wa chama hicho na kuahidi kuwatafutia vifaa vya michezo mabondia wa Mkoa huo ili kuinua vipaji vyao. Amebainisha kuwa ushindani mkubwa uliooneshwa na vijana wa Mkoa huo katika mashindano hayo ni ishara tosha kwamba kama watawezeshwa vifaa watafika mbali zaidi na kuwa mabondia wakubwa. ‘Nawapongeza viongozi wa ngumi wa Mikoa yote iliyoshiriki mashindano haya, naamini kupitia mashindano hayo watapatikana wapinzani wa akina Dula Mbabe, Twaha Kiduku, Mwakinyo na wengine, nitawatafutia vifaa v...

MBUNGE WA USHETU DKT. CHEREHANI AHADI KUEZEKA NYUMBA YA PADRE .KIGANGO CHA KISUKE.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  MBUNGE  wa jimbo la Ushetu mkoani shinyanga  Emmanuel Cherehani ameahidi kutoa mbao 300 zenye thamani ya shilingi 1,350,000 kwaajili ya kuezeka nyumba ya mapadre katika kanisa la mtakatifu Karolilwanga kigango cha Kisuke parokia ya Nyamilangano. Ahadi hiyo ametoa Leo Disemba 25 ,2023 katika Ibaada ya sikukuu ya Krismas ambapo  Cherehani amesema, katika kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu Kristo ni vyema pia waumini kuzaliwa upya katika Imani kwa kusali na kujenga kanisa  kwani uwepo wa nyumba ya mapadre utarahisisha utoaji wa huduma za kiroho. Pia  Cherehani amewataka wananchi wa Ushetu kudumisha amani na upendo kwani kusherehekea Krismas ni kukumbuka kuwa tunae Kristo anaetaka tusali na tusitende dhambi hivyo amewasihi kusherehekea sikukuu kwa utulivu na amani. Akizungumza kwa niaba ya waumini  Mwenyekiti wa kigango hicho Grace Kiondo amemshukuru mbunge wa jimbo la Ushetu kwa moyo wa kujitolea, ambapo ameahidi kuwa Wataendel...