WABUNGE ZAIDI 40 WASHIRIKI MKUTANO MKUU WA 14 WA AFRIKA WA JUKWAA LA UTAWALA WA MTANDAO
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline DAR ES SALAAM NAIBU Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ,Eng.Maryprisca Mahundi amefungua kikao Cha awali Jukwaa la Utawala wa Mtandao Barani Afrika. Akizungumza na waandishi wa habari Leo Mei 29,2025 Jijini Dar es Salaam amesema kwamba zaidi ya wabunge 40 toka nchi mbalimbali za Afrika wamehudhuria mkutano . Naibu Waziri Mahundi amesema kwamba kikao hicho ni maandalizi kuelekea ufunguzi rasmi wa mkutano unaotarajiwa kufunguliwa Mei 30,2025 unaohusu masuala ya Utawala wa Mtandao ambapo mkutano huo unafanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Aidha ,ameeleza kwamba serikali imejipanga kwa kuthibiti matumizi yasiyosahihi ya mitandao kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. "Wakati wa chaguzi mbalimbali wapo baadhi ya watu wanatumia vibaya mitandao hasa kudhalilisha wanawake kwahiyo wameonya kuwa hawatavumilia kwani sheria itac...