Posts

Showing posts from November, 2025

WATANZANIA MSIKUBALI KUYUMBISHWA KUINGIZWA KATIKA MACHAFUKO’

Image
      Mwandishi wetu,DmNewsonline WATANZANIA wameshauriwa wasikubali kuyumbishwa na wanaharakati ambao wenyewe wapo kwa ajili ya kuiona nchi ya Tanzania inavurugika na kukosa utulivu. Ushauri huo umetolewa leo Novemba 30 ,2025 jijini Dar es salaam na wanaharakati huru ambao wamemua kueleza hatua kwa hatua mbinu chafu ambazo zinatumiwa na baadhi ya wanaharakati ambao wamekuwa wakitafuta mbinu mbalimbali kuvuruga amani ya Tanzania. Wamesema kuwa sababu kubwa ya vurugu ambazo zinatengenezwa na wanaharakati hao wenye nia ovu na Taifa la Tanzania ni kutaka kuvuruga kasi ya ukuaji wa maendeleeo ambayo imekuwa tishio kwa baadhi ya nchi jirani. Akizungumza katika mkutano wake na waandishi wa habari Mwanaharakati Huru Ahmed Kombo amebainisha kuwa  tangu kuazishwa kwa vyama vingi nchini mwaka 1995 baadhi ya wanaharakati na vyama vya siasa vya upinzani vimekuwa vikilalamikia tawala zote ambazo zinapita katika uongozi wa nchi yetu. Amesema kuazia utawala wa Awamu ya Tatu ch...

MSAMA: TUWAPUUZE WANAOLIPWA KUVURUGA AMANI YETU

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNewsonline                     DAR ES SALAAM  MKURUGENZI wa Msama Promotions na Mfanyabiashara malufu nchi Tanzania  Alex Msama amewataka Watanzania kuwapuuza watu ambao wanalipwa ili kuvuruga amani ya nchi yetu ya Tanzania. Amesema maranyingi watu wanaofanya hivyo sio Watanzania na baadhi yao ni Watanzania wanaoishi nje ya nchi kama vile nchi jirani na Tanzania pamoja na mataifa mengine ya nje. "Watanzania wenzangu, nawasihi kwa moyo mmoja tuwapuuze watu wanaotaka kuvuruga amani yetu, maana watu hawa wanalipwa Mamilioni ili kuvuruga amani yetu tuliyo nayo."amesema  " Miongoni mwa watu hawa hawaishi hata hapa nchini bali wanaishi nje ya nchi na wengi sio Watanzania na wanalipwa na baadhi ya Watanzania na watu wengine wa nje ya nchi ili wavuruge amani yetu iliyoasisiwa na wazee wetu."amesisitiza  Nakuongeza kuwa, watu wanaofanya hivi furaha yao nikuona amani yetu inavurugika ili watuibie rasil...

NIDA, WANANCHI NENDENI MKACHUKUWE VITAMBULISHO ILI MUENDELEE KUPATA HUDUMA.

Image
 Na Timoth Marko,DmNewsonline             DAR ES SALAAM MKURUGENZI wa  Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), James Kaji amesema Mamlaka hiyo imetoa kibali maalum cha muda wa mwaka mmoja kwa ajili ya kushughulikia maombi ya marekebisho ya taarifa za wananchi kwenye Mfumo wa Utambulisho wa Taifa, kuanzia Oktoba 2025. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na mkurugenzi huyo katika mkutano wake na waandishi wa habari ambapo amesema kibali hicho kimetolewa ili kuwasaidia wananchi waliokumbwa na changamoto mbalimbali za usajili, ambazo awali zilishindikana kufanyiwa marekebisho kutokana na ukinzani wa miongozo iliyokuwepo. Amesema kibali hicho kinahusu makundi manne maalumu ambayo ni waathirika wa vyeti vya kughushi, wakiwemo waliowahi kufutwa kazi Serikalini na ambao taarifa zao za usajili wa NIDA zinatokana na vyeti hivyo pamoja na Watu waliotumia majina ya watu wengine kupata vyeti vya elimu.  Amesema kundi lingine ni wale  wali...

WAZIRI MAVUNDE ABAINISHA MIKAKATI YA KUIMARISHA BIASHARA YA TANZANITE NCHINI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline       MIRERANI ,SIMANJIRO WAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde, amesema Serikali imejipanga upya kuitangaza na kuiinua Tanzanite kimataifa kupitia mkakati wa kurejesha hadhi ya jiwe hilo adimu duniani. Akizungumza katika mkutano na wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini ya vito katika eneo tengefu la ukuta wa Magufuli, Mirerani mkoani Manyara, Waziri Mavunde amesema hatua hiyo inalenga kurejesha hadhi na uhitaji (*rebranding* )wa Tanzanite ili kuimarisha thamani na soko lake duniani. Katika Mkutano huo ambao pia ulihusisha hafla ya kukabidhi leseni kwa wanufaika 423, Waziri Mavunde amesema Serikali imedhamiria kurejesha minada ya madini ya vito kama njia ya kuongeza uwazi, ushindani na thamani ya madini ya vito nchini. Akifafanua zaidi, amesema Serikali inaendelea kukamilisha ujenzi wa Tanzanite Exchange Centre (TEC), jengo ambalo hadi sasa limefikia asilimia 98 ya ujenzi katika ghorofa mbili na kumtaka mkandarasi kuongeza kasi ili kitu...

CHINA NA TANZANIA KUBORESHA RELI YA TAZARA KWA KIWANGO CHA SGR.

Image
  Timothy Marko DmNews online               DAR ES SALAAM. BALOZI  wa China Nchini Tanzania Chen Mingjian amesema itaendelea Kudumisha Mahusiano ya Uchumi wa kikanda kati yake na Tanzania na Zambia katika kuboresha Sekta ya Miundombinu ikiwemo reli ya Tazara. Akizungumza Katika hafla ya makubaliano ya Ujenzi wa reli ya Tazara kwa kiwango cha Kimataifa SGR, Balozi Chen Mingjian amesema kuwa China ni mdau Muhimu wa Maendeleo kati ya Tanzania na Zambia kupitia reli ya Tazara. ,, Ilikuweza kuhakikisha Sekta ya Bandari inaimarika Sekta ya Miundombinu ya reli nimuhimu kuboreshwa kwa kiwango cha Kimataifa,, Amesema Chen Mingjian. Mingjian Ameongeza kuwa uboreshwaji wa Sekta ya Bandari kutawezesha Uchumi wa Nchini ambazo Hazina Bandari kukuwa . Ameongeza kuwa uboreshwaji wa reli hiyo yenye Umri wa miaka 50 utawesha Uchumi wa Tanzania na Zambia.kukuwa  ,, Wazo lauboreshaji wa reli ya Tazara kwa kiwango cha Kimataifa SGR liibuliwa na Rais wa ...

MACHUMU, ANG'ATUKA TEF, MGONGANO WA MASLAHI WA WADHIFA NDIO CHANZO.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                  DAR ES SALAAM MKURUGENZI wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Bakari Machumu amejijuzulu nafasi ya makamu mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) kwa kile alichodai kwa nafasi yake mpya anaona kutakuwa na mgongano wa masilahi na wadhifa huo. Machumu ambaye hivi karibuni ameteuliwa na Rais Dtk.Samia Suluhu Hassan kuwa mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu amekabidhi barua ya kujiuzulu kwake kwa Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile, leo  Novemba 26, 2025 alipokutana na wahariri kwenye kikao cha ndani, Ikulu jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa TEF Deodatus  Balile amepokea baruahi hiyo na kukubali kujiuzulu kwa Machumu na kuwa Kamati ya Utendaji ya TEF itakutana baadaye leo kujadili suala hilo.

WAZIRI MKUU DKT.NCHEMBA :AKEMEA WATUMISHI WAZEMBE, WALA RUSHWA ATOA MAELEKEZO.

Image
 Na Mwandishi wetu, DmNewsonline               DAR ES SALAAM  WAZIRI Mkuu, wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amewaeleza watanzania kuwa Serikali haitokuwa na mzaha na Watumishi wa Wazembe, Wavivu na Wala rushwa na kwamba ikithibitika Mtumishi anafanya makosa hayo na anakwamisha utendaji asiishie kuhamishwa bali afukuzwe kazi kabisa. Waziri mkuu Dkt Nchemba ametoa kauli hiyo leo Novemba 25,2025 jijini Dar es salaam wakati akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari, pamoja na Waandishi wa habari.ambapo amesema.  “kuhusu  nidhamu kazini hatutokuwa na mzaha nalo, uadilifu hatutokuwa na mzaha nao, bila nidhamu na uadilifu hatutotimiza malengo yaliyopo kwenye dira na Ilani, na nimewaelekeza Watendaji wa Serikali wasiwe na mzaha kwenye hili, na wale Wazembe, Wavivu, Wadokozi, Wala rushwa tutashughulika nao”amesema Dkt Nchemba  “Nimeelekeza Mtumishi Mzembe na Mla rushwa asihamishwe kituo Cha kazi aki...

WAZIRI WA KAZI UWEKEZAJI ZANZIBAR ATOA NENO TUZO ZA WAKUU NA WATENDAJI WA MAKAMPUNI.

Image
  Na Mwandishi,DmNewsonline WAZIRI wa Kazi na Uwekezaji Zanzibar, Shariff Ali Shariff (katikati),  amesema tuzo za wakuu na Watendaji wa Makampuni 100 Bora Kuvutia Uwekezaji na kukuza uchumi wa Tanzania. Waziri Shariff ameyasema hayo wakati akishiriki hafla ya utoaji tuzo hizo zilizofanyika  Novemba 21 ,2025 katika ukumbi wa The Super Dome Masaki jijini  Dar es salaam.