Posts

Showing posts from April, 2025

TLP KINAWATA WANACHAMA WENYE SIFA KUJITOKEZA KWA WINGI KUWANIA NAFASI ZA UONGOZI

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline ‎ ‎.           DAR ES SALAAM  ‎ ‎CHAMA cha Tanzania Labour Party(TLP) kinapenda kuwataarifu na kuwatangazia wanachama wote pamoja na wananchi na wapiga kura kuwa kimeanza kutoa fomu za  mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Ubunge na Udiwani kuanzia Aprili 25,2025. ‎ ‎Akizungumza na mwandishi wa habari wa DmNewsOnline kwa mahojiano maalum Ofisi kwake  leo Aprili 30,2025  Jijini Dar es Salaam Mwenyekiti wa TLP Taifa,Richard Lyimo amesema kwamba fomu za Urais zinapatikana Makao  Makuu ya Chama Dar es Salaam na Ofisi ndogo za Zanzibar na zoezi la kuchukua fomu lilianza Aprili 25,2025 na mwisho ni Mei 15,2025 kwa wagombea wa Urais. ‎ ‎Aidha,Mwenyekiti Lyimo amesema kuwa fomu za Ubunge na Udiwani zinapatikana kwenye ofisi zetu za Mikoa,Wilaya na Majimbo kwa nchi nzima kwa wenyeviti wa Mikoa,Wilaya,Majimbo na Makatibu na zimeanza kutolewa Aprili 30,2025 hadi...

MBUNGE KOKA ATOBOA SIRI YA MAFANIKIO UTEKELEZAJI WA ILANI MWAKA 2020/2025

Image
Na Victor Masangu,DmNewsOnline,              KIBAHA MBUNGE  wa Jimbo la Kibaha Mjini Mhe.Sylvestry Koka amesema kwamba katika kipindi cha miaka mitano kwa mwaka 2020/2025 ameweza kuleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo ambayo yametokana na juhudi zake binafsi pamoja na fedha ambazo zimetolewa na  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Koka ameyabainisha  hayo wakati wa mkutano mkuu maalumu wa Jimbo la Kibaha mjini wa utekelezaji wa ilani ya chama kwa kipindi cha miaka mitano kwa mwaka wa 2020 hadi 2025 katika nyanja mbali mbali. Koka amesema kwamba  kitendo cha kuwa na Rais msikivu kimekuwa chachu ya maendeleo katika Jimbo la Kibaha mjini ambapo kero katika sekta mbalimbali zimetatuliwa na hivyo kuwafanya wabunge kumsaidia kwa urahisi utekelezaji wa ilani ya Chama. "Raisi wetu ni mama msikivu anapoelezwa shida za wananchi hachelewi tutoa maelekezo ya utatuzi wa haraka kwa maendeleo yaliyopatikana kwenye Jimbo letu tuna kila sababu ya kumpa ...

ULENGE ATOA VIFAA VYA UJENZI NYUMBA ZA MAKATIBU UWT KOROGWE

Image
Na Yusuph Mussa,DmNewsonline             Korogwe MBUNGE  wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga Mhandisi Mwanaisha Ulenge ametoa msaada wa vifaa vyenye thamani ya sh. milioni 5,320,000 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa nyumba ya Katibu wa UWT Wilaya ya Korogwe Vijijini na Katibu wa UWT Wilaya ya Korogwe Mjini.  Kwa nyumba ya Katibu wa UWT Korogwe  Vijijini ametoa mifuko 100 ya Saruji yenye thamani ya sh. milioni 1.7. nondo 35 zenye thamani ya sh. 770,000  tripu tatu  za mchanga zenye thamani ya sh. 270,000, na usafiri wa saruji hadi eneo la mradi (Site) sh. 480,000, hivyo jumla kuwa sh 3,120,000. Wakati kwa nyumba ya Korogwe Mjini ametoa mifuko 100 ya Saruji ya sh. milioni 1.7 na nondo 25 zenye thamani ya sh. 500,000 jumla kuwa sh. milioni 2.2. Ametoa vifaa hivyo alipotembelea na kuona ujenzi wa nyumba ya Katibu huyo inayojengwa kwenye Makao Makuu mapya ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, Kijiji cha Makuyuni, ambapo alikuta wameanza ujenzi kwa ...

KOROGWE TC WAENDELEA KUTOA ELIMU MALIPO YA TASAF

Image
Na Yusuph Mussa,DmNewsonline             Korogwe MFUKO wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) Halmashauri ya Mji Korogwe mkoani Tanga umeendelea kupata mafanikio kwa kuweza kuwaelimisha wanufaika wa Mpango wa Kunusuru Kaya za Walengwa kuwa wanahakikisha wanaendelea kupata malipo yao kwa njia ya simu ama benki. Akizungumza Aprili 29, 2025 na mwandishi wa habari hizi ambapo zoezi la malipo linafanyika kwa siku mbili, Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji Korogwe, Rehema Letara, amesema idadi ya wanaopokea kwa njia ya fedha taslimu inazidi kupungua. Letara alisema malengo ya TASAF ni kuona walengwa wote wanalipwa kwa njia ya simu au benki, hiyo itarahisisha malipo hayo, lakini pia ni salama na rahisi, tofauti na kutumia fedha taslimu, na wamekuwa wanatumia Benki ya NMB na CRDB kukamilisha zoezi hilo. "Tunataka walengwa wote waweze kuwa na simu kwa ajili ya malipo. Lakini hata kama mtu ana akaunti ya benki hiyo itakuwa nzuri zaidi. Katika kufanikisha hilo, tunazunguka na ...

MABONDIA WAPIMANA UWEZO KUELEKEA. KNOCK OUT YA MAMA MEI 24,2025. ‎

Image
‎ Na Mwandishi wetuDmNewsOnline ‎               DAR ES SALAAM  ‎ ‎MSIMU wa nne wa Knock Out ya Mama unatarajiwa kufanyika Mei 24,2025 Jijini Dar es Salaam  ,hivyo mabondia mbalimbali wamekuta kupimana uwezo kwa kufanya mazoezi kwa lengo la kujifunza na kujiimarisha pambano hilo lililopewa jina sparring  lilihusisha mabondia mbalimbali ndani na nje ya nchi. ‎ ‎Pambano hilo la Sparring limefanyika Aprili 26,2025  lilofanyika    katika gym ya Mbezi Msumi  ya Kampuni ya Mafia Boxing eneo la msitu wa  Mwabepande nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam ambapo mabondia walipanda ulingo kwa kupima . ‎ ‎Akizungumza wakati wa zoezi hilo la sparring Kocha wa Gym ya Mafia Boxing Hamfrey Mohamed Said alisema kuwa hatua hii ni sehemu ya maandalizi kuelekea awamu ya nne ya mchezo wa Knocking Out ya Mama itakayochezwa hivi karibuni. ‎ ‎Kocha Said amesema  sparring hii ni kwa ajili ya kujua kwamba  yale mazoezi ambayo tumew...

MWENYEKITI MLALE KINYAMWEZI ATANGAZA NEEMA YA MIKOPO KWA WANANCHI WAKE.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                 DAR ES SALAAM  UONGOZI wa Serikali ya Mtaa wa kinyamwezi uliopo kata ya Pugu Wilayani ilala  chini ya Mwenyekiti wake Fahad Mlale(Bilionea) umetangaza Neema ya kuwapatia mikopo wananchi wake na hiyo ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni za uchaguzi wa Serikali za mitaa . Akizungumza katika mkutano wa Kwanza wa wananchi tangu kuchaguliwa kuwa kiongozi wa mtaa huo Mwenyekiti Mlale kwaza aliweza kuwashukuru wananchi hao kwa kuweza kumwamini na kuchagua kuwa kiongozi wao na pili amewaeleza wananchi hao kuwa kazi iliyopo mbele Yao ni kuujenga mtaa huo. Mkutano huo ambao umefanyika Machi 25 ,2025 katika ofisi za Serikali hiyo mtaa mwenyekiti pamoja na mambo mengine amewaeleza wananchi wake kuwa wakati akijinadi ili kupata ridhaa ya kuwa mwenyekiti alihaidi wakimchagua basi atahakikisha anatoa mikopo kwa makundi mbalimbali hivyo basi kuazia mei 18 mwaka huu ataaza kutoa mikopo hi...

TABORA YAONGOZA KIWANGO CHA MAAMBUKIZI YA MALARIA KWA ASILIMIA 23.

Image
Na Deborah Lemmubi,DmNewsonline                DODOMA  WAZIRI wa Afya Mhe Jenista Mhagama amesema kuwa Takwimu zinaonesha kuwa Mkoa wa Tabora unaongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ya Malaria kwa asilimia 23,huku Takwimu zikionesha kiwango cha Nchi kupungua kwa asilimia 45 kutoka asilimia 14.8 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 8.1 mwaka 2022. Waziri Mhagama amesema hayo Jijini Dodoma Aprili 25,2025 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari akitoa Taarifa ya Maambukizi hayo Kitaifa katika siku ya Maadhimisho ya Malaria Duniani inayoongozwa na kauli mbiu inayosema "Malaria Inatikomezwa na sisi: Wekeza Chukua Hatua -Ziro Malaria Inaanza na Mimi". Na kusema kuwa pamoja na kuwepo kwa Mikoa yenye maambukizi ya juu lakini pia ipo Mikoa yenye kiwango cha chini cha Maambukizi ya Malaria ya chini ya asilimia moja ikiwemo Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Dodoma, Songwe, Mwanza, Dar Es Salaam,Iringa na Singida. "Takwimu hapa nchini kwetu zinaon...

WANANCHi WAMETAKIWA KUTEMBELEA MAKUMBUSHO YA TAIFA ‎

Image
‎ Na  Mwandishi wetu,DmMewsOnline ‎ ‎         DAR ES SALAAM  ‎ ‎ ‎‎MHIFADHI Historia Makumbusho ya Taifa, Shomari Rajabu Shomari amewata wananchi  kutembelea makumbusho ya Taifa  kwani  ni sehemu sahihi ya kujifunza na kujione historiambalimbali. ‎ ‎Hayo ameyabainisha leo Aprili 25,2025 Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara maalum ya Maafisa Utamaduni na Maafisa Maendeleo ya Michezo. ‎ ‎"Makumbusho ni sehemu ambayo wanapokea wageni mbalimbali  na taasisi  ambapo Leo tumepokea maafisa utamaduni toka mikoa tofauti tofauti wamekuja kujifunza jinsi makumbusho yanavyohifadhi historia yeti pamoja na utamaduni",amesema ‎ ‎Aidha ,amesema kwamba mwamko wa watu kuja kujifunza kwani huwa tunaandaa programu mbalimbali kwa ajili ya kujifunza. ‎ ‎ ‎Pia amewakaribisha watanzania kutembelea makumbusho hasa siku ya tarehe 26,Aprili 2025 kwa lengo la kujifunza na  na kuelimika zaidi jinsi waasisi wetu waliopigania Muungano wetu na kuona ule ...

KATIBU WA CHADEMA NYASA AHAMIA CCM.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                      NYASA ALIYEKUWA Katibu wa Chama cha Democrasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya Nyasa Bw. Jacob Benworth Kunani tarehe 25.04.2025 amejiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)  katika Hafla fupi ya kumpokea iliyofanyika katika Ofisi za Umoja wa Vijana UV-CCM Wilaya ya Nyasa. Akikabidhi Kadi ya CHADEMA Na kupokea Kadi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bw. Kunani amesema anayofuraha kubwa kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kupokelewa na Viongozi wa UV-CCM Wilaya ya Nyasa na kusema kuwa   amepata amani ya roho, kwa kuwa Chama cha Mapinduzi ni chama imara kinachoendeshwa kwa misingi ya amani na Utulivu NA  Kiko kwa ajili ya kujenga Taifa na kuleta Maendeleo ndani na nje ya Tanzania. Ameongeza kuwa amejikuta ametoka kifungoni na sasa yuko huru, hata hivyo ameahidi kuwa atashirikiana vema na wanachama wa CCM.  Mgeni Rasmi katika Hafla hiyo ni Komred Clavian Matembo mweny...

WATANZANIA NA WANAJUMUIYA AFRIKA MASHARIKI WAHIMIZWA KUDUMISHA AMANI

Image
Mwandishi wetu,DmNewsonline                  DAR ES SALAAM WATANZANIA na wanajumuiya ya Afrika Mashariki wametakiwa kuendelea kudumisha amani na hasa kipindi hiki ambacho Taifa la Tanzania linaelekea katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu. Kauli hiyo imetolewa na  Mchungaji Patrick  Muthee kutoka nchini Kenya ambao wapo nchini Tanzania kwa mwaliko  wa Kwaya ya Gethsemane Group Kinondoni (GGK) kutokea Kanisa  la Wadventista Wasabato Kinondoni Jijini Dar es Salaam  pamoja na uongozi wa kanisa  ambapo wameandaa Wiki ya maombi yakiwemo ya kuliombea Taifa la Tanzania amani,upendo na mshikamano. “Tumekuja nchini Tanzania kuungana na ndugu zetu wa Kwaya ya Gethsemane pamoja na Kanisa Group Kinondoni (GGK)ambapo wameandaa wiki ya maombi mbalimbali ya kuliombea Taifa na kwa wakati huu kuomba amani,Umoja na mshikamano ni kipaumbele chetu kwani tunatambua Watanzania watakuwa na uchaguzi Mkuu mwaka huu.H...