Posts

Showing posts from March, 2024

MAKONDA RC MPYA ARUSHA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline  ALIYEKUWA Katibu wa NEC Itikadi Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi CCM Taifa Paul Makonda ameteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Arusha . Makonda anachukua nafasi ya John Mongella ambaye atapangiwa kazi nyingine Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa usiku na Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu. Paul Makonda aliwahi kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kabla ya kutimkia kwenye ubunge katika Jimbo la kigamboni katika uchaguzi mkuu uliofanyika 2020. Baada ya kushindwa uchaguzi huo na  aliyakuwa Mbunge wa Jimbo hilo Faustine Ndugulile kufanikiwa kutetea Jimbo hilo ,makonda alikuwa nje ya Serikali Kwa muda mrefu kabla ya mapema mwaka huu kuteuliwa na Chama chake kuwa Katibu wa Nec Itikadi ,Uenezi na Mafunzo na Sasa ni mkuu wa mkoa mpya wa Arusha.

OLE-SENDEKA AFYATULIWA RISASI NNE NA WATU WASIOJULIKANA

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline. Mbunge wa Simanjiro Mkoani Manyara, Christopher Ole-Sendeka amefyatuliwa risasi zisizopungua nne na Watu wasiojulikana akiwa ndani ya gari lake safarini pamoja na Dereva wake majira ya saa moja leo usiku na kisha watu hao kukimbia muda mfupi baada ya Mbunge huyo kuanza kupiga risasi juu kuwatishia. " “Ni kweli nimeshambuliwa kwa risasi majira ya saa moja kasoro katika Wilaya ya Kiteto kati ya Kijiji cha Ngabolo na Ndedo, kulikuwa na gari ambayo ilikuwa inanifuatilia kwa nyuma tukawapisha kidogo kama tunataka kuwapisha wapite kulia walipofika usawa wetu wakaanza kumimina risasi kwa Dereva "

FT : SIMBA 0-1 AL AHLY

Image
Simba yapoteza nyumbani kwa mara ya kwanza dhidi  ya Al Ahly Kwa bao 1-0

KATIBU MKUU WA CCM DKT. NCHIMBI AFIKA MSIBANI KWA MKE WA GACHUMA,TARIME NA KUTOA POLE.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline TARIME KATIBU  Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amewasili wilayani Tarime, Mkoa wa Mara, kushiriki mazishi ya Askofu wa Kanisa la New Life Gospel Community Church (NLGCC), Jimbo la Mara Kaskazini, Francisca Mwita Gachuma. Francisca ni mke wa wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Christopher Mwita Gachuma  Dkt .Nchimbi baada ya kuwasili msibani nyumbani kwa marehemu Mtaa wa Bomani, Tarime Mjini, leo Ijumaa, Machi 29, 2024, amepokelewa na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi CCM. Katibu Balozo Dkt Nchimbi ametoa pole Kwa  wafiwa, wakiongozwa na Familia ya Mzee Gachuma, pamoja na kushiriki ratiba ya awali ya msiba, kabla ya mazishi yatakayofanyika Machi 30, 2024, huko Komaswa,  Mjini Tarime

MIAKA 3 YA RAIS SAMIA, TRA TABORA YAPATA MAFANIKIO MAKUBWA

Image
Na Allan Vicent,DmNewsOnline TABORA MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoani Tabora inajivunia kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka 3 ya uongozi wa Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan. Akizungumza na Ofisini kwake Machi 28,2024 Meneja wa Mamlaka hiyo Mkoani hapa Fredrick Kanyilili amesema kuwa kasi na weledi wa Rais Samia vimekuwa kichocheo cha utendaji mzuri kwa Watumishi wa taasisi hiyo. Amesema kuwa katika kipindi cha miaka 3 tangu aingie madarakani, Mamlaka hiyo imefanikiwa kuwa na Ofisi katika Wilaya zote 7 za Mkoa huo huku Wilaya ya Uyui ikihudumiwa na Ofisi ya Tabora Manispaa.  Amefafanua kuwa mbali na kuwa na Ofisi katika Wilaya hizo jengo la Ofisi za TRA Mkoa nalo linafanyiwa ukarabati mkubwa ili kuwa na mwonekano bora zaidi, jengo hili litakuwa kichocheo kikubwa cha kasi ya utendaji wa Mamlaka hiyo. Mbali na mafanikio hayo, Kanyilili amebainisha kuwa kasi ya ukusanyaji mapato imekuwa ikiongezeka kila mwaka hivyo kuw...

PUMA ENERGY TANZANIA YAFUTURISHA ,MKURUGENZI WAKE ATOA NENO.

Image
 Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline DAR ES  SALAAM KAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo huku ikitumia nafasi hiyo kuwaomba Watanzania kuendelea kuwaunga mkono sambamba na kuhimiza  kudumisha amani. Hafla ya Iftar iliyoandaliwa na Kampuni hiyo ikiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wake Fatma Abdallah imefanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa wadau mbalimbali wakiwemo wakuu wa taasisi za umma na binafsi pamoja na wateja wa kutoka maeneo mbalimbali nchini. Mgeni rasmi katika Iftar hiyo alikuwa Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam Alhad Walid aliyewakilishwa na Sheikh wa Wilaya ya Temeke ... Akizungumza wakati wa Iftar hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo Dk Selemani Majige ametumia nafasi hiyo kueleza kuwa ni vema kila Mtanzania kwa nafasi yake kuendelea kuliombea Taifa sambamba na kumuunga mkono Rais Dk.Samia Suluhu Hassan. "Tunafahamu kwa sasa tunaendelea na Mfungo wa Ramadhan pamoja na Kwaresi...

UWT WAKUTANA NA WADAU WA MAENDELEO,WAKIWEMO WAFANYABIASHARA KUTOKA CHINA.

Image
Na Mwandishi Wetu,DmNewsOnline DAR ES SALAAM  KATIBU mkuu wa Umoja  Wanawake Tanzania (UWT)  Jokate Mwegelo amesema kuwa katika kumuunga mkono Rais Dkt  Samia Suluhu Hassan, umoja huo umejipanga kwa uwekezaji katika sekta ya nishati safi ya kupikia kwa lengo la kumtua mama  kuni kichwani. Amesema katika kufanikisha hatua hiyo,  Leo Machi 28 ,2024 katika ofisi ndago za Makao makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es salaamwameweza kukutana  na wadau wa maendeleo kutoka Chama cha Kikomunisti cha China (CCP) pamoja na wafanyabiashara ambapo wamejadiliana mambo mbalimbali..  Ameongeza kuwa katika nazungumzia yao wameweza kuzungumza mambo mengi mbalimbali lakini Moja ya mambo ambayo wamezungumza na wao wapo tayari kushirikiana nao ni uwekezaji wa upande wa Nishati mbadala itakayoweza kumtua mwanamke mzigo wa Kuni kichwani kwae.  Jokate amesema wawekezaji hao ambao ujio wao umeratibiwa na Kampuni Canopus Energy Solution, wameonyesha utayari wa kushirikian...

VIJIJI 14 ,SIMANJIRO,KITETO KUNUFAIKA NA MRADI MPYA TOKA UCRT

Image
Na Mary Margwe,DmNewsOnline SIMANJIRO  JUMLA ya Vijiji  14 , kati ya hivyo Vijiji 9 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro na  Vijiji 5 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto vinatarajia kunufaika na mradi mpya kutoka Shirika la UCRT Mkoani Manyara, Hali itakayosaidia kuondokana na Migogoro mingi ya ardhi. Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mratibu wa Shirika lisilo la Kiserikali la UJamaa Community Resource Team ( UCRT ) Edward Loure wakati wa kuutambulisha Mradi mpya wa " Uhifadhi Jumuishi wa Mazingira na kuboresha maisha ya Jamii katika Halmashauri hizo mbili za Mkoa wa Manyara. Mradi huo umezinduliwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Dkt.Suleiman Serera katika Mji Mdogo wa Orkesument mbele ya Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mh.Baraka Kanunga, Mbunge wa Jimbo hilo Mh. Christopher Ole Sendeka, pamoja na madiwani, Maafisa Tarafa, watendaji  wa Kata na Vijiji pamoja, viongozi wengine pamoja nawataalam kutoka idara mbalimbali. Aidha Loure amesema Shirika la UCRT linashughulik...

WAFANYABIASHRA NA WAWEKEZAJI KUTOKA CHINA KUWEKEZA NCHINI, WAMWAGA MABILIONI.

Image
Na Said Mwishehe, DmNewsOnline  DAR ES SALAAM UJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou nchini China umeeleza kwamba umeridhia kufanya uwekezaji wa zaidi ya dola za Marekani milioni 312 sawa na zaidi ya Sh bilioni 800 katika maeneo ya nishati,afya,ujenzi, kilimo na vifaa vya uchakataji. Pia, ujumbe huo umeonesha nia kushirikiana na kutafuta wawekezaji katika maeneo takribani nane ambayo ni viwanda vya kujenga viwanda vya kuzalisha na kufunga pawatila, kuzalisha vifaa vya trekta, kuzalisha majenereta na pampu za maji, kuzalisha vifaa tiba, viwanda vya bidhaa za umeme na paneli za kuhifadhi baridi. Akizungumza Dar es Salaam leo Machi 27,2024 wakati wa kikao kati ya ujumbe huo na menejimenti ya Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Mhandisi Anna Nyangasi kutoka kampuni ya Canopus Energy Solutions, amesema ujumbe huo wa watu 11 wakiwemo wafanyabiashara,Wawakilishi kutoka serikalini pamoja na ujumbe wa Chama cha Kikomunisti cha China(CPC)umewasili nchini b...

BITEKO AMWAGIZA KATIBU MKUU KUMTENGUA MENEJA KAMPUNI

Image
Na  Benny Kingson,DmNewsonline TABORA. NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt.Dotto Biteko amemwagiza Katibu Mkuu wizara ya Nishati kumtengua Meneja Mkuu wa kampuni ya ujenzi wa miundombinu,usafirishaji na usambazi wa shirika la umeme nchini ETDCO Mhandisi Mohamed Abdallah kwa kushindwa kusimamia vema majukumu yake. Dkt.Biteko ametoa agizo hilo Leo Machi 27 ,2024  wakati akikagua kituo cha kupokea,kupoozea na kusambazia umeme kilichopo Mtaa wa Uhuru,Kata ya Vumilia wilaya ya Urambo Mkoani Tabora . Dkt.Biteko  amesema Meneja huyo ameshindwa kuhudhuria hafla hiyo na kumtuma mwakilishi huku akitambua kuwa amefanya uzembe katika utekelezaji wa ujenzi wa kituo hicho. Amesema kuwa kampuni hiyo inayoongozwa na Meneja huyo imepeleka  nguzo za umeme katika mradi wa ujenzi wa kituo hicho kwa kufikisha asilimia 10 tu hadi sasa ambapo umefikisha aslimia 84 ya utekelezaji mradi huo na kwamba ameonyesha dharau na kufanyakazi kwa mazoea. “Amemtuma mwakilishi huyo  Dismas M...

TMDA KANDA YA MAGHARIBI YAFANYA MSAKO WA KAMATA KAMATA DAWA HATARISHI.

Image
Na Benny Kingson,DmNewsOnline TABORA. MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba kanda ya Magharibi TDMA  Tabora imekamata dawa ya kuongeza nguvu za kiume aina ya Vega ambayo haijasajiliwa.  Pia mamlaka hiyo  imekamata  Sigara dawa kutoka India ambazo ubora wake haujulikani na zimeekwisha muda wa matumizi Hayo yamebainishwa na Meneja wa TMDA Kanda hiyo Dkt .Christopher Migoha Machi 26,2024 katika mahojiano maalumu  ofisini kwake na Mwandishi wa Habari hizi  ambapo pia alitoa taarifa ya utendaji kazi kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai mwaka 2023 hadi Machi 2024. Amesema  katika kipindi hicho wameweza kukamata madawa  yenye thamani ya sh.milioni 3,972,017. Dkt Migoha amesema  kati ya madawa hayo walikamata sigara dawa zenye thamani kubwa ya fedha ambapo miongoni mwa madawa hayo ni  kutoka nchini India na kuongeza kuwa matumizi ya madawa hayo yana madhara makubwa kwa afya kwa kuwa yanaongeza msukumo wa damu mwilini. “Madawa haya ni hatari kwa afya za j...

LATRA WAPONGEZWA KUBORESHA HUDUMA ZA USAFIRI TABORA

Image
Na Allan Vicent,DmNewsOnline  TABORA WAKAZI Mkoani Tabora wameipongeza Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kwa kuboresha huduma za usafiri barabarani na kupunguza kero na manyanyaso waliyokuwa wanapata abiria kwa kiasi kikubwa. Pongezi hizo zimetolewa jana na baadhi ya wasafiri na wasafirishaji Mkoani hapa walipokuwa wakiongea na mwaandishi wa gazeti hili kuhusu mafanikio ya miaka 3 ya Rais wa awamu ya 6 Dkt Samia Suluhu Hassan. John Johasy mkazi wa Isevya katika Halmashauri ya Manispaa Tabora alisema kuwa katika miaka 3 ya utawala wa Rais Samia huduma za usafiri barabarani zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa sana tofauti na hali ilivyokuwa huko nyuma. ‘Tunawashukuru sana LATRA, wametusaidia kudhibiti ulanguzi wa nauli uliokuwa unafanywa na baadhi ya wasafirishaji, mawakala na wapiga debe wenye tamaa ya kujipatia faida kwa kuumiza wananchi’, amesema.      Mmiliki wa vyombo vya usafiri Mkoani hapa, Said Juma Said maarufu kwa jina Yamelee alimpongeza Mkurugezi Mkuu ...