WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA BIDHAA ZA BATTERIES ZINAZOZALISHWA NCHINI.
DAR ES SALAAM.
KATIKA kuhakikisha Sekta ya Uwekezaji inakua kupia Sekta ya Viwanda, Kampuni ya Izzo Batteries imekuja kuwekeza Sekta ya Batteries za Magari na Mashine ilikuweza kuhakikisha Watanzania wananufaika na Bidhaa zinazozalishwa hapa Nchini.
Akizungumza Leo Mei,12 ,2026 Jijini Dar es Salaam Meneja wa IZO Batteries IZZO Mahange amesema kuwa Bidhaa za Batteries zinazozalishwa kwenye Kampuni hiyo zina dhamana ya miaka 10 ,Ambapo tayari Kampuni hiyo ina mawakala Takribani 150 Nchi nzima.
"Batteries zetu zinazozalishwa hapa nchini,tayari Kampuni yetu imezalisha Ajira takriban 50" Amesema Meneja Izzo BATTERIES IZZO Mahange.
Naye balozi wa Kampuni hiyo Dotto Magari amesema kuwa Bidhaa hiyo ya Bettries Izzo zinaubora kwenye Mashine pamoja Magari, sambamba na Bajaji .
"Hii ni fursa kwa Wawekezaji katika sekta ya Viwanda kuzalisha Bidhaa ya BATTERIES, badala ya kuagiza bidhaa hii kutoka China "Amesema Balozi wa Izzo Batteries Dotto Magari.
Magari Ameongeza kuwa lZO Batteries imekuja nasuluhisho kuokoa Vyombo vya Moto Nchini Tanzania.

Comments
Post a Comment