RC MAKONGORO AIBUKA MSHINDI KUSHUHUDIA KOMBE LA DUNIA NCHINi CANADA

 Na Angelina Mganga,DmNewsOnline

         DAR ES SALAAM 

MKUU wa Mkoa wa Rukwa ,Charles Makongoro Nyerere ametangazwa  kuwa mshindi kupitia  droo ya FIFA WORLD CUP 26 ,Fainali ndo Mpango naTemboCardVisa inayochezeshwa na Benki ya CRDB

Katika droo hiyo wamepatikana washindi watatu waliojinyakulia TV Janja Smart  za nchi 85 pamoja na king'amuzi.

Washindi  hao waliojinyakulia Tv  Janja ni Amina Kaswale Awadhi, Esther Dauson Kabakama na Lusekelo Michael Mwamwala.

Makongoro ameibuka  mshindi katika droo hiyo  pamoja na wenzake wawili  kwenda nchini Canada kushuhudia Fainali za Kombe la Dunia.

Akizungumza kwa njia ya simu na watangazaji wa droo hiyo Charles Makongoro Nyerere amewapongeza kwa kutoa huduma Bora kwa wateja wao na kuelezea furaha yake kwa kuwa miongoni mwa washindi waliopata fursa yakushuhudia  Fainali ya Kombe la Dunia.

Naye Meneja Mwandimizi Kitengo cha Kadi CRDB Benki,Karington Chahe  amesema washindi wote watasafarishwa ya kwenda na kurudi na benki hiyo na wale waliojinyakulia Tv Janja zitasafirisha kwa gharama za benki hiyo

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA TIBA ASILI TANZANIA WADAIWA SI HALALI NA UMEKOSA DIRA YA KUENDESHA VYAMA VYA WAGANGA WA TIBA ASILI

DKT. KIJAZI KUSIMAMIA MIRADI YA MAENDELEO JIMBO LA KOROGWE MJINI.