DC MSANDO ATOA MAAGIZO KWA TANESCO NA TARURA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline
DAR ES SALAAM
JESHI la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam limeungana na wazimamoto duniani kuadhimisha Siku hiyo katika maonesho yaliyofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam
Akizungumza katika Maadhimisho hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mkuu wa Wilaya ya Ubungo,Wakili Albert Msando ametoa maagizo kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO) pamoja na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini(TARURA) kuwa ujenzi wa miundombinu ya Barabara na wale wanaounganisha umeme kuwa makini ili inapotokea majanga ya moto iwe rahisi kuyadhibiti.
Amesema Zimamoto wanatakiwa kujiridhisha ubora wa vifaa vinavyotumika kuunganisha umeme kwenye maeneo ya biashara,masoko na maduka wahakikishe vifaa hivyo viko salama,kama haviko salama aliyeunganisha huduma hiyo achukuliwe hatua za kisheria.
Kwa upande wake Naibu Kamishna wa Jeshi la Zimamoti na Uokoaji Tanzania na Msemaji wa Jeshi hilo DCP Puyo Nzalayaimisi aimeishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi za Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kulipatia vifaa vya kisasa na magari ambayo yatarahisisha utendaji wa kazi ya uokoaji yanapotokea majanga.
"Jeshi hilo litaendelea kujitoa kwa hali na Mali na kwa moyo wa dhati kwa ajili yakuwahudumia wananchi",amesema 





Comments
Post a Comment