Posts

Showing posts from January, 2026

DIWANI MALILO ATOA MSAADA KWA WATOTO WASIOJIWEZA SHULE YA MSINGI BONYOKWA

Image
  Na Angelina Mganga,DmNewsOnline         Dar es Salaam  DIWANI wa Kata ya Bonyokwa  Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Mhe.Tumike Malilo ametoa msaada  wa sare za shule ,kalamu na daftari kwa watoto wasiojiweza katika shule ya msingi Bonyokwa Akizungumza na waandishi wa habari Leo Januari 29,2026 mara baada ya kukabidhi msaada huo  amesema kwamba ameamua kutoa msaada kwa watoto hao kuonyesha upendo na kujitoa kwa ajili ya jamii inayomzunguka katika  Kata hiyo. "Nimeona ni vema kuwasaidia watoto wasiojiweza kwa kuwapatia msaada wa sare za shule ili nao watambue kuwa tunawapenda na kuwathamini",amesema Mh.Tumike Aidha,amesema tunaendelea kusimamia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Afya,elimu na miundombinu ya Barabara.                   Sekta ya Elimu   Akizungumzia sekta ya elimu Diwani huyo amesema kwamba  katika Kata ya Bonyokwa Ina shule Mbili za msi...

SERIKALI IMEFANYA MAGEUZI MAKUBWA KWA VIJANA KATIKA UONGOZI WA RAIS SAMIA

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline                Dar es Salaam  MRATIBU wa Taasisi ya Together for Samia Gulatone Masiga amesema kwamba katika kipindi cha miaka mitano ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan serikali imefanya mageuzi makubwa ya kuwanufaisha vijana wa Kitanzania katika sekta za ajira,ujuzi na elimu pamojana uwezeshaji wa kiuchumi. Akizungumza na waandishi wa habari Leo Januari 26,2026 Jijini Dar es Salaam wakati wa kumbukizi ya maadhimisho ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais Samia yaliyoandaliwa na taasisi ya Together for Samia,amesema  Rais ametoa fursa nyingi kwa   vijana zenye mafanikio. Aidha amesema kwamba Rais Samia amewekeza kwa vijana katika kizazi cha Sasa na kijacho hasa katika ujenzi wa vyuo vya ufundi na ujuzi katika wilaya zaidi 62 nchini jambo lilopelekea vijana kupata fursa ya kujiajiiri na kushinda katika soko la ajira. Aliendelea kwamba Rais Samia amewekeza kwa vitendo,kwani vyuo ni chachu ya kuwaapatia vi...

PROFESA LIPUMBA, AWATAKA WATANZANIA KUTOGAWANYIKA.

Image
  Timothy Marko,DmNewsOnline               DAR ES SALAAM.   MWENYEKITI wa  Chama Cha Civil United Front (CUF) Professa Ibrahim Lipumba amewataka Watanzania  kutorubuniwa kwa Migawanyiko inayochochewa na Baadhi ya Wanasiasa,Nakusisitiza kuwa Taifa la Tanzania  litajengwa kwa Misingi ya Amani na Umoja nasio Misingi ya Migawanyiko. Akizungumza Katika Maadhimisho ya kumbukukizi ya Machafuko yaliyotokea 27 January 2001 Zanzibar Ambapo zaidi wafuasi 71 wachama hicho waliopoteza Maisha, Profesa Ibrahim Lipumba amesema kuwa nivyema kukapatikana Mfumo mzuri wa Uchaguzi  unaozingatia haki na Umoja wa kitaifa. "SsiI ni Chama tunachosimamia misingi ya Umoja wa kitaifa,tusikubali kugawanyika kwa misingi ya uzanzibari na Utanganyika" Amesema Mwenyekiti wa Chama Cha CUF Professa Ibrahim Lipumba. Professa Lipumba Ameongeza kuwa nivyema kutatua Matatizo yetu kwa Misingi ya Amani. "Watu wapate kura nyingi kwa misingi ya Uhuru na haki" ...

WATENDAJI WA MIKOA WATAKIWA KUJITAFAKARI, KUBAINI MAENEO YA MABORESHO

Image
Na mwandishi wetu,DmNewsOnline  Dodoma Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM- TAMISEMI) Mhe. Sospeter Mtwale amewataka watendaji wa Sekretarieti za Mikoa kutafakari na kutathmini maeneo ya utendaji kazi yanayohitaji kufanyiwa maboresho pamoja na kujenga timu za utendaji kazi zenye kuleta tija. Mhe. Mtwale ametoa rai hiyo leo Januari 26, 2026 katika ukumbi wa mikutano wa St Gasper Dodoma, wakati akifungua mafunzo ya uongozi kwa makatibu tawala wa mikoa sehemu ya elimu na mafunzo ya ufundi, wakuu wa vitengo vya uhasibu na fedha, ukaguzi wa ndani na maendeleo ya jamii kutoka katika sekretarieti za mikoa yote 26 ya Tanzania Bara. Amesema TAMISEMI imeona umuhimu wa kutoa mafunzo ya uongozi kwa watendaji hao ili kuongeza ufanisi na tija katika sekretarieti za mikoa na kuwa awamu hii inahitimisha mafunzo kwa watendaji wa sekretarieti hizo ambapo tayari mafunzo yameshatolewa kwa wakuu na sehemu na vitengo vingine. "Sitarajii ushiriki hafifu, mat...

RC BALOZI BATILDA BURIAN AFUNGA MAADHIMISHO YA WIKI YA HUDUMA YA FEDHA KITAIFA

Image
Rc Tanga, Balozi Batilda Burian. Leo Januari 26,2025, amefunga Maadhimisho ya wiki huduma ya fedha Kitaifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya usagara Mkoani Tanga Kabla ya kufunga alitembelea mabanda yalikuwa kwenye viwanja hivyo ikiwemo Banda la Benki ya  NMB na akawapa hongera kwa kazi kubwa wanayoifanya

DKT. HOMERA AWEKA MSINGI WA MOTISHA KWA WATUMISHI NAMTUMBO

Image
- Ataf­siri maono ya Rais Samia kwa vitendo akitoa magodoro 222 -  asema motisha ni nguzo ya huduma bora kwa wananchi Na. Mwandishi wetu,DmNewsOnline                      Namtumbo WAZIRI wa Katiba na Sheria na Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Dkt. Juma Zuberi Homera, ameendelea kutafsiri kwa vitendo maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ya kuwajengea motisha na mazingira bora ya kazi watumishi wapya, baada ya kukabidhi magodoro 222 kwa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo, hatua inayolenga kuinua morali na kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi. Magodoro hayo yamegawanywa kwa mpangilio mahsusi ambapo 202 kwa watumishi walioajiriwa tayari, 13 kwa watumishi wanaotarajiwa kuajiriwa, na 7 kama akiba.  Makabidhiano yamefanyika tarehe 23 Januari 2026 katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo. Akizungumza mbele ya viongozi wa Serikali na Chama, Dkt. Homera amesema motisha kwa...

MWENYEKITI TUME HURU YA UCHAGUZI AWATAKA WARATIBU NA WASIMAMIZI WA UCHAGUZI KUZINGATIA SHERIA.

Image
    Na Eliasa Ally,DmNewsonline               IRINGA  MWENYEKITI  wa Tume huru ya taifa ya uchaguzi   Jaji  Jacob Mwambegele amewakumbusha wasimamizi na waratibu wa uchaguzi kuzingatia weredi Sheria na kanuni za uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha sita ibara ya kwanza na utendaji kazi kwa kuzingatia uzoefu wao bila kupendelea Jaji Mwambegele ameyabainisha hayo wakati wa ufunguzi  wa mafunzo kwa watendaji wa uchaguzi ngazi ya mkoa Jimbo na kata yanayofanyika mkoani Iringa kwa siku tatu katika ukumbi wa mkuu wa mkoa  wa Iringa Mafunzo hayo yanahusisha  waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya  jimbo na kata maafisa uchaguzi,maafisa ununuzi na uhasibu kwa lengo la kukumbushana masuala muhimu kuhusu usimamizi uratibu na uendeshaji mdogo wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika Jimbo la Peramiho na udiwani katika kata ya shiwinga. Pia amewasisitiza  kuheshimu viapo vyao kwa nafasi wal...

VIKUNDI 222 UYUI VYAWEZESHWA MIKOPO NAFUU YA BILIONI 1

Image
      Na Allan Kitwe,DmNewsonline                   TABORA  HALMASHAURI ya Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora imetoa mikopo nafuu isiyo na riba ya shilingi bilioni 1 kwa vikundi 222 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu wanaojishughulisha na biashara ndogo ndogo ili kuwainua kiuchumi. Akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi mfano wa hundi za mikopo hiyo jana, Afisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya hiyo Amoniche Mtweve amesema kuwa mikopo hiyo imetokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri. Ameongeza kuwa jumla ya wanachama 1,121 wanaounda vikundi hivyo wamenufaika na mikopo hiyo na kuwapa nguvu ya kuendeleza miradi yao ya biashara na uzalishaji mali katika maeneo yao. Naye Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Shabani Katalambula, amewataka wanufaika kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwezesha wananchi wengine kunufaika na mikopo hiyo katika awamu zijazo. Amefafanua lengo la mikopo hiyo kuwa ni kusaidia vijana, wana...

NAIBU WAZIRI LONDO ATAKA WAKALA WA VIPIMO KUSIMAMIA SHERIA ZA VIPIMO ILI KULINDA HAKI ZA MLAJI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsTz ‎Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Dennis Londo, ameitaka Wakala wa Vipimo nchini kuongeza uwajibikaji na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa sheria za vipimo ili kuwalinda walaji dhidi ya udanganyifu na kuhakikisha wanapata thamani halisi ya fedha zao. ‎Londo amesema usimamizi madhubuti wa vipimo ni msingi muhimu katika kujenga uchumi shindani, himilivu na jumuishi, sambamba na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 na 2050. ‎Ameyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi katika Ofisi za Wakala wa Vipimo Mkoa wa Pwani, ambapo amesisitiza kuwa Wizara ya Viwanda na Biashara imejipanga kuhakikisha kunakuwepo mazingira wezeshi ya biashara huku ikijenga imani kwa walaji katika huduma na bidhaa wanazopata. ‎Naibu Waziri ameongeza kuwa kutokuwepo kwa usimamizi sahihi wa vipimo kunawanyima walaji haki zao za msingi na kudhoofisha ushindani wa haki katika biashara, jambo linaloweza kuathiri ukuaji wa uchumi kwa ujumla. ‎Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mku...

PROF. SHEMDOE - TUMETEKELEZA VIZURI MKATABA WA LISHE 2024/25

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsTz Dodoma Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25 imeonesha mafanikio makubwa, ambapo rangi ya kijani imetawala katika viashiria vingi vya utekelezaji, ikiwa ni ishara ya kufanya vizuri kwa mikoa na halmashauri nchini. Hayo yamesemwa leo Januari 22,2026 jijini Dodoma na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, wakati akifungua mkutano wa tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe kwa mwaka wa fedha 2024/25. Prof. Shemdoe amesema Taifa limeendelea kupiga hatua kubwa katika kuboresha hali ya lishe kwa wananchi, hali inayochangia kuimarisha nguvu kazi yenye afya bora na kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa Taifa. “Nawashukuru Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Maafisa Watendaji wa Kata, Vijiji na Mitaa pamoja na viongozi na watendaji wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Mikoa na Halmashauri kwa kazi kubwa ya kusimamia, kuratibu na kutekeleza Mkataba wa Lishe,” ame...