Posts

Showing posts from December, 2025

WAUMINI KATOLIKI WAZIDI KUWAPINGA KITIMA, RUWA'ICHI ,WASEMA HOJA ZA SIASA ZACHOCHEA MGOGORO

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline               DAR ES SALAAM  UPINZANI wa waumini wa Kanisa Katoliki dhidi ya mwenendo wa baadhi ya viongozi wa juu wa kanisa, akiwemo Padri Dkt. Charles Kitima na Askofu Mkuu Ruwa’ichi, unaendelea kushika kasi, huku hoja za kimaadili, kisheria na kiteolojia zikiwekwa wazi hadharani. Kupitia tafakuri nzito ya dhamiri iliyotolewa na Mwalimu Ludovick Joseph, muumini wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania, waumini wameanza kujenga hoja ya pamoja kwamba Kanisa si mtu mmoja, si padri wala askofu, bali ni jumuiya ya waumini, na kwamba viongozi wa kanisa hawako juu ya Injili wala juu ya waumini. Katika tafakuri hiyo, waumini wanasema wazi kuwa kuhoji, kukosoa na kuomba uchunguzi dhidi ya kiongozi wa kanisa si uasi, si dhambi wala si chuki, bali ni haki ya kisheria inayotambuliwa ndani ya mfumo wa Kanisa Katoliki lenyewe. “Kanisa ni takatifu kwa sababu ya Kristo, lakini viongozi wake ni wanadamu wenye mipaka na wanaweza kuk...

WAWILI WAFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI TABORA

Image
              Na Allan Kitwe, DmNewsonline                    TABORA  WATU wawili wamepoteza maisha kwa kupigwa na radi wakiwa wamejikinga mvua kwenye kibaraza cha nyumba yao iliyoegemewa na mti katika Kijiji cha Songambele, Kata ya Uyowa, Wilayani Kaliua Mkoani hapa. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani hapa SACP Richard Abwao amethibitisha kutokea tukio hilo Desemba 27 mwaka huu na kuongeza kuwa mbali na waliopoteza maisha watu wengine wawili walijeruhiwa pia. Ametaja waliopoteza maisha kuwa ni Mwagala Marando (19) na Moses Lwega (20) wakulima, wakazi wa kijiji hicho na waliojeruhiwa ni Yohana Peter (18) na George Deusi (18), na wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye kituo cha afya. Kamanda Abwao  ametoa wito kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhari hasa katika kipindi hiki ambapo mvua zimeendelea kuongezeka na kuwataka wajikinge katika maeneo yaliyo salama ili kuepusha madhara yanayoweza kujito...

ASKOFU MATARO WA KANISA LA INJILI HASA YA YESU KRISTO AMEASA WATANZANIA KUENZI AMANI, UPENDO NA UMOJA WETU.

Image
 Mwandishi wetu,DmNewsonline              DAR ES SALAAM  ASKOFU  wa Kanisa la Injili Hasa  ya Yesu Kristo (Actual Gospel Of Jesus Christ Church), Mataro Kikoba amewaasa Watanzania kushirikiana kwa pamoja kulirejesha taifa la Tanzania katika misingi yake ya awali ya upendo, umoja na amani. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam,  waliofika kanisa hapo kushuhudia tendo la ndoa takatifu Askofu Mataro  pia alitumia mahubiri yake kutoa Ushauri kwa watanzania .  Askofu Mataro amesema nivema kukumbuka misingi  ambayokwa namna moja ama nyingine ilitikiswa hasa kutokana na vurugu zilizojitokeza Oktoba 29, mwaka huu. Amesema Watanzania hawana sababu ya kugawanyika kwa namna yoyote ile akidai kuwa taifa linapaswa kuwa moja na la mfano kote duniani. “Taifa pamoja na kuwa na watu wenye mitazamo tofauti tofauti halipaswi kugawanyika na kupoteza malengo yake, linatakiwa kuwa imara na kuendesha shughuli zake mit...

DIWANI AGUSWA NA KERO ZA WAJAWAZITO TABORA

Image
 Na Allan Kitwe,DmNewsonline              TABORA DIWANI wa Kata ya Chemchem katika halmashauri ya manispaa Tabora kupitia CCM, Bandola Salum Milambo ameanza mikakati ya kutatua kero wanazopata akinamama wajawazito na wagonjwa wengine katika kata yake.  Akizungumza na wanahabari jana ameeleza kuwa baada ya kuapishwa sasa ana kazi moja tu ya kuhakikisha kero zote zinazowakabili wapiga kura wake zinashughulikiwa ipasavyo na mamlaka husika. Amedokeza kuwa kwa kuanzia anaanza na kero ya wajawazito ambao wamekuwa wakilalamikia kutozwa gharama kubwa wanapoenda kuanza kliniki kwenye Kituo cha kutolea huduma za afya cha Town Kliniki, kilichoko hapa Chemchem. ‘Nimepanga kutembelea Kituo hiki (Zahanati ya Town Kliniki) ili kujionea hali ya utoaji huduma lakini pia kufuatilia malalamiko ambayo yametolewa na akinamama wajawazito ya kutozwa gharama kubwa ili wapate huduma za kliniki’, ameeleza. Amesema kuwa utaratibu wa wananchi kuchangia huduma za afya un...

SERIKALI YAWATAKA WANANCHI KUFUATILIA VITAMBULISHO NIDA KWAKUTUMIA SIMU ZA VIGANJANI.

Image
Timothy Marko DmNews Online            DAR ES SALAAM.  SERIKALI imewataka Wananchi kuweza kutumia simu za viganjani kwa kupiga namba 15274 ilikuweza kupata kwa urahisiVitambulisho vya Taifa. Akizungumza Leo Desemba 29,2025 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene amesema kuwa kwa kutumia Namba hiyo kutamuwezesha Mwananchi kupata taarifa za Vitambulisho hivyo na Majibu yake kwa Muda wa siku Tano. "Kwakutumia namba hii utapata taarifa ya kitambulisho chako kama kimeteng'enezwa,Nakusisitiza Vitambulisho Vilivyoharibika watavipata Febuary 2026" Amesema Simbachawene Ameongeza kuwa Serikali imepanga mkakati wa matumizi ya kitambulisho kimoja kwaajili ya Matumizi yahuduma za kiserikali. Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kutoa Ajira kwa maafisa wapya kupitia Mamlaka hiyo kwa Ngazi ya Wilaya na Kata. Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) James Kaji amesema kuwa Awali taasisi hiyo ilianzisha mfumo wa kupata Vi...

WAUMINI WA KANISA KATOLIKI WAPINGA KAULI ZILIZOTOLEWA NA ASKOFU RUWA'ICHI

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsonline             DAR ES SALAAM  WAUMINI wa Kanisa Katoliki,Mackdeo Shilinde na Gerald Abel  wanapinga hadharani kauli zilizotolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam,Jude Thaddaeus Ruwa'ichi wakati wa homilia ya Misa Takatifu ya Krismasi tarehe 25 Desemba 2025 wakisema mimbari imegeuzwa jukwaa la matusi,hukumu na vitisho badala ya Injili ya mapendo . Katika taarifa ya waumini hao wamesema maneno makali yaliyotamkwa  madhabauni katika homilia ya Misa ya Krismas ,Askofu Ruwa'ichi alitumia maneno mazito kama "lofa", "mpumbavu", "njaa njaa", "msaliti" na Ndumilakuwili", wakisema kauli hizo zinakiuka mafundisho ya Biblia. Waumini hao wamesema "Biblia inaonya wazi dhidi ya matumizi ya lugha ya matusi na hukumu huku wakinukuu maandiko Matakatifu"Msihukumu ,msije mkahukumiwa", (Mathayo 7:1) Katika msimamo wao,waumini hao wamesema mimbari imewekwa kwa ajili ya kuhubiri Neno la Mungu,kuimaris...

WAZEE TABORA WANENA MAZITO KWA RAIS SAMIA

Image
 Na Allan Kitwe,DmNewsonline                      TABORA  ZIKIWA zimebakia siku chache kumalizika mwaka 2025 na kuanza mwaka mpya wa 2026, wazee wa Mkoa wa Tabora wameeleza kuridhishwa na utendaji wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika awamu yake ya pili baada ya kuingia madarakani. Wameeleza kuwa weledi na ufanisi wa Kiongozi mzuri unapimwa kwa mambo makubwa matatu ambayo ni hali ya usalama wa nchi, kasi ya maendeleo na uchumi, mambo haya yamesimamiwa vizuri na nchi inapiga hatua kubwa. Mzee Elisha Daud Mponeja ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi wa Jadi katika halmashauri ya manispaa Tabora ameeleza kuwa Rais Samia amefanya kazi nzuri sana katika kipindi chake cha miaka minne na hata sasa anaendelea vizuri. Amefafanua kuwa baada ya kukabidhiwa nchi Machi 19, 2021 kutoka kwa mtangulizi wake aliyetangulia mbele za haki, Dkt John Pombe Magufuli, watanzania walishuhudia kasi kubwa ya utekekezaji miradi ya maendeleo kati...

ASKOFU MEIVUKIE ATAKA UPENDO, HAKI NA AMANI VIDUMISHWE

Image
   Na Allan Kitwe, DmNewsonline                    TABORA  ASKOFU wa Kanisa la TAG Jimbo la Tabora Kati na Kiongozi wa Kanisa la Kitete Christian Centre (KCC) la Mjini Tabora Rev. Paul Meivukie ameomba upendo, haki na amani viendelee kudumishwa nchini ili jamii iishi kwa utulivu. Ametoa rai hiyo leo kwenye ibada ya sikukuu ya krismas ambapo ameeleza kuwa krismasi ni tukio kubwa linalobeba ujumbe wa upendo, haki na amani kwa watu wote, hivyo mamlaka na jamii kwa ujumla hawana budi kuyadumisha. Amesisitiza kuwa tunapoadhimisha sikukuu hii ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo hatuna budi kumwomba Mungu ili taifa liendelee kuwa na amani na utulivu na upendo na haki viendelee kudumishwa wakati wote ili Mungu aliinue taifa lake. ‘Taifa liliingia kwenye wakati mgumu sana Oktoba 29, 2025 siku ya uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, hili halipaswi kufumbiwa macho, kama taifa tunapaswa kusameheana na kupendana ili kudumishwa amani yet...

MSTAHIKI MEYA TEMEKE: UVUMILIVU WANGU UTAKUWA SIFURI KWA MTU ATAKAYECHELEWESHA UKAMILIFU WA MIRADI.

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsonline              DAR ES SALAAM MEYA wa Manispaa ya Temeke, jijini Dar es Salaam,  Uzairu Athumani, amesema atakuwa na uvumilivu sifuri kwa mkandarasi  atakayechelewesha ukamilishaji wa miradi ya maendeleo.                 Akizungumza ofisini kwake, Meya Uzairu alisemaatakayeshindwa kutekeleza mradi kwa wakati uliopangwa atachukuliwa hatua kwa haraka.        Meya huyo amesema atakuwa na uvumilivu sifuri kwa mkandarasi atakayepewa mradi wa kujenga miundo mbinu akiwamo barabara na kujenga chini ya kiwango.     "Kwa mkandarasi yeyote atakayeshindwa kukamilisha mradi kwa wakati atachukuriwa hatua haraka sana," amesema Meya Uzairu.     Meya Uzairu amesema hatakuwa na uvumilivu hata kidogo kwa mkandarasi atakayejenga barabara chini ya kiwango na miradi mingine na kuhaiidi kufuatilia  kwa  karibu mno kuhakiki...

DKT. PIMA AAGIZA WAKUU WA SHULE KUSIMAMIA NIDHAMU

Image
   Na Allan Kitwe, DmNewsonline                     TABORA   WALIMU Wakuu wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Manispaa Tabora wameagizwa kusimamia ipasavyo nidhamu za walimu na wanafunzi katika shule zao ili kuinua juu taaluma.   Agizo hilo limetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa hiyo Dkt John Pima alipokuwa akifunga semina maalumu ya Maafisa Elimu, Walimu wa Nidhamu, Waratibu na Wakuu wa shule zote mjini hapa. Amesema kuwa serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan imefanya maboresho makubwa ya miundombinu katika shule zote za Manispaa hiyo hivyo kuboreshwa mazingira ya ufundishaji na kujifunza. ‘Mazingira bora yaliyopo katika shule zetu ni chachu muhimu ya kuwezesha watoto wetu kufanya vizuri zaidi katika mitihani yao ya kitaifa hivyo kuongeza ufaulu katika manispaa yetu, katika hili ni lazima tuimarishe nidhamu’, ameeleza. Dkt.Pima ameahid...

WAJASIRIAMALI WA MKOA WA DAR ES SALAAM WAMEWATAKA WATANZANIA KULINDA AMANI

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsonline            DAR ES SALAAM  UMOJA wa Wajasiriamali wa Mkoa wa Dar es Salaam umewataka Watanzania wote kujiepusha na vitendo vya vurugu vinavyoweza kuliingiza taifa katika uvunjifu wa amani, wakisisitiza kuwa machafuko hayaleti tija wala suluhu ya changamoto za kijamii na kiuchumi. Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari Leo Desemba 24,2025, viongozi na wanachama wa umoja huo wamesema wanapinga vikali wito wowote unaotolewa na wanaharakati wa ndani na nje ya nchi wanaohamasisha vurugu kwa maslahi yao binafsi, huku wakilitumbukiza taifa kwenye machafuko na hofu. Wajasiriamali hao wamesema wamefuatilia kwa karibu matukio ya vurugu yaliyotokea Oktoba 29, 2025 na kubaini kuwa kulikuwa na watu waliokuwa nyuma ya pazia wakihamasisha vitendohivyo.Wamesisitiza kuwa wamewashtukia na wanapinga vikali mienendo hiyo hatarishi. “Matukio ya Oktoba 29 yametosha kuwa somo. Tumeshuhudia athari zake na tumejifunza kuwa uvunjifu wa amani ha...