JENISTA MHAGAMA NYOTA ILIYOZIMIKA GHAFLA.
Timothy Marko, DmNewsnline Jenister Mhagama ni Mwanasiasa maarufu kutoka Tanzania ambaye amehudumu kwa miaka mingi katika uongozi wa Serikali na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Marehemu Mhagama alizaliwa Juni 23, 1967 katika Wilaya ya Songea Mjini, Mkoani Ruvuma Nchini Tanzania. Jenister Alipata Diploma ya Ualimu kutoka chuo Cha ualimu wilaya ya Korogwe (Teachers Training College)mkoani Tanga na aliwahi kufanya kazi kama mwalimu kabla ya kuingia kwenye siasa. Jenista Mhagama kifo chake kimetokea leo Desember 11,2025 akiwa bado ni mmoja wa viongozi wakubwa wa taifa, na taarifa ya kifo chake ili tangazwa rasmi na Bunge na vyombo vya habari nchini Tanzania Jenista Mhagama alikuwa Mbunge na kiongozi ndani ya Serikali kabla ya awamu hii alikuwa wa afya wa Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania . Pia marehemu Jenister alikuwa mstari wa mbele katika masuala ya sera, afya, ajira, vi...