Posts

Showing posts from August, 2025

DK.MWINYI:CCM ITAFANYA KAMPENI ZA KISTAARABU KWA SERA ZENYE TIJA KWA WANANCHI

Image
 Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                 ZANZIBAR RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) na kuahidi kuwa CCM itafanya kampeni za kistaarabu zitakazozingatia Utamaduni, Silka na Desturi za Wazanzibari. Dkt. Mwinyi amechukua fomu hiyo katika Afisi za Tume ya Uchaguzi leo, tarehe 30 Agosti 2025, asubuhi, na hatimaye msafara wake ukaelekea Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui kupitia Barabara ya Miembeni, Kariakoo, Rahaleo na Michenzani, akisindikizwa na mamia ya wanachama wa chama hicho waliokuwa wamejipanga pembezoni mwa barabara. Aidha, Dkt. Mwinyi amezuru Kaburi la Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume, na kisha kuzungumza na Wazee wa Chama Cha Mapinduzi afisini hapo. Akizungumza na mamia ya wanachama wa CCM katika Uwanj...

MGOMBEA URAIS KUNJE NA MGOMBEA MWEZA WAKE AAFP KUZINDUA KAMPENI KIHOMBOHOMBO MOROGORO AGOSTI 31

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline          DAR ES SALAAM  CHAMA cha Wakulima(AAFP) kinapenda kuwataarifu wananchi na wanachama wake,vyombo vya habari kuwa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 zitafanyika  Kihombohombo Vijijini Mkoa wa Morogoro Agosti 31,,2025 kuanzia saa nne  asubuhi hadi saa 12:00 Jioni Katika uzinduzi huo,Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kunje Ng'ombale Mwiru  pamoja na mgombea Mwenza Chumu Abdallah Juma wanatarajiwa kuhutubia wananchi na kueleza kwa kina sera na vipaumbele vya Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha AAFP kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu. Aidhaa ,viongozi wakuu wa chama,wagombea ubunge ,na wagombea wa udiwani kutoka mikoa mbalimbali nchini watashiriki katika tukio hilo kubwa la kihistoria na la kisiasa pamoja na wasanii mbalimbali wa bongo fleva watakupo Wakazi wote wa Mkoa wa Morogoro na mikoa ya Jirani  mnakaribishwa kuhudhuria kwa wingi katika uzinduzi huo wa kampeni ili kupata ...

AMEIR MGOMBEA URAIS ZANZIBAR KUPITIA CHAMA CHA MAKINI MGENI RASMI UZINDUZI WA KAMPENI SEPT,2

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline           DAR ES SALAAM  CHAMA cha Makini kinapenda kuwataarifu wananchi na wanachama wake,vyombo vya habari kuwa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 zitafanyika  katika Viwanja vya Bakhresa Manzese Jijini Dar es Salaam Septemba 2,2025 kuanzia saa nane kamili mchana na mgeni rasmi katika uzinduzi ni Ameir Hassani Ameir Mgombea Urais wa Serikali ya Mapunduzi Zanzibar kupitia Chama cha Makini Katika uzinduzi huo,Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Coaster Kibonde pamoja na mgombea Mwenza,Azza Haji Suleiman wanatarajiwa kuhutubia wananchi na kueleza kwa kina sera na vipaumbele vya Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Makini kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Mwaka huu. Aidhaa ,viongozi wakuu wa chama,wagombea ubunge ,na wagombea wa udiwani kutoka mikoa mbalimbali nchini watashiriki katika tukio hilo kubwa la kihistoria na la kisiasa. Wakazi wote wa Jiji la Dar es Salaam na mikoa ya Jirani  mnakaribishwa kuh...

MDAU WA MAENDELEO IRINGA MJINI NDUGU SUFIAN MGUDE AKABIDHI KITUO CHA POLISI ,RC JAMES ATIA NENO.

Image
        Na Eliasa Ally DmnewsOline             IRINGA JUMLA ya shilingi milioni 58 zimetumika katika ujenzi wa kituo Cha Polisi kilichojengwa katika Kata ya Mseke Tanangozi wilaya ya iringa mjini chini ya ufadhili wa mdau wa maendeleo Sufian Mgude . Akizungumza katika uzinduzi wa kituo hicho kilichojengwa na mdau wa maendeleo wilayani humo Sufian Mgude ,mkuu wa mkoa wa Iringa Kheri James amempongeza mdau huyo nakusema kwamba amefanya jambo jema kwa kukumbuka alikotoka. Amesema kuwa uwepo wa kituo hicho karibu utasaidia kupunguza viendo vya uhalifu kwani awali ilikuwa wanafuata huduma mbali na eneo hilo hivyo jambo kubwa kwa wananchi ni kushirikiana na Jeshi la Polisi na pia kuacha kujichukulia sheria mkononi. "Nakupongeza sana ndugu Mgude kwani ulichofanya ni kitu kikubwa na wachache sana wanakumbuka walikotoka lakini wewe licha ya kuishi nje ya mkoa wa Iringa lakini bado umekumbuka kuunga mkono Serikali katika kuhakikisha wananchi wetu ...

NAIBU KATIBU MKUU AAFP NA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA MTUMBA AIPONGEZA INEC

Image
      Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline              DODOMA NAIBU Katibu Mkuu wa Chama Cha Wakulima (AAFP), Mark Isdory Mhemela ameipongeza Tume Huru ya Uchaguzi(INEC) kwa kusimamia vizuri zoezi la uteuzi wa wagombea kuanzia ngazi ya Urais,Ubunge na Udiwani. Akizungumza kwa njia ya simu mapema asubuhi Agosti 29,2025 amesema kwamba yeye kama mgombea wa nafasi ya Ubunge ,ameona jinsi INEC walivyofanikisha zoezi Hilo kwa ufanisi kwani wagombea wote wameteuliwa bila tatizo lolote. "Naipongeza Serikali kupitia Tume Huru ya Uchaguzi kwa kuwapatia  usafiri wagombea wa nafasi ya Urais ,hii ni mara ya kwanza kwa kujali",amesema Mhemela Aidha,amesema kwamba anatarajiwa kuanza kampeni Septemba 5,2025 katika Jimbo la Mtumba Jijini Dodoma,hivyo amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi kupitia chama chake. Pia, amewataka vijana,wazee na wanawake wenye mapenzi mema na AAFP kwa kushiriki kwa wingi katika Uzinduzi huo wa kampeni kwa kuwa...

RASMI KIPENGA KIMELIA VUMBI KUTIMKA KWA MIEZI MIWILI KAMPENI ZA UCHAGUZI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline       DAR ES SALAAM  SHAMRASHARA za Uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika viwanja vya Tanganyika Packers Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti, 2025. Katika uzinduzi huo wa kampeni pia ulihudhuliwa na wagombea ubunge akiwemo mgombea Ubunge Jimbo la kilindi mkoani Tanga mh.Sarehe Mhando .

CCM YAZINDUA KAMPENI RASMI DAR ES SALAAM LEO

Image
Na Mwandishi wetu, DmNewsonline        DAR ES SALAAM MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika viwanja vya Tanganyika Packers Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Agosti, 2025.   

KIKWETE:UTEUZI WA SAMIA UEZINGATIA TARATIBU ZA KIKANUNI

Image
    Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                  DAR ES SALAAM  MWENYEKITI mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jakaya Kikwete amesema mchakato wa kumteua mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho Dkt. Samia Suluhu Hassan ulifuata utaratibu wa siku zote, na kwamba kwa wale walioona mchakato huo haukufuata taratibu hawafahamu taratibu za chama hicho. Dkt. Kikwete amesema hayo wakati akitoa salamu katika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi za CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, unaofanyika katika Viwanja vya Tanganyika Packers jijini Dar es Salaam. Amesema anashangaa kuona watu wanabeza uteuzi huo wakati wengine walishiriki katika michakato ya teuzi za wagombea wa awamu zilizopita ambao unafanana na mchakato uliofuatwa kwa awamu hii. Dkt. Kikwete ametumia jukwaa hilo kumpongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutekeleza kwa kishindo miradi mbalimbali iliyoachwa na mtangulizi wake Hayati Dkt...

Dkt. JAFARI ASHIRIKI UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM DAR ES SALAAM

Image
        Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                   DAR ES SALAAM  MGOMBEA  ubunge wa Jimbo la Busanda kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Jafari Rajabu Seif, amehudhuria uzinduzi wa kampeni za chama hicho uliofanyika leo, Agosti 28, 2025, katika viwanja vya Tanganyika Packers, jijini Dar es Salaam. Uzinduzi huo umefanyika sambamba na kuanza rasmi kwa kampeni za uchaguzi kwa vyama vyote vya siasa, kwa mujibu wa ratiba ya Tume Huru ya Uchaguzi (INEC).  Tarehe hii inaashiria mwanzo rasmi wa harakati za kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Dkt. Jafari ni miongoni mwa wagombea walioteuliwa na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho katika majimbo mbalimbali nchini, yeye akiwakilisha Jimbo la Busanda lililopo Wilaya ya Geita  mkoani Geita. Uzinduzi huo umeonesha nguvu ya CCM katika maandalizi ya uchaguzi, na umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama, wagombea wa nafasi za udi...

SERIKALI YAWATAKA WATUNZA NYARAKA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU

Image
Na Timothy Marko, DmNewsonline            DAR ES SALAAM SERIKALI imewataka watumishi wa umma wanaoshughulika na utunzaji wa nyaraka kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na kuzingatia matumizi ya mifumo ya kisasa ya kidijitali ili kulinda taarifa nyeti za taifa. Wito huo umetolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, wakati wa kufungua Mkutano wa 13 wa Chama cha Menejimenti ya Kumbukumbu na Nyaraka (TRAMPA) uliofanyika jijini Dar es Salaam. Amesema utunzaji wa nyaraka za Serikali ni uti wa mgongo wa maendeleo ya taifa, hasa kuelekea Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050. “Watunza nyaraka ni wasimamizi muhimu wa dira ya maendeleo ya taifa letu. Serikali ya Awamu ya Sita inalenga kuhakikisha nyaraka zote za serikali zinatunzwa kwa usahihi, usalama, usiri na kwa kutumia mifumo ya kidijitali,” amesema Waziri Mkuu Majaliwa. Aidha, amesisitiza kuwa mifumo ya utunzaji nyaraka isomeane kwa njia ya mtandao ...

ACT WAZALENDO WAKIMBILIA MAHAKAMANI KUPINGA MAAMUZI YA INEC

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsOnlie            DAR ES SALAAM  CHAMA Cha ACT Wazalendo kimeamua kukimbilia Mahakamani kwenda kupinga maamuzi ya Tume Huru ya Uchaguzi(INEC) kutokana na kumuondoa mgombea wao wa nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Luhaga Mpina ambaye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ilibaini mapungufu ya kisheria  na kikanuni kuhusiana na uyeuzi wake,mapungufu yanayompotezea sifa za kuwa mgombea halali wa chama hicho. Akizungumza na waandishi wa habari Leo Agosti 27,2025 Jijini Dar es Salaam,Mwanasheria Mkuu wa Chama hicho Omar Said amesema kwamba ACT Wazendo haikubaliani na maamuzi hayo kutokan na kile walichodai kuwa yamefanywa kinyume na Sheria na Katiba. "Tume Huru ya Uchaguzi(INEC) haina mamlaka kisheria kumiengua mgombea yoyote wa nafasi yoyote kwa kufuata maelekezi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ama taasisi youote ,badala yake mtu au taasisi inaruhusiwa kuweka mapingamizi kwa mgombea inayemtilia shaka,"amesema ...