Na Mwandishi wetu,DmNewsonline KOROGWE_TANGA NI Katibu Mkuu (Mstaafu) Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Katibu Mkuu (Mstaafu) Wizara ya Maliasili na Utalii, Mkurugenzi Mkuu (DG), na Kamishna wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), sio mwingine bali ni Dkt. Allan Kijazi. Ameonesha nia ya kuendelea kuwatumikia wananchi kupitia Mhimili mwingine wa Bunge baada ya kumaliza kazi, tena iliyotukuka kwenye Mhimili wa Serikali. Ametangaza nia kutaka kuwa Mtumishi wa Wananchi kama Mbunge wa Jimbo la Korogwe Mjini mkoani Tanga. Ana uwezo, ni msikivu, mchapa kazi na mwenye maono. Anafahamu maendeleo makubwa yaliyofanywa na Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo huduma za jamii (Elimu, Afya na Maji). Lakini pia shughuli za maendeleo kwa mtu mmoja mmoja, vikundi na Taifa. Hivyo, yeye anataka kuendeleza pale ambapo watangulizi wake wamefikia il...
Comments
Post a Comment