Posts

Showing posts from July, 2025

SEKTA YA KILIMO YAINUA MAISHA YA WAKAZI KASULU

Image
  Na Allan Kitwe,DmNewsonline               KASULU HALMASHAURI ya Mji Kasulu ni miongoni mwa halmashauri 8 za Mkoa wa Kigoma ambapo asilimia 80 ya wakazi wake wanaishi Vijijini na shughuli kuu ya kiuchumi katika maeneo hayo ni kilimo. Maboresho makubwa ya sekta ya kilimo yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan yameleta tija kubwa kwa wakazi wa halmashauri hiyo na Wilaya nzima ya Kasulu. Akiongea na gazeti hili hivi karibuni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Vumilia Simbeye ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka 4 ya uongozi wa Rais Samia, halmashauri hiyo imepiga hatua kubwa kimaendeleo kupitia sekta hiyo. Amebainisha mambo yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita ambayo yamechochea mafanikio makubwa kwa wakazi wa halmashauri hiyo kuwa ni kuongezwa bajeti, ugawaji mbolea ya ruzuku na kutafuta masoko ya kutosha. Haya yamepelekea wakazi wengi wa halmashauri hiyo kuchangamkia sekta ya kilimo hali a...

ESTER JEMSI AWAOMBA KURA WANACHIKOBE NA NYACHILULUMA, AAHIDI KUJA NA MFUKO MAALUMU WA KUSAIDIA WANAFUNZI WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU

Image
  Na Mwandishi wetu, DmNewsonline                      GEITA            MGOMBEA  wa ubunge Jimbo la Katoro kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ester Jemsi, amewaomba wanachama wa chama hicho katika kata za Bukondo na Nyachiluluma kumpa ridhaa ya kuwa mbunge wao, akiahidi kuwa ataleta maendeleo yenye tija kwa wananchi wa jimbo hilo. Akizungumza mbele ya wajumbe wa CCM kwenye kata hizo, Ester amesema ana ndoto kubwa ya kulifanya Jimbo la Katoro kuwa eneo la kuvutia kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, endapo atapewa nafasi ya kuliongoza. "Naomba niaminiwe. Nina ndoto ya kuona Katoro inabadilika, na nina nia ya dhati kuhakikisha wananchi wananufaika na rasilimali zao," amesema Ester. Ester Jemsi amebainisha kuwa moja ya mipango yake ni kuanzisha mfuko maalumu wa kusaidia wanafunzi wanaoishi katika mazingira magumu, akisema tayari alikuwa akitekeleza mpango huo akiwa kiongozi wa vijana, lakini sas...

SIMBA YAINGIA MKATABA MNONO WA SHILINGI BILIONI 20 NA BETWAY

Image
  Timothy Marko DmNewsonline              DAR ES SALAAM  KLABU ya Simba Sports Club Nchini Tanzania imeingia mkataba wa Shilingi bilioni 20 wa miaka mitatu na Kampuni ya Ubashiri ya michezo hususani Mpira wa miguu ya  Betway. Akizungumza naWaandishi wa Habari Jijini katika Hafla ya makabidhiano ya Hundi ya Mkataba huo Mjumbe wa bodi ya wa kurugenzi  Klabu ya Simba Salimu Abdallah Muhene  Try Again amesema Makubaliano hayo ya udhamini kati ya Betway na Klabu ya Simba unalenga kukuza jina la timu hiyo kitaifa na Kimataifa. "Kampuni yoyote inapenda kushirikiana na  Kampuni yenye hadhi Kimataifa yenye nguvu,Sisi kama Simba tutahakikisha tunailinda Brand hii ya Betway" Amesema Try again.  Try again Ameongeza kuwa Katika Mkataba huo kutakuwa na Uwazi ili kuhakikisha pande zote mbili zina nufaika na Mkataba huo. Amesisitiza kuwa nivyema wapenzi na Mashabiki wa timu ya Simba kuhakikisha wanakuwa wa moja ili kuweza kuiletea Ma...

SIGRADA MLIGO:NIMEONDOKA CHADEMA, KIMEKOSA MWELEKEO WA KUKIONDOA CCM MADARAKANI.

Image
  Timothy Marko DmNewsonoine              DAR ES SALAAM ALIYEKUWA KATIBU Mwenezi wa Baraza la Wanawake Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA SIGRADA MLIGO amesema Ameondoka Chama hicho na kujiunga na Chama cha Umma ,Baada ya  CHADEMA kukosa Dhamira ya dhati ya kukiondoa Chama cha Mapinduzi CCM Madarakani Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam SIGRADA MLIGO amesema kuwa Chama cha Mapinduzi CCM Wana akiili ya Kisiasa,hivyo inahitaji jitihada za dhati za kuking'oa Chama hicho Madarakani. "Ili Uweze kuking'oa Chama cha Mapinduzi CCM Madarakani lazima Ukifanye Chama cha Mapinduzi CCM kisilale " Amesema SIGRADA MLIGO.  MLIGO Ameongeza kuwa amekuwa akishutumiwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuwa anakihujumu Chama hicho. Amesisitiza kuwa Amekuwa na Imani na Mwenyekiti wa Chama hicho Tundu Lisu kuwania Urais lakini Kumekuwa na sitofahamu Juu ya Hatima yake. "Nimekuja Chauma kuungana na kuungana na KATIBU Mkuu w...

Aweso Apongeza Usimamizi Mradi wa Maji Chato Uliofikia 53%, Wananchi Waomba Uharakishwaji

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                  GEITA  WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amewapongeza wasimamizi wa mradi wa maji wa miji 28 unaoendelea kutekelezwa wilayani Chato kwa usimamizi mzuri, huku akieleza kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji ambao kwa sasa umefikia asilimia 53. Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua mradi huo, Waziri Aweso alisema hatua iliyofikiwa ni ya kutia moyo na kuonyesha dhamira ya dhati ya serikali ya kuwapatia wananchi huduma bora ya maji safi na salama. Katika ziara hiyo, wananchi wa Kijiji cha Mkungo, Kata ya Mkome, waliiomba serikali kupitia Wizara ya Maji kuharakisha utekelezaji wa mradi huo ili kuondokana na adha ya upatikanaji wa maji safi inayowakumba kwa muda mrefu. Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Chato (CHAWASA), Aisaki Mgeni, alieleza kuwa mradi huo unatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 41 hadi kukamilika, na utaongeza uzalishaji wa maj...

Aweso Apongeza Usimamizi Mradi wa Maji Chato Uliofikia 53%, Wananchi Waomba Uharakishwaji

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                  GEITA  WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amewapongeza wasimamizi wa mradi wa maji wa miji 28 unaoendelea kutekelezwa wilayani Chato kwa usimamizi mzuri, huku akieleza kuridhishwa na maendeleo ya utekelezaji ambao kwa sasa umefikia asilimia 53. Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua mradi huo, Waziri Aweso alisema hatua iliyofikiwa ni ya kutia moyo na kuonyesha dhamira ya dhati ya serikali ya kuwapatia wananchi huduma bora ya maji safi na salama. Katika ziara hiyo, wananchi wa Kijiji cha Mkungo, Kata ya Mkome, waliiomba serikali kupitia Wizara ya Maji kuharakisha utekelezaji wa mradi huo ili kuondokana na adha ya upatikanaji wa maji safi inayowakumba kwa muda mrefu. Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Chato (CHAWASA), Aisaki Mgeni, alieleza kuwa mradi huo unatarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 41 hadi kukamilika, na utaongeza uzalishaji wa maj...

KIWANDA CHA XINGHAO GROUP COMPANY LTD (LULU CEMENT) CHAKABIDHI MADAWATI 200 NA FEDHA MILIONI 3 KWA AJILI YA SHULE YA MSINGI MISUGUSUGU

Image
  Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                       KIBAHA KIWANDA cha XINGHAO GROUP COMPANY LTD ( LULU CEMENT)  kimekabidhi madawati 200 yenye thamani ya shilingi milioni 33, pamoja na shilingi milioni 3 kwa ajili ya ununuzi wa fenicha za walimu katika Shule ya Msingi Misugusugu, iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha, mkoani Pwani msaada wenye thamani ya TSH milioni 36. Msaada huo umetolewa kwa lengo la kutatua changamoto ya uhaba wa madawati na samani kwa walimu, ili kuimarisha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji shuleni hapo. Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Meneja wa kiwanda hicho, Wan Jianguo, amesema kuwa kiwanda hicho kmeanza shughuli zake katika eneo hilo mwaka jana, na walipofanya ziara shuleni hapo walibaini changamoto mbalimbali, ikiwemo uhaba  wa madawati licha ya serikali kuwa imejenga miundombinu bora. “Tumeona ni wajibu wetu kama wawekezaji kushiriki kuboresha mazingira...

MAONESHO YA KILIMO KANDA YA MAGHARIBI KUFANYIKA TABORA AGOSTI 1-8

Image
Na Allan Kitwe, DmNewsonline                  TABORA  TAASISI mbalimbali, wadau wa maendeleo na wakazi wa Mikoa ya Tabora, Kigoma na Mikoa jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi katika maonesho ya wakulima nane nane Kanda ya Magharibi ambayo yanatarajiwa kuanza Agosti 1-8. Hayo yamebainishwa leo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora Dk. John Mboya alipokuwa akiongea na vyombo vya habari Ofisini kwake ambapo alibainisha kuwa maonesho ya mwaka huu yamesheheni mambo mengi mazuri. Amesema kuwa maonesho hayo ya sikukuu ya wakulima hufanyika kila mwaka hapa nchini na kwa Kanda ya Magharibi yanafanyika katika Viwanja vya Nane Nane Ipuli Mjini Tabora na kushirikisha Mikoa miwili ya Tabora na Katavi. Dkt. Mboya amefafanua kuwa maonesho hayo yenye kauli mbiu isemayo ‘Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi: Viongozi Bora ndiyo msingi wa maendeleo. Ametaja taasisi zilizoshiriki maonesho ya mwaka jana kuwa ni za sekta ya ...