Posts

Showing posts from July, 2025

MKUU WA CHUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE ATEMBELEA SABASABA

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline            DAR E SALAAM  MKUU wa Chuo Cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere(MNMA) ,Prof.Haruni Mapesa ametembele Banda la Chuo katika Maonesho ya 49 Kimataifa ya Biashara(SABASABA) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K.Nyerere  Jijini Dar es Salaam. Prof.Mapesa ametembelea Leo Julai 3,2025 na pia ametumia nafasi hiyo kuwakaribisha  watanzania kujitokeza kwa wingi kutembelea Banda lao  ili kupata historia ya chuo na kujionea bunifu mbalimbali zinazofanywa na wanafunzi. Aidha ,amesema Chuo cha MNMA kinahistoria ndefu kilianzishwa na Mwalimu Nyerere mwezi Julai 29, 1961 miezi michache kabla yakupata uhuru. Pia ameeleza kwamba Chuo kilianzishwa kwa lengo la kuandaa viongozi wa Tanzania ambao wameongoza baada yakupata uhuru. "Chuo hiki kimepewa jina la Mwalimu Nyerere  kwa ajili ya kumuenzi mwalimu kwa juhudi kubwa yakuwaelimisha watanzania lakini pia kuokoa nchi ya Tanzania",amesema Hata hivyo, a...

JIMBO JIPYA LA KIVULE WAGOMBEA WAPISHANA .MAAMUZI YAPO KWA WAJUMBE.

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline                 DAR ES SALAAM  WAKATI zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu kwa Watia Nia wa Ubunge, katika majimbo manne ya Wilaya ya Ilala, likihitimishwa, kwa Jumla ya Wagombea 84 Kati ya 87 waliochukua fomu hizo kuzirejesha.  Hali ya joto la kinyang'anyiro hicho kwa wagombea katika Jimbo jipya la Kivule imezidi kuongezeka. Kujitokeza kwa Komredi Brendan Maro, Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa na Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Tanzania (TUGHE) kunatajwa  kuongeza uganzi kwa watia nia wengine katika mchuano huo. Komredi Maro, ambaye ni Mkazi wa Tawi la Kitundakati, Kata ya Kitunda, ni kada aliyelelewa ndani ya chama na hivyo kujipatia uzoefu was kiuongozi ndani na nje ya Chama cha Mapinduzi, ambako alianza kukitumikia akiwa Chipukizi wa chama cha Mapinduzi, huko wilayani Kilombero.  Katika Uchaguzi Mkuu wa 2005, Komredi Maro alikuwa mmoja wa Waratibu wa kun...

MA-DC TATUENI KERO ZA WANANCHI...

Image
    Na Allan Kitwe,DmNewsonline               TABORA WAKUU wapya wa Wilaya walioteuliwa hivi karibuni na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika Mkoa wa Tabora wametakiwa kuwa karibu zaidi na wananchi, kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi ili kumaliza kero zinazowakabili. Wito huo umetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Paul Chacha alipokuwa akimwapisha Mkuu wa Wilaya ya Sikonge, Thomas Myinga na wa Tabora Mjini Upendo Wella katika ukumbi wa Mtemi Isike Mwanakiyungi mjini hapa. Amesema kuwa kila mteule wa Rais aliyeletwa katika Mkoa huo amekuja kuhudumia wananchi, si vinginevyo, hivyo anapaswa kuwa karibu zaidi na wananchi, kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi. Ili kufanikisha utekelezaji majukumu yao kwa tija amewataka kushirikiana kwa karibu zaidi na viongozi wa kiroho, watumishi walio chini yao, taasisi za umma na zisizo za umma, mashirika na wadau wote wa maendeleo. RC Chacha amesisitiza kuwa Mheshimiwa Rais ana imani kubwa na ...

TAWA YAWAKARIBISHA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LAO KATIKA MAONESHO YA SABASABA

Image
Na Angelina Mganga,DmNewsOnline ‎                ‎DAR ES SALAAM  ‎ ‎MAMLAKA ya Wanyamapori Tanzania(TAWA) inawakaribisha watanzania kutembelea Banda lao katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara(SABASABA) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K.Nyerere Jijini Dar es Salaam. Hayo yamebainishwa Leo Julai 3,2025 na Afisa Muhifadhi TAWA, ‎Dkt. Gladstone Mlay wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Banda la TAWA amesema kwamba  kwa mwaka 2024 jumla ya watalii Milioni 5.3 wametembea hifadhi za Taifa ambapo watalii wa ndani milioni 3.2 na watilii  wa Kimataifa milioni 2.1 wamepita katika maeneo mbalimbali yanayosimamiwa na Mamlaka hiyo. Aidha ,Afisa Muhifadhi Mlay ameeleza kwamba TAWA imekusanya shilongi  bilioni 3.9 ambazo zimechangia kwa kiasi kikubwa kukuza Pato la Taifa. Pia amesema watalii wanapotembelea kwa wingi wanatoa fursa kwa wananchi kwa kuuza bidhaa mbalimbali katika maeneo yanayozungukwa na hifadh...

TIRDO YAJA KIVINGINE MAONESHO YA SABASABA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline      DAR ES SALAAM  SHIRIKA  la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) wamewataka wananchi kutembelea Banda lao katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara(SABASABA) yanaoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere  Jijini Dar es Salaam . Hayo yamebainishwa leo Julai 3,2023 na Mtaalam wa Nishati ,Ali Moh'd Rashid wakati akizungumza na waandishi wa habari amesema kwamba wamekuja na tafiti mbali  mojawapo ni utaalam juu ya matumizi bora ya nishati .    Amesema kuwa matumizi bora ya nishati ni kutumia nishati kwa namna ambayo inapunguza upotevu wa nishati na kufikia matokeo sawa na bora bila kuathiri utendaji. Aidha ,ameeleza kwamba inapaswa kufanya ukaguzi wa mifumo ya nishati Kila baada ya muda ili kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima. Pia,amesema kwamba kutumia vifaa vinavyotumia teknolojia za kisasa ambazo zinatumia nishati kwa ufanisi mfano Taa za LED. Sanjarari na hayo, Mtaalamu Rashid ...

RC KUNENGE :DAWASA FANYENI TASIMINI UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI.

Image
Na Mwandishi wetu ,DmNewsonline           KIBAHA  Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kufanya tathmini ya kina ya utekelezaji wa miradi ya maji kwa kuzingatia changamoto halisi zinazowakabili wananchi katika maeneo mbalimbali. Kunenge alitoa wito huo leo, Julai 2, 2025, wakati akifungua kikao kazi cha kupokea na kujadili mipango na mikakati ya DAWASA kwa mwaka wa fedha 2025/2026, kilichofanyika katika ukumbi wa Destiny, Kibaha kwa Mathias, mkoani Pwani. Amesisitiza kuwa tathmini yoyote ya miradi lazima itokane moja kwa moja na maoni ya wananchi pamoja na viongozi , badala ya kutegemea taarifa za ripoti peke yake ambazo mara nyingine hazioneshi uhalisia wa mambo. “Tujitahidi kupata tathmini kutoka kwa wananchi na viongozi. Itakuwa ni jambo la kusikitisha kuwa na tathmini nzuri ilhali wananchi hawaridhishwi. Tathmini bora ni ile inayotoka kwa wananchi,” alisema Mhe. Kunenge. Amesis...

WATIA NIA 84 WARUDISHA FOMU ZA UBUNGE WILAYA ILALA

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsOnline         DAR ES SALAAM  WAGOMBEA 84 waliochukua fomu za kutia nia katika nafasi ya  Ubunge  wamerejesha fomu za Ubunge Wilaya ya Ilala katika majimbo  manne ambayo ni Ilala,Segerea,Ukonga na Kivule. Akizungumza na waandishi wa habari  Leo Julai 2,2025 Jijini Dar es Salaam Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala Chief Sylvester Yaredi amesema mchakato wa kuchukua fomu na kurudisha fomu dirisha limefungwa saa kumi kamili . Aidha, amesema kwamba  katika zoezi hilo wagombea 87 waliochukua fomu   na Wagombea  84 ndio waliorudisha fomu. Katibu wa wilaya Yared alisema katika jimbo la Kivule wamechukua fomu 46 wamerejesha 44,Jimbo la Segerea wamechukua 18,wamerejesha 17,Jimbo la ukonga wamechukua 11 na wamerejesha 11,na Jimbo la Ilala wamechukua 12 na wamerejesha 12.   

MSHINYANGA ARUDISHA FOMU YA UDIWANI KATA YA IBOLOGERO

Image
    Na Tunu Nassir,DmNewsonline                 IGUNGA. ALIYEKUWA  Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi kata ya Ibologero wilaya ya Igunga,mkoa wa Tabora, Ally Mshinyanga amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kugombea udiwan. Mshinyanga ambaye amehudumu nafasi ya uenyekiti wa kata hiyo  kwa muda wa  miaka nane.  Hapo awali Mshinyanga aliwahi kuwa mwenyekiti wa vijana tawi la Ibologero. Pia mwaka 2007/ 2012 Mshinyanga amekuwa katibu hamasa CCM wa kata hiyo. Akizungumza baada ya kurejesha fomu Mshinyanga amesema amechukua uamuzi huo kwa lengo la kuisaidia kata hiyo kupata maendeleo ya haraka. "Ibologero in raslimali nyingi invitation msukumo kidogo tu wa kiuongozi kupata maendeleo," amesema.

KADA CCM ABUBAKAR OMARY ARUDISHA FOMU YA UBUNGE JIMBO LA MANONGA.

Image
Na Tunu Nassir,DmNewsonline                  IGUNGA  KADA wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abubakar Omary amerudisha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Manonga wilaya ya Igunga mkoani Tabora.  Abubakari anakuwa miongoni mwa wagombea kumi akiwamo mbunge anayemaliza muda wake Seif Gulamali.

SALMIN NCHIMBI ACHUKUWA FOMU YA UDIWANI ,MWEMBESONGO Na

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                MOROGORO ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti Chipukizi (CCM) wilaya Ya Morogoro Mjini na Mjumbe wa Baraza Kuu (Uvccm) Taifa - Kuiwakilisha Chipukizi,Salmini Nchimbi amechukua fomu leo ya kugombea nafasi ya Udiwani katika Kata ya  Mwembesongo,wilaya ya Morogoro Mjini Mkoa wa Morogoro. Salmini ni miongoni mwa vijana wachache waliamua kugombea nafasi hiyo katika Kata ya Mwembesongo.    

CCM ILIVYOJIPAMBANUA KWA VIJANA ,NA NAMNA VIJANA WANAVYOJENGA TAIFA.

Image
               MAKALA      Na Mwandishi wetu,DmNewsonline KATIKA  historia ya taifa letu, vijana wamekuwa mstari wa mbele katika harakati za kisiasa, kijamii na kiuchumi. Kuanzia mapambano ya kupigania uhuru hadi ujenzi wa taifa jipya, mchango wa vijana hauwezi kupuuzwa. Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejidhihirisha kuwa ni chama pekee chenye imani ya kweli kwa vijana—kikiwa kinawashirikisha, kinawajenga, na kuwawezesha kuwa viongozi wa sasa na kesho.  MISINGI YA HISTORIA: VIJANA WALIVYOJENGA TAIFA Ushahidi wa kwanza wa mchango wa vijana katika historia ya taifa letu ni kuanzishwa kwa TANU na ASP na viongozi vijana kama Mwalimu Julius Nyerere akiwa na umri wa miaka 32, na Rashid Kawawa akiwa na miaka 28. Hawa waliamini kwamba nguvu ya kijana ni msingi wa mabadiliko, na kweli walileta mapinduzi yaliyowezesha Tanganyika kupata uhuru mwaka 1961. Tangu kuanzishwa kwa CCM tarehe 5 Februari 1977, chama kimeendelea kurithi misingi h...

CCM ILIVYOJIPAMBANUA KWA VIJANA ,NA NAMNA VIJANA WANAVYOJENGA TAIFA.

Image
               MAKALA      Na Mwandishi wetu,DmNewsonline KATIKA  historia ya taifa letu, vijana wamekuwa mstari wa mbele katika harakati za kisiasa, kijamii na kiuchumi. Kuanzia mapambano ya kupigania uhuru hadi ujenzi wa taifa jipya, mchango wa vijana hauwezi kupuuzwa. Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimejidhihirisha kuwa ni chama pekee chenye imani ya kweli kwa vijana—kikiwa kinawashirikisha, kinawajenga, na kuwawezesha kuwa viongozi wa sasa na kesho.  MISINGI YA HISTORIA: VIJANA WALIVYOJENGA TAIFA Ushahidi wa kwanza wa mchango wa vijana katika historia ya taifa letu ni kuanzishwa kwa TANU na ASP na viongozi vijana kama Mwalimu Julius Nyerere akiwa na umri wa miaka 32, na Rashid Kawawa akiwa na miaka 28. Hawa waliamini kwamba nguvu ya kijana ni msingi wa mabadiliko, na kweli walileta mapinduzi yaliyowezesha Tanganyika kupata uhuru mwaka 1961. Tangu kuanzishwa kwa CCM tarehe 5 Februari 1977, chama kimeendelea kurithi misingi h...

HALMASHAURI YA MANISPAA YA KIBAHA YAFANYA KIKAO KAZI KUIMARISHA UWAZI NA UWAJIBIKAJI KAZINI

Image
Na Mwandishi wetu,DmNewsonline                      KIBAHA   HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imefanya kikao kazi maalum kilichowakutanisha Maafisa Kilimo na Maafisa Maendeleo ya Jamii wote, kwa lengo la kukumbushana wajibu wa kila siku katika kutekeleza majukumu yao ya kiutumishi. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Kibaha, kikilenga kuimarisha utendaji kazi, uwajibikaji, ubunifu katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha, Dkt. Rogers Shemwelekwa, amewataka watumishi wote kuongeza ubunifu katika kazi zao, kuachana na kufanya kazi kwa mazoea, na kuhakikisha mapato ya ndani yanakusanywa kikamilifu kwa maendeleo ya Halmashauri na wananchi wake. “Ni lazima tuwe wabunifu katika kila tunalolifanya. Tusifanye kazi kwa mazoea. Wananchi wanategemea huduma bora kutoka kwetu, na sisi ndiyo daraja la utekeleza...